Thursday, November 29, 2012

 Na Lucas Raphael.Tabora

Makala.

Januari 16 mwaka huu ni siku ya kukumbukwa katika mkoa wa Tabora, kutokana na mkoa huo kuandika historia mpya katika nyanja ya elimu nchini. Mkoa huo umeweza kupata Chuo kikuu cha Kwanza toka Tanganyika ilipopata uhuru wake mwaka 1961.

Kwa muda mrefu Mkoa wa Tabora haukuwa na vyuo vinavyotoa elimu ya juu hapa nchini hali ambayo iliufanya mkoa huo ushindwe kupata ustawi mkubwa wa kimaendeleo ikilinganishwa na mikoa mingine, ambayo ina vyuo vikuu.

Mkoa huo ulikuwa na vyuo vinavyotoa elimu ya kati tu kama vyuo vya Ualimu ambavyo ni chuo cha Ualimu Ndala, wilayani Nzega na Chuo cha Ualimu cha Tabora ambavyo vilianza kutoa huduma hiyo kwenye miaka ya sitini na sabini.

Ukiondoa vyuo hivyo vyuo vingine vilivyopo ni Chuo cha Utumishi wa Umma, Chuo cha Ardhi na chuo cha kilimo Tumbi na vyuo vya ufundi vya VETA na vituo vidogo vidogo vya utoaji wa elimu mbali mbali ndivyo vilivyokuwa vikifanyakazi ya kuwaelimisha wakazi wa Tabora katika fani Tofauti.

Kabla ya vyuo hivyo Mkoa wa Tabora, ulikuwa ukisifika sana kutokana na kuwa na shule mahiri za sekondari ambazo ziliweza kuchangia maendeleo ya taifa hili kikamilifu na kwa ushindani uliostahili.

Shule hizo ni Pamoja na Tabora Boys, Milambo sekondari, Tabora Girls, Kazima ambazo kwa pamoja zimetoa wataalam wengi zaidi hapa nchini pamoja na viongozi wa serikali.

Hata hivyo kukosekana kwa elimu ya chuo kikuu katika mkoa wa Tabora, kumeufanya mkoa huo uliokuwa ukisifika kielimu hapa nchini upoteze umaarufu wake wa miaka mingi na kujikuta ukiwa miongoni mwa mikoa isiyokuwa tena na sifa ya kufanya vizuri katika nyanja hiyo muhimu kwa maisha ya binadamu.

Chuo hicho kikuu kilizinduliwa na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Samuel Sitta, ambaye ndiye aliyekuwa mgeni rasmi katika sherehe hizo za uzinduzi zilizofanyika katika uwanja wa Chipukizi mjini hapa.

Katika hotuba yake waziri Sitta, alisema kuwa hiyo ni hatua kubwa ya maendeleo katika mkoa wa Tabora, ambao alisema umekuwa nyuma kwa muda mrefu na hivyo kuufanya usiwe miongoni mwa mikoa yenye maendeleo makubwa kielimu hapa nchini.

Alisema kuwepo kwa chuo hicho ni maendeleo ya kweli kwa mkoa na kuwataka wakazi wa mkoa huo kuwa makini na kushiriki katika utoaji wa mazingira mazuri na kuwapa ushirikiano watumishi, wahadhiri na wanafunzi ili kuongeza sifa za mkoa huo katika elimu ya juu nchini.

Aliilaumu bodi ya mikopo Tanzania kutokana na kushindwa kuweka mazingira mazuri ya utoaji wa mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu nchini huku akibainisha wazi kuwa utendaji katika bodi hiyo umejaa urasimu.

Alisema pamoja na Urasimu, bodi hiyo imekuwa ikifanyakazi zake kwa chuki, upendeleo, dhulma na kufanya mambo mengine ambayo hayakubaliki katika utoaji wa elimu ya juu hapa nchini.

Alisema kunahaja ya kufanya mabadiliko makubwa katika bodi hiyo ili utendaji wake uwe na tija kwa watanzania wanaotafuta elimu ya juu nchini ili waweze kuja kulitumikia taifa katika nyanja mbali mbali.

Alisema suala hilo atalifikisha serikalini kwa ajili ya kutafutiwa ufumbuzi wa kina ambao utasaidia kuboresha utendaji katika bodi ya mikopo nchini ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kuwa watoto wa watanzania wananufaika zaidi na mikopo hiyo ya kielimu.

Akizungumza katika Ibada maalum ya ufunguzi wa chuo hicho Askofu mkuu wa kanisa Katoliki Jimbo kuu la Tabora, Mhasham Paul Ruzoka, alisema kuwa elimu ni kitu muhimu kwa maisha ya binadamu na kudokeza kuwa Kanisa katoliki linapenda kutoa huduma hiyo kwa watanzania wote pasipokuwa na ubaguzi wa aina yeyote.

Alisema elimu ni kama Mwanga unaomuwezesha mtu yeyote kuona na kufanya shughuli mbali mbali za kimaendeleo na kijamii hapa nchini, huku akisema kuwa kinyume na elimu ni ujinga ambao unafananishwa na giza nene ambalo linamzuia binadamu kufanya kazi mbali mbali za maendeleo.

Askofu alisema ni wajibu wa kila mtu kuhakikisha kuwa anapata elimu ili aweze siyo tu kuishi vizuri bali pia kuishi maisha ambayo yatamsaidia kumjua na kumthamini Mungu ambaye ndiye aliyejalia vipawa vya kila namna kwa binadamu.

Alisema kwa kuwa Kanisa katoliki linatambua umuhimu wa jambo hilo litaendelea kutumia fursa zilizopo ili kuweza kuendelea kuwasaidia wananchi waweze kupata fursa hiyo muhimu kwa maendeleo ya umma na kuondoa ubabaishaji katika utoaji wa huduma za kijamii miongoni mwa watanzania.

Askofu mkuu aliwahimiza waumini wa kanisa hilo na wale ambao si waumini kukitumia vizuri chuo hicho kikuu kwa ajili ya manufaa ya kijamii na kudokeza kuwa lengo la kanisa ni kuhakikisha kwamba ustawi wa watu unakuwabora zaidi kadri miaka inavyoongezeka.

Akizungumza mara baada ya ibada hiyo maalum ya kufungua chuo kikuu cha Archbishop Mihayo university College of Tabora ( AMUCTA) ambacho kitakuwa chuo kikuu kishiriki cha mtakatifu Augustine cha Jijini Mwanza (SAUT) Makamo mkuu wa chuo hicho nchini Dk. Charles Kitima, alisema ni muhimu watoto wa Tanzania wakinufaika na elimu ya juu.

Alisema katika siku za karibuni kumeibuka mtindo wa viongozi wa kiserikali kuweka vikwazo kadha wa kadha kwa wanafunzi wa vyuo vikuu wanaosoma katika vyuo binafsi wasipatiwe mikopo na kwamba wanafunzi watakaopewa mikopo ni wale wanaosoma katika vyuo na taasisi za serikali pekee.

Alisema kauli hiyo ilipingwa vikali na wakuu wa vyuo binafsi kwa sababu si haki kufanya hivyo na kwamba vyuo vya elimu ya juu vya binafsi vimeanzishwa kwa ajili ya kuisaidia serikali iweze kupata wataalam wengi zaidi.

Kulingana na Dk. Kitima, serikali haiwezi kuwasomesha wanafunzi wote waliomaliza elimu ya kidato cha sita na kufaulu mtihani kwahiyo ni vyema ikashirikiana na vyuo vikuu vya binafsi vinavyowapatia vijana elimu hiyo muhimu kwa maendeleo ya Taifa.

Alisema ni vyema basi serikali ikajitahidi kuondoa kero hizo ndogo ndogo zinazowakabili wanafunzi hasa katika sekta ya mikopo kwani alisema bodi ya mikopo nchini imekuwa ikionekana kama kikwazo kwa watoto wa wakulima kupata elimu ya juu nchini Tanzania.

Alisema mikopo ni haki yao na kwamba wananchi wanapaswa kujua na kutambua kuwa suala la utoaji wa elimu ya juu nchini ni la lazima na ni haki yao ya kimsingi watoto wao kuipata elimu hiyo muhimu kwa ustawi wa taifa hili.

Alisema jamii ya wasomi itaendelea kupinga sera mbovu ambazo hazina tija kwa taifa letu na kubainisha kuwa jamii hiyo itaendelea kufanya utafiti utakaosaidia kuimarika kwa elimu nchini ikiwa ni njia pekee ya kupambana na tatizo la kuwa na wataalam wasiokuwa na sifa zinazotakiwa.

Mkuu wa chuo kikuu cha Askofu Mkuu Mihayo cha Tabora ( AMUCTA) Dk. Thadeus Mkamwa, alisema kuwa chuo hicho kikuu kimeanza rasmi novemba 3 mwaka jana, kwa kuanza na mafunzo ya shahada ya kwanza ya Ualimu kikiwa na wanachuo 886.

Alisema kutokana na mikakati ya chuo hicho kinatarajia kuanzisha pia shahada za masomo ya sayansi ya jamii, biashara na sheria ambayo yanatarajia kuleta mapinduzi mazito katika suala zima litakalosaidia maendeleo ya Taifa hili.

Alisema pamoja na kuanza fani hizo, alisema katika mipango ya muda mfupi chuo hicho kitaanza kutoa mafunzo ya elimu ya juu katika fani hizo kwa watu wa makundi maalum ambao ni walemavu kama wasiosikia, wasiosema na wenye matatizo tofauti.

Alisema kwa mujibu muongozo wa chuo hicho, kinapaswa kuwa na wanachuo wasiopungua 5000 kitakapokamilika kimejikita zaidi katika ufundishaji wa masomo ya juu kwa kiwango kizuri na bila ya kusahau suala zima la maadili ya umma.

Alisema kampasi ya chuo hicho inatarajia kujengwa katika eneo la Kazima, umbali kama wa kilomita nane kutoka mjini Tabora, ambapo kazi ya kulipa fidia kwa wananchi waliokuwa wakimiliki eneo hilo ikiwa inaendelea.

Aliwataka wakazi wa Tabora kuwatambua na kuwathamini wanafunzi wa chuo hicho, hasa pale wanapotafuta makazi kwa ajili ya kusoma wasiwapandishie bei kwa kudhani kwamba wanapesa za kutosha hivyo kuwakwamisha kufikia malengo yao ya kielimu.

Alisema hao ni watoto wa masikini kama wao hivyo wanachopaswa kukifanya ni kuwasaidia na si kuwakomoa kwani kama tujuavyo kuwepo kwa wanachuo kutasaidia pia kukuza maendeleo katika mji huo kwa sababu mzunguuko wa pesa utaongezeka katika mji huo.

Mkuu wa Chuo, aliwataka wanachuo kusoma kwa bidii kubwa na kuhakikisha kuwa wanapata taaluma bora zaidi itakayowasaidia kupata uelewa mkubwa utakaosaidia kuwapa ushindani na kumudu kufanyakazi mahali popote katika ulimwengu bila ya kuathiri mila na desturi za wenyeji wao.

Sherehe hizo za ufunguzi wa chuo hicho zimehudhuriwa na maelfu ya wakazi wa mji wa Tabora, viongozi wa chama Tawala na serikali, wabunge, maaskofu wa majimbo mbali mbali nchini na mapadri wanaoziwakilisha jumuiya mbali mbali katika jimbo Kuu la Tabora.

Mwisho.

WEKEZENI ELIMU KWA WATOTO WENU MWASSA


Na Lucas Raphael ,Tabora 

wekezini kwenye elimu ya watoto

Wazazi na walezi mkoani Tabora wametakiwa kuwekeza kwenye elimu ya watoto wao kwa kufanya hivyo watakuwa wamewapata urithi wa pekee watoto wao ,urithi huo ni mzuri kuliko mali .

Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa mkoa wa Tabora Fatuma Mwassa wakati wa mahafali ya kwanza ya shule ya msingi ya Istiqaama inayomilikiwa na taasisi ya kiislamu ya Istiqaama yaliyofanyika katika viwanja vya shule hiyo jana .
 
Alisema kwamba kuwekeza kwenye elimu kutawasaidia watoto wetu kuwa na akili ya kutafuta elimu na mali hata baada ya wazazi wao kuwa hapo duniani,kwani tumeona watu wengi wanawashia watoto mali lakini mali hizo zinatumiwa na watu wengine na watoto wanazidi kuteseka .

Alisema kwamba familia nyingi zimekuwa zitafuta mali bila kuwekeze kwa elimu ya watoto wao na mwisho wa siku watoto wanakosa elimu na mali walizoziacha kwani wanadhulumiwa na wale waliwaacha kusimamia mali hizo .

Mwassa alisema kwamba iwapo wazazi watawaachia elimu watoto wao ni vizuri na hakuna mtu wa kudhurumu elimu hiyo zaidi ya mtoto huyo kuitumia kwa maufaa yake na taifa kwa ujumla .

Alisema kwamba hakuna mtu  ambaye hajui umuhimu wa elimu kwa maana hiyo kila mtoto anatakiwa kupata elimu iliyobora kwa ajili  ya kukabiliana na soko la ajira.

Hata hivyo mkuu huyo wa mkaow a Tabora alifanikisha kuongoza harambee na kuichangia kiasi cha shilingi milioni 25,fedha zilizopatikana zitasaidia kukamilisha ofisi na madarasa ya wanafunzi  

Katika mahafali hayo watoto 42 wa eli mu wa hawali walipatiwa vyeti kwa ajili ya kujiunga na darasa la kwanza mwakani.

Awali shekhe wa mkoa wa Tabora Shabani Salum aliwataka wakazi wa mkoa wa tabora kuwekeza mkoani hapa tofauti  na watu wengine ambao wanawekeza katika mkoa wanayotoka .

Alisema kwamba imekumekuwe[po kasumba ya baadhi ya watu hasa wa mkoa huu kushindwa kuwekeza katika mkoa wao na kuwekeza katika mikoa mingine ,aliomgeza kuwekeza huo sio tatizo bali na msisahua kwenu.

Mwisho

WAZIRI WA HABARI AFUNGUA MKUTANO WA MA-RAS JIJINI DAR


Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara akifungua Mkutano baina ya Baraza la Michezo la Taifa (BMT) na wajumbe wa Kamati za Michezo za Mikoa Tanzania Bara “Ma-RAS” (hawapo pichani) Jijini Dar es Salaam.Mkutano huo unalengo la kujadili maendeleo ya Michezo nchini.
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara akisalimiana na RAS wa Njombe mara baada ya kufungua kufungua Mkutano baina ya Baraza la Michezo la Taifa (BMT) na wajumbe wa Kamati za Michezo za Mikoa Tanzania Bara Ma-RAS Jijini Dar es Salaam.Mkutano huo unalengo la kujadili maendeleo ya Michezo nchini. (Picha na Benjamin Sawe wa WHVUM).

WAKALA WA NISHATI YA UMEME JUA WATOA MAFUNZO

Na Lucas Raphael,Tabora.

WANANCHI waishio Vijijini wameshauriwa kuungana majirani wawili mpaka Watatu kulingana na umbali uliopo ili kuwa na nguvu ya pamoja ya kuweza kumudu kununua vifaa vya kutengenezea Mfumo wa Nishati ya umeme wa Jua ili kuondokana na adha ya kuishi gizani.

Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Tabora Suleiman Kumchaya katika Hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Katibu Tawala wa Wilaya hiyo Ignas Kabale wakati wa kufunga mafunzo ya Mafundi wa Nishati ya umeme wa Jua yalifanyika katika shule ya sekondari ya Nkumba mjini hapa.

Mkuu huyo wa wilaya  anawashauri Wananchi majirani kuungana ili kumudu gharama za vifaa vya Nishati ya umeme wa Jua kwani kwa kufanya hivyo kutapunguza uharibifu wa mazingira unaosababaishwa na ukataji wa miti hovyo.

Alisema kwamba kupatika na umeme jua utawaonzea wananchi wa vijijini tija na afya kwani kutumia tena kuni kutapungua na afya zao zitakuwa bora na mazingira yatakuwa mazuri .

Hata hivyo alisema kwamba kitendo cha wakala wa nishati wa umeme jua vijijini kufunga umeme huo katika jingo la shule ya nkumba kutasaidia wanafunzi kufanya vizuri katika masomo yao.

Alisema kipindi shule hizo za kutwa zinaanza mazingira yake yalikuwa ni magumu sana lakini kwa sasa shule hizo na iwapo hostel zitajengwa katika shle huyo kusaidia sana wanafunzi wa shule.

Wahitimu wa Mafunzo ya ufundi wa Nishati ya umeme wa Jua kutoka vijiji mbali mbali vya Mkoa wa Tabora walipatiwa na Wakala wa Nishati ya umeme wa Jua Vijijini kwa lengo likiwani kuwajengea uwezo Wananchi wa kutengeneza na kueneza wenyewe Nishati hiyo vijijini .

Aidha alisema kwamba mafunzo hayo yamefanyika kwa Nadharia na Vitendo, ambapo Zahanati mbili na shule moja ya Sekondari katika Manispaa ya Tabora zimewekewa mfumo wa Nishati hiyo.

Mafunzo hayo ya siku kumi yaliwahusisha Vijana 17 kutoka maeneo mbali mbali ya vijiji vya Mkoa wa Tabora wakiwemo  Wanafunzi wa Vyuo vya ufundi stadi (VETA) ambao watatumika kueneza Teknojia hiyo kwa Wananchi katika Vijiji vyao.

 MWISHO

WADAU WA TAKWIMU NCHINI WAKUTANA KATIKA KONGAMANO LA PILI LA MWAKA JIJINI DAR LEO

 Mkurugenzi wa Takwimu nchini, Morrice Oyuke, akisoma hotuba yake kumwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa  TAKWIMU nchini Dkt.. Albina Chuwa, wakati wa kongamano la pili la mwaka la wadau wa TAKWIMU nchini lililofanyika leo jijini Dar es Salaam. 
 Mwakilishi kutoka Benki ya Dunia, Thomas Danielewitz, akitoa hotuba yake  leo jijini Dar es Salaam katika ufunguzi wa kongamano la pili la mwaka kwa  Wadau wa Takwimu nchini.  Kongamano hilo la siku moja limefunguliwa na Naibu Waziri wa Fedha Dkt. Saada M. Salum (hayupo Pichani).
 Baadhi ya washiriki  wa kongamano la pili  la mwaka unaowashirikisha  Wadau wa Takwimu nchini  wakimsikilza Naibu Waziri wa Fedha Dr. Saada M. Salum (hayupo pichani) katika ufunguzi wa kongamano hilo leo jijini Dar es Salaam.
 Naibu wa Wizara ya Fedha Dkt. Saada M. Salum akifungua kongamano la pili la mwaka kwa wadau wa Takwimu nchini leo jijini Dar es Salaam., ambapo amewasisitiza  wadau kutumia takwimu zilizo  sahihi. Picha na Mwanakombo Jumaa- MAELEZO

SERIKALI YAZINDUA BARAZA LA WATAALAM WA KUREKEBISHA UPEO WA MACHO KUONA,PIA YAKABIDHI MAGARI 9 NA PIKIPIKI 107 KUSAIDIA HUDUMA ZA AFYA NCHINI


Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Hussein Mwinyi akizungumza na wajumbe wa Baraza la Wataalam wa Kurekebisha Upeo wa Macho Kuona nchini leo jijini Dar es salaam.
Mwenyekiti wa Baraza la wataalam wa kurekebisha upeo wa macho kuona nchini Adam Simbeye (kulia) akiwaeleza wajumbe malengo ya baraza hilo ya kusimamia, kudhibiti na kuratibu utoaji wa huduma bora za macho nchini yanayofanywa na baraza hilo kwa mujibu wa sheria ya Optometria Na.12 ya mwaka 2007. Kushoto ni Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Hussein Mwinyi.
Wajumbe wa Baraza la Wataalam wa Kurekebisha Upeo wa Macho Kuona nchini wakiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Hussein Mwinyi (Katikati) mara baada ya kuzinduliwa kwa baraza hilo leo jijini Dar es salaam.
Waziri wa Afya na Ustawi wa jamii Dkt. Hussein Mwinyi (kushoto) na mwakilishi wa Shirika la UNFPA nchini Tanzania Bi.Mariam Khan (kulia) kwa pamoja wakisaini nyaraka za kukabidhi magari 9 ya kubebea wagonjwa na pikipiki 107 kwa ajili ya kupelekwa katika maeneo mbalimbali kusaidia huduma za afya.
Mwakilishi wa Shirika la UNFPA nchini Tanzania Bi.Mariam Khan (kulia) akimkabidhi funguo za gari la kubebea wagonjwa Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Hussein Mwinyi leo jijini Dar es salaam.
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Hussein Mwinyi (kushoto) akimkabidhi funguo za gari la kubebea wagonjwa mganga mkuu wa hospitali ya wilaya ya Bukombe Dkt.Archard Rwezahura (katikati) leo jijini Dar es salaam. Anayeshuhudia makabidhiano hayo ni mwakilishi wa Shirika la UNFPA nchini Tanzania Bi.Mariam Khan.Picha na Aron Msigwa - MAELEZO.

UZINDUZI WA TUSKER LITE NDANI YA USIKU WA MAAFISA MASOKO

Mkurugenzi Masoko wa Kampuni ya bia ya Serengeti (SBL), Epraim Mafuru akizungmza mara baada ya uzinduzi wa bia mpya ya Tusker Lite wakati wa uzinduzi wake rasmi uliofanyika mbele ya maafisa masoko wa makampuni mbalimbali nchini wakati wa tafrija maalum ya ‘Markerts Night’ jijini Dar es Salaam jana.
Baadhi ya wafanyakazi wa Kampuni ya bia ya Serengeti (SBL) wakifuatilia matukio mbalimbali wakati bia mpya ya Tusker Lite ilipozinduliwa sanjari na usiku maalum wa maafisa masoko jijini Dar es Salaam jana
Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL), Epraim Mafuru (mwenye suti kushoto) akimkabidhi zawadi ya Tusker Lite, Meneja bidhaa wa Push Mobile, Gonzoga Rugambwa  baada ya kuibuka mshindi wa kwanza wa shindano maalum la uchezaji mziki lililofabnyika wakati wa uzinduzi wa bia ya Tusker Lite sanjari na usiku wa maafisa masoko jijini Dar es Salaam jana.
Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya bia ya Serengeti (SBL), Steve Gannon akinyanyua juu bia mpya ya Tusker Lite wakati wa uzinduzi wake rasmi uliofanyika mbele ya maafisa masoko wa makampuni mbalimbali nchini wakati wa tafrija maalum ya ‘Markerts Night’ jijini Dar es Salaam jana
Vijana wa sarakasi wakionesha ufundi wao wakati wa tafrija ya maalum ya Maafisa masoko na uzinduzi wa bia mpya ya Tusker Lite inayozalisha na kusambazwa na Kampuni ya Bia ya Serengeti.

Wednesday, November 28, 2012

MAELFU YA WATU WAMZIKA MSANII SHARO MILIONEA KIJIJI KWAO MKOANI TANGA


 Nape akimpa pole Zaina Mkieli Mama wa Hussein Ramadhani, Sharo Milionea, Kijiji cha Lusanga, Muheza Tanga
Baadhi ya wasanii msibani, Lusanga
DC Muheza, Subra Mgalu akisoma salam za EOTF ya Mama Mkapa
Baadhi ya wasanii msibani, Lusanga
 Nape (Watatu kulia, waliobeba jeneza) akishiriki kubeba jeneza lilipofika Lusanga, nyumbani kwa marehemu
 Nape akitoa pole za Chama kwenye mazishi hayo
 Nape akitupa udogo kaburini wakati wa mazishi ya Sharo Milionea, Lusanga, Tanga
 Waombolezaji wakaimsaidia mwenzao aliyepoteza fahamu msibani
 Mwili wa SharoMilionea ukiswaliwa
 Mzee Kingi Majuto akitupa mchanga kaburinu kumzika Sharo Milionea
 Nape, Rais wa Bongo Movies Simon Mwakifwamba, Meneja mahusiano wa kamuni ya Airtel,Jackosom Mbando wakisubiri mwili wa marehemu kuwasili nyumbani Lusango, Muheza.
Msanii wa muziki wa kizazi kipya a.k.a Bongofleva Hamis Mwinjuma a.k.a Mwana FA akitoa salam kwa niaba ya Wanamuziki wa Bongofleva.
Kutokana na Umati wa Watu kuwa mkubwa wengine ilibidi wapande juu ya minazi ili kushuhudia safari ya mwisho ya Ndugu yetu Sharomilionea.Picha kwa Hisani ya jiachie Blog

EVANS BUKUKU COMMENDY CLUB YAWASHIKA WAKAZI WAPENZI WAKE NDANI YA NYUMBANI LOUNGE, DAR


  Mshereheshaji Taji Liundi akiongoza jahazi ndani Commedy live ambayo hufanyika kila mwishoni mwa mwenzi ndani Nyumbani Lounge jijini Dar.
...Kila mmoja yupo busy akifuatilia onyesho.
Mchekeshaji wa kundi la VUVUZELA ENTERTAINMENT linalosimamiwa na Evans Bukuku, Raymond akionyesha makeke yake, katika onyesho lao ambalo hufanyika kila mwishoni mwa mwenzi ndani Nyumbani Lounge jijini Dar.
...Watu waliojitokeza wakijiachia kwa kicheko.
Mchekeshaji machachali wa kundi la Vuvuzela, DOGO PEPE akiwavunja mbavu wageni waliojitokeza katika onyesho lao.
Vicheko kila mahali maana DOGO PEPE alikuja kivingine ka kuwaacha watu hoi.
Mwanadada Enika nae alitoa burudani.
Watu waliojitokeza katika onyesho hilo.
Mchekeshaji mwalikwa kutoka nchini Kenya, Mdomo Bag akitoa burudani katika onyesho la Vuvuzela Entertainment ambalo hufanyika kila mwishoni mwa mwenzi ndani Nyumbani Lounge jijini Dar.
Missie Popular nae akikuwepo kutoka sapoti.
Mchekeshaji wa kundi la VUVUZELA ENTERTAINMENT, Evans Bukuku akionyesha makeke yake, katika onyesho lao ambalo hufanyika kila mwishoni mwa mwenzi ndani Nyumbani Lounge jijini Dar. Picha zote na Cathbert Angelo wa Kajunason Blog.

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AAGANA NA RAIS WA KENYA MWAI KIBAKI BAADA YA UFUNGUZI WA OFISI ZA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI, JIJINI ARUSHA JANA

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na Rais wa Kenya, Mwai Kibaki, ambaye ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, katika Uwanja wa Ndege  wa Kimataifa wa Kilimanjaro, mara baada ya ufunguzi wa Jengo la ofisi za Jumuiya hiyo iliyofanyika Jijini Arusha jana.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimsindikiza Rais wa Kenya, Mwai Kibaki, ambaye ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro, mara baada ya ufunguzi wa Jengo la ofisi za Jumuiya hiyo iliyofanyika Jijini Arusha jana.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipunga mkono kuwaaga wananchi baada ya kumsindikiza Rais wa Kenya, Mwai Kibaki, ambaye ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro, mara baada ya ufunguzi wa Jengo la ofisi za Jumuiya hiyo iliyofanyika Jijini Arusha jana.