Sunday, January 27, 2013

VIJIJI VYAPAYAN MAJI SAFI NA SALAMA NZEGA DC

 
 NA LUCAS RAPHAEL NZEGA

MKUU  wa Wilaya ya Nzega Mkoani Tabora Bituni  Msangi amsema huduma ya maji vijijini  imeboreshwa kwa kiasi kikubwa hadi hadi  kufikia  asilimia 40% kutoka  asilimia 36% mwaka 2005. 

Akizungumza na waandishi wa Habari  jana Ofisini kwake alisema huduma hiyo ya maji safi na salama imepatikana kwa kuchimba visima virefu vya maji pamoja na visima vifupi ambavyo vimechimbwa katika kata mbalimbali za wilaya hiyo. 

Alisema kuwa hapo awari wananchi waishio vijijini walikuwa wakipata shida kubwa ya maji kutokana na uhaba wa vyanzo vya maji  nakuongeza kuwa vijiji vilivyo bahatika kupata visima hivyo vya maji vitumie kwa uangalifu miradi hiyo . 

Msangi alisema kuwa  Richa ya kuwa na 40% ya upatikanaji wa maji safi vijijini bado kuna uhaba wa maji kwa baadhi ya vijiji ambapo serikali imejipanga kukabiliana na tatizo hilo ilikuhakikisha wananchi wanapata maji kwa asilimia 100% hasa kwa kukamilika mradi mkubwa wa maji kutoka ziwa Victoria hadi Tabora. 

Alibanisha kuwa katika miradi hiyo visima vilivyo chimbwa mwaka 2005 vilikuwa visima 472 ambapo mwaka 2012 visima hivyo vimefikia idadi ya 538 kati ya hivyo visima virefu ni 203 huku visima vifupi vikiwa 335. 

Amewataka wananchi wananchi wa wilaya ya Nzega kutuma visima hivyo kwa uangalifu ili kuepuka adha ya maji kwa musimu wa masika. 

Alisema serikali wialayani hapa imeweka sheria ndogo za kuhakikisha utunzaji wa vyanzo vya maji vinatunzwa pamoja na kuhakikisha wananchi wanapata Elimu ya maji safi na salama ili kila mwananchi apate kuelewa ikiwa na kutunza vyanzo vya maji. 

Msangi alisema kuwa upatikanaji wa maji mjini ni kwa asilimia 59% kwa mwaka 2005 ambapo mwaka 2012 upatikanaji wa mjini ulikuwa 61% huku upatikanaji huo wa maji kwa ukiwa ni 40% kwa mwaka 2012 wakati mwaka 2005 ulikuwa 36%. 

Mwisho.


Friday, January 25, 2013

BALOZI ZETU ZINAHITAJI KUJITEGEMEA:SPIKA MAKINDA


1Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda akiwasili kwenye Ubalozi wa Tanzania DRC na kusalimiana na watendaji wa ubalozi huo baada ya kupokelewa na Kaimu Balozi Mhe. Hemed Mgaza (kushoto) Spika Makinda ameandamana na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulizni na Usalama, Mhe. Mussa Azzan Zungu. Spika Makinda ameshauri kuwa wakati umefika kwa balozi zetu kuwezeshwa ili zijitegemee.
2Spika Anne Makinda akisalimiana na wafanyakazi wa Ubalozi
3Spika akisaini Kitabu cha wageni
4Makamu Mwenyekiti  Mhe. Zungu akisaini kitabu cha wageni
5Picha ya Pamoja na wafanyakazi
6Jengo la Ubalozi. Jengo hili lipo kando ya barabara kuu Kinshasa, eneo maarufu kwa biashara.
7
Wajumbe kaamati maalum wakiendelea na mkutano wa FP/ICGLR

KAMATI YA BUNGE YA VIWANDA NA BIASHARA YATEMBELEA VIWANDA VYA KONYAGI NA TBL DAR


 Mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Viwanda  na Biashara, Deo Sanga (kulia), akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanda cha Konyagi cha Tanzania Distilleries Limited (TDL), David Mgwassa,kuhusu utengenezaji wa konyagi kubwa wakati wa ziara ya kamati hiyo, kwenye kiwanda hicho, Dar es Salaam juzi.
 Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Viwanda na Biashara, wakiangalia uzalishaji walipotembelea kiwanda cha Konyagi cha Tanzania Distilleries Limited (TDL), Dar es Salaam
 Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Viwanda na Biashara, Mahamoud Mgimwa (kushoto) akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanda cha Konyagi cha Tanzania Distilleries Limited (TDL), David Mgwassa wakati wajumbe wa kamati hiyo walipotembelea kiwanda hicho Dar es Salaam.PICHA ZOTE NA KAMANDA WA MATUKIO BLOG
Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Viwanda na Biashara, wakiangalia uzalishaji walipotembelea kiwanda cha Konyagi cha Tanzania Distilleries Limited (TDL), Dar Es Salaam
 Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Viwanda na Biashara wakitembelea sehemu ya mitambo ya kujaza bia kwenye chupa katika kiwanda cha TBL, Dar es Salaam
 Meneja wa Kiwanda cha Bia cha Kampuni ya Bia Tanzania, Martine Calvin (kulia), akiwapatia maelezo kuhusu historia ya kiwanda hicho, wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Viwanda na Biashara, walipotembelea kiwanda hicho.

 Ofisa Uhusiano wa TBL, Doris Malulu (kulia) akiwakaribisha wajumbe wa kamati hiyo kwenye chumba cha mikutano tayari kupata taarifa ya utendaji wa kampuni hiyo.
 Mkurugenzi wa Miradi Maalumu wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Phocas Lasway akitoa maelezo jinsi ongezeko la kodi ya asilimia 25 lililovyoathiri uzalishaji wa kampuni hiyo.
 Mwenyekiti wa kamati hiyo, Mgimwa akielezea jinsi watakavyoshirikiana na TBL kutafuta ufumbuzi wa changamoto mbalimbali zinazikabili kampuni hiyo.Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Joyce Mapunjo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Joyce Mapunjo (kushoto), ambaye pia ni mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), akizungumza wakati wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Viwanda na Biashara walipotembelea kiwanda cha Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), juzi katika Makao Makuu kampuni hiyo, Dar es Salaam. Kutoka kulia ni Mjumbe wa kamati hiyo,  Ahmed Salum na Mahamoud Mgimwa ambaye ni mwenyekiti wa kamati hiyo.
 Mkurugenzi wa Maendeleo ya Wanachama na Mawasiliano wa CTI, Neema Mhondo akielezea jinsi Kikosi cha Zimamoto na Uokoaji kilivyopandisha kiholela ada kwa kampuni mbalimbali kutoka sh. 400,000 hadi milioni 7 kwa mwaka.
Wajumbe wa Kamati hiyo ya Bunge wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kumaliza ziara kiwandani hapo.PICHA ZOTE NA KAMANDA WA MATUKIO

Tuesday, January 22, 2013

POLISI TABORA WAPATA PIKIPIKI 13 KWA AJILI YA KUKABILIANA NA UHARIFU


 Kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora Acp Anthony Rutha akimkabidhi Pikipiki mkaguzi msaidizi wa Polisi Joseph Matui katika hafla fupi iliyofanyika kwenye ofisi ya Jeshi la Polisi mkoani Tabora.


Na Beatrice Masaki - Tabora

Jeshi la polisi mkoani Tabora limepokea pikipiki  13 kutoka kwa Inspekta Jenerali  Said Mwema zitakazosaidia harakati za kukabiliana na vitendo vya uhalifu   katika mkoa huo.

Akikabidhi pikipiki hizo kamanda wa polisi mkoa wa Tabora, ACP Anthon Rutha amesema kuwa,pikipiki hizo zitagawiwa kwa wakaguzi wa kila tarafa wa wilaya za Igunga ,Uyui,Urambo ,Sikonge,Nzega na Tabora mjini  kwa lengo la kusaidia ulinzi  na usalama wa wananchi.

 Kamanda huyo wa polisi wa mkoa wa Tabora ametoa  wito kwa wakaguzi wa kila tarafa kuzitumia pikipiki hizo  kwa malengo yaliyokusudiwa na si kuzitumia kwa matumizi binafsi na kuwataka wazitunze  vizuri kwani kwa kufanya hivyo , kunaweza kusaidia kudhibit uhalifu kwa wakati na kuimarsha amani mkoani hapa.

Akipokea pikipiki hizo kwa niaba ya  wakaguzi wa tarafa mkoani hapa mkaguzi wa polisi Joseph Matui wa tarafa ya Tabora kaskazini amesema kuwa, pikipiki hizo zitawasaidia kufika maeneo ambayo wananchi wanahitaji kujua mambo  mbalimbali ikiwa ni pamoja na  juu ya ulinzi na usalama wa mali zao.

 Matui  amewataka wananchi kuonesha ushirikiano kwa askari  jeshi la polisi  pindi wanapofika katika maeneo yao  na pika wawe tayari  kuwafichua wahalifu.

TAREFA YAHITAJI MSAADA WA WADAU WA SOKA TABORA


Na Lucas Raphael,Tabora

CHAMA cha soka mkoa wa Tabora,(TAREFA),kimewataka wadau na wapenzi wa
mchezo huo,kuweka uzalendo mbele na kuunga mkono jitihada
zinaazofanyika kuhakikisha timu ziliopo daraja kwanza zinafanikiwa
kuingia ligi kuu.

Mwenyekiti wa chama hicho,Yusuph Kitumbo alisema hayo wakati akiongea
na waandishi wa habari akibainisha mikakati iliyopo chini ya uongozi
wake ikiwemo mikakati ya kurejesha Tabora inarejesha hadhi ya mchezo
wa soka kama kipindi cha timu ya Mirambo.

Kitumbo alifafanua kuwa hivi sasa kwa kushirikiana na viongozi
wenzake,wanaweka mipango mizuri ili kupandisha timu moja ambayo
itawakilisha mkoa kwenye ligi kuu na kurejesha makali ya kipindi cha
miaka ya 1994.

Aidha mwenyekiti huyo aliingeza kuwa hivi sasa kuna timu mbili za
Rhino Rangers,na Polisi,na kwamba wanaweka mikakati mikubwa
kuhakikisha timu hizo zinzcheza ligi kuu mwakani.

“Nawaomba wapenzi na wadau wa mchezo wa soka mkoani Tabora,yakiwemo
mashirika na taasisi za fedha kuungana katika kufaniukisha malengo ya
uongozi wa TAREFA ili hapo baadaye mkoa wetu unakuwa na timu zaidi ya
moja ligi kuu.”alisema.

Alisema haya yote hayatafanikiwa endapo kutakuwa hakuna uzalendo
kuanzia ngazi ya uongozi wa soka wenyewe,wapenzi na wadau katika
kuinua soka mkoani Tabora.

Kitumbo aliongeza kuwa chini ya uongozi wake wamejipanga vyema ikiwemo
kualika timu kadhaa kuja Tabora kucheza na timu za Polisi na Rhino
Rangers ili kujenga uwezo wa timu hizo.

Kuhusiana na mikakati ya kiuongozi mwenyekiti huyo alisema
watahakikisha wanawaunganisha wana Tabora katika michezo kadhaa
ikiwemo soka ya wanawake na kuweza kuweka timu ya wanawake inayocheza
soka la kisasa.

Kwa upande wake mwakilishi wa soka upande wa wanawake mkoa wa
Tabora,mwalimu Janeth Kabeho, alisema amejipanga vyema kuhakikisha
anawawakilisha vyema wanawake kwenye mchezo huo.

Mwalimu Kabeho alioingeza kuwa hivi sasa anajipanga kujenga timu imara
ya wanawake kila wilaya na baada ya hapo ni kutafuta timu ya mkoa
ambayo itawakilisha Tabora kwenye mashindano mbalimbali.

Aliongeza kuwa hivi sasa amepata mipira 10 ambayo itatumika kwa timu
za wilaya na kwamba baada ya hapo anatarajia kutafuta vifaa vya mchezo
huo kwa wafadhili baada ya timu za wilaya zitakapopatikana.

MAPOKEZI YA JK NCHINI UFARANSA


c2
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikagua gwaride rasmi aliloandaliwa kwa heshima yake mjini Paris Ufaransa leo Januari 21, 2013 ikiashiria kuanza rasmi kwa ziara yake ya kiserikali ya siku tano nchini humo.
PICHA NA IKULU


c3
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikagua gwaride rasmi aliloandaliwa kwa heshima yake mjini Paris Ufaransa leo Januari 21, 2013 ikiashiria kuanza rasmi kwa ziara yake ya kiserikali ya siku tano nchini humo.
c4Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na mwenyeji wake Rais Francois Hollande wa Ufaransa katika Ikulu ya nchi hiyo maarufu kama Champs L’Elyesee (hutamkwa chanz elezee) jijini Paris leo Januari 21, 2013
c6
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na ujumbe wake akiwa katika maongezi rasmi na mwenyeji wake Rais Francois Hollande wa Ufaransa na ujumbe wake  katika Ikulu ya nchi hiyo maarufu kama Champs L’Elyesee (hutamkwa chanz elezee) jijini Paris leo Januari 21, 2013
c7
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisindikizwa na mwenyeji wake Rais Francois Hollande wa Ufaransa baada ya mazungumzo yao rasmi katika Ikulu ya nchi hiyo maarufu kama Champs L’Elyesee (hutamkwa chanz elezee) jijini Paris leo Januari 21, 2013
c9
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na mwenyeji wake Rais Francois Hollande wa Ufaransa wakiongea na wanahabari baada ya mazungumzo yao rasmi katika Ikulu ya nchi hiyo maarufu kama Champs L’Elyesee (hutamkwa chanz elezee) jijini Paris leo Januari 21, 2013
c11
Gari iliyomchukua Rais Jakaya Mrisho Kikwete ikiondoka Ikulu ya nchi hiyo maarufu kama Champs L’Elyesee (hutamkwa chanz elezee) jijini Paris leo Januari 21, 2013

MAAFA STENDI YA UBUNGO JIJINI DAR-ES-SALAAM


ubungo1 6ac3f
ubungo2 cc0a5
SEHEMU ya ukuta wa kituo cha mabasi ya kwenda mikoani cha Ubungo, jijini Dar es Salaam, leo alfajiri umeanguka na kuyaharibu vibaya magari zaidi ya ishirini yaliyokuwa yameegeshwa nje ya eneo hilo. Akizungumza na waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Charles Kenyela alisema kuwa idadi ya magari yaliyopatwa na ajali hiyo yanakadiriwa kufikia 24 ambapo watu watatu wanasemekana wamejeruhiwa.
ubungo3 3104f
ubungo4 27999
ubungo5 bb613
ubungo c5ed1

Monday, January 21, 2013

JK AWASILI UFARANSA KWA ZIARA YA SIKU TATU


1
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakiwa na mke wa Rais wa Mali Mama Touré Lobbo Traoré waliyekutana naye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Charles de Gaulle jijini Paris, Ufaransa, baada ya kuwasili tayari kuanza ziara ya kiserikali ya siku tatu.
1c37
Mama Salma Kikwete akiongea na mke wa Rais wa Mali Mama Touré Lobbo Traoré waliyekutana naye uwanja wa ndege wa Kimataifa Charles de Gaulle jijini Paris, Ufaransa, baada ya kuwasili tayari kuanza ziara ya kiserikali ya siku tatu.
2Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na mke wa Rais wa Mali Mama Touré Lobbo Traoré waliyekutana naye uwanja wa ndege wa Kimataifa Charles de Gaulle jijini Paris, Ufaransa, baada ya kuwasili tayari kuanza ziara ya kiserikali ya siku tatu.

UKOMBOZI WA TAIFA NI MUSOMA UTALII TABORA YAKAMILISHA MAJENGO YAKE .

 
 NA LUCAS RAPHAEL,TABORA

UKOMBOZI wa taifa letu kwa kizazi cha sasa na kijacho,  jambo la
msimngi zaidi ni elimu bora ni suala muhimu sana ambalo litasaidia
kuondokana na hali ya umasikini,maradhi na ujinga ambao umekithiri
miongozi mwa watanzania waliowengi kwa sasa.

Chuo cha musoma utalii,kilichopo mkoani Tabora, ni chuo

kilichosajiliwa na “NACTE” kinachoendesha mafunzo ya kozi mbalimbali
na kimekuwa kikitoa elimu inayolingana na hali halisi ya sasa ya
sayansi na teknolojia.

Aidha chuo hicho kimekuwa kikitoa mafunzo ua juu ya kozi kama vile

uongozaji wa  watalii,hotel management,uwalimu wa chekechea,
uandishi wa habari na utangazaji, secretarial na Computer hali
iliyopelekea kufanikiwa  kutoa wahitimu bora waliofanikiwa kuajiriwa
na kujiairi ili kwenda sanjari na changamoto za soko la ajira ndani na
nje ya nchi.

Mkurugenzi wa chuo cha Musoma Utalii tawi la Tabora, Shabani

Mrutu,alisema hayo wakati alipokuwa akifanya mahojiano maalumu na
gazeti hili ofisini kwake alisema chuo kimekuwa ni chuo cha  mfano wa
kuigwa,na kimbilio la wengi na hadi sasa chuo hicho kimeanza ujenzi
wake.

Alisema ujenzi huo umekamilika kwa asilimia 80, ambapo kutakuwa na

mabweni yanayoweza kuchukua wanafunzi zaidi 200,vyumba vya madarasa
10,jengo la utawala la ghorofa na maktaba ya  kisasa,jiko la
kisasa,ukumbi na sehemu za  mapumziko.

Alisema kuwa mkoa wa Tabora una vivutio vingi vya kitalii lakini

haviendelezwi ipasavyo hivyo ujenzi wa chuo mkoani hapa ni ukombozi
mzuri ambao utasaidia vivutio hivyo kuonekana na hatimaye kukuza secta
ya utalii mkoani Tabora.

Mrutu alifafanua zaidi kuwa chuo hicho kilianzishwa mwaka 2004 kikiwa

na wanafunzi 42 na sasa kuna wanafunzi 280,ambapo chuo kilikua chini
ya usimamizi VETA.

Aidha mkurugenzi huyo aliongeza kuwa chuo hadi sasa,kimesajiliwa na

kutambulika na NACTE kwa barua ya awali yenye kumb. Namba
NACTE/BA/77/465/605/Vol 1/9 usajili ambao ulianza mwaka 2012.

Anabainisha kuwa chuo kina matawi mengi nchini ili kuwafikia vijana

wengi zaidi kwa gharama nafuu sana.

Mafanikio toka 2004 hadi sasa kampasi ya Tabora.


Mrutu anabainisha kuwa mafanikio kwa tawi la Tabora,ni kuongezeka kwa

wanafunzi toka 2004 wanafunzi 42 hadi 280 mwaka 2012.

Akizungumzia mafanikio katika utoaji wa elimu katika chuo  hicho,

mkuu huyo wa chuo alisema wamejipanga vyema kutoa elimu bora na zaidi
chuo kina kwa kuenmdelea kuongeza walimu ambapo hadi sasa kuna waalimu
18 wenye sifa zinazotambulika kisheria.

Alisema ili kuweza kutoa elimu bora pia wanafunzi wa chuo hicho

wamekuwa wakienda mafunzo ya vitendo kulingana na kozi wanazosoma
katika mikoa mbalimbali hapa nchini


Mkurugenzi huyo anaongeza kuwa wanafunzi hupelekwa katika hotel kubwa

za kitalii,kampuni za uongozaji watalii ,TANAPA na kozi za ufundishaji
chekechea hupelekwa katika shule za kiingereza,wengine vituo vya radio
kwa wanafunzi wanaochukua masomo ya uandishi wa habari.

Alisema maeneo mengine ya kitalii wanafunzi hao hupelekwa kwenye

makumbusho ya Kwihara nje kidogo ya mji wa Tabora, sehemu ambayo
makumbusho hayo yana historia ya kipekee kwa mkoa na taifa kwa ujumla.

Akizungumzia muitikio wa wanafunzi  kujiunga na chuo ni mzuri kwani

kila wanapochukua wanafunzi kila muhula idadi huwa inaongezeka
kulingana mahitaji halisi,ambapo sifa zilizowekwa ni wanafunzi
waliohitimu kidato cha nne hadi cha sita.

Malengo na matarajio ya chuo.


Mkurugenzi huyo Shabani Mrutu, alisema chuo hadi sasa kinakamilisha

majengo yake tawi la Tabora,ambayo yanatarajiwa kukamilika ndani ya
miezi minne kuanzia sasa  ujenzi huo unatarajia kukamilika kwa gharama ya zaidi ya sh
milioni 800.

Alisema malengo mengine ni kusajili  kozi nyingi zaidi kwenda

NECTA,sanjari na kusajili chuo kiweze kutoa elimu ya juu kutokana na
kozi zilizopo.

Aidha malengo mengine ni kuweza kusajili wanafunzi watakaofikia

1000,kuongeza matawi nchini ili chuo kiweze kutoa huduma bora zaidi
kwa jamii tena kwa gharama nafuu na kutoa elimu bora yenye ushindani
katika soko la ajira.

Kuhusu changamoto zilizopo.


Kuhusu changamoto zilizopo mkurugenzi huyo alisema chuo kimekuwa

kikikabiliwa na changamoto kadhaa ambazo ni uelewa wa jamii katika
vyuo binafsi kwani imejengeka fikra potofu vyuo binafsi wahitimu huwa
hawawezi kupata ajira na kwamba fikra hizo ni potofu kwani vyuo
binafsi na vya serikali vina nafasi sawa ilimradi viwe na usajili
unaotambulika serikalini.

“Ipo dhana ya namna hiyo lakini tumekuwa tukijitahidi sana kutoa elimu

kwa wazazi na zaidi ufaulu na ksaidia wanafunzi kujiajiri na kuajiriwa
kumekuwa kukitusaidia kuondoa dhana hiyo potofu.” Alisema.

Alitaja changamoto nyingine kuwa uelewa mdogo wa wazazi juu ya kozi ya

“Hotel Management,” kuwa ni kozi ya kihuni kiasi cha kuleta wanafunzi
kiduchu,ili hali si kweli ni kozi nzuri na ina uwanja mpana wa ajira
na uhuni ni tabia ya mtu binafsi.

Aliongeza changamoto nyingine ni hali ya kipato cha wazazi na walezi

na jamii kwa ujumla kwani imekuwa moja ya changamoto ya chuo kushindwa kufikia malengo yake hasa kutokana na ulipaji mgumu wa ada kwa wanafunzi,kwani “Wakazi wa mkoa wa Tabora wengi wao ni wakulima kwa asilimia kubwa hivyo wengi husubiri kipindi cha msimu kimalipo ama
mvua inaponyesha vyema.”alisema.

Alisema hali hiyo hupelekea chuo kutofikia malengo yake ya kujiendesha

hasa ukizingatia chuo hakina ufadhili wowote zaidi ya kujiendesha
chenyewe.

Alisema chuo pia kinakabiliwa na changamoto ya upungufu wa vifaa na

hasa vinapopatikana huwa ni vya bei ya juu,huku  vifaa vya kozi za
utalii navyo huwa ni tatizo kubwa kupatikana.

Mkurugenzi huyo alitoa wito na ushauri kwa jamii kuendelea kukiamini

chuo cha Musoma Utalii,kwani toka kimeanzishwa kimeweza kutoa wahitimu bora kwa asilimia 90 wamefanikiwa kujiajiri na kuajiriwa kote nchini.

“Tunaomba wazazi na jamii kwa ujumla kuendelea kuleta wanafunzi ili

waweze kupata elimu bora yenye kutambulika kitaifa na kimataifa.”
Aliongeza.

Aidha aliomba pia wazazi kuendelea kuchangia fedha za kwenda mafunzo

ya vitendo ,(Study Tour), kwani chuo kina ratiba ya kutembelea Mbuga
za wanyama mara tatu (3) kila mwaka ikiwa ni sehemu mojawapo ya
kuhamasisha utalii wa ndani kwa Watanzania kwa ujumla.

Alisema ana imani endapo chuo kitakamilika ujenzi wa majengo ya yake

ana imani mkoa wa Tabora ambao ni mkoa wenye historia ya
kiuchumi,kisiasa na kiutamaduni utapiga hatua ya kimaendeleo na kutoa
ajira zaidi.

Mrutu anaongeza kuwa ni dhahiri mkoa wa Tabora una fursa nyingi sana

lakini bado hakuna jitihada za makusudi na hasa elimu kwa vijina wetu
kusoma ili kukabiliana na ushindani wa shirikisho la afrika mashariki
kwa sasa.

Hata hivyo mkurugenzi huyo amesifu kasi mkuu wa mkoa wa Tabora,Fatma
Mwassa katika usimaizi na kutoa vipaumbele ya elimu mkoani hapa kwani dalili za mbadiliko ya elimu zimeanza kutoa picha ya mafanikio mazuri tuendako.

Mrutu anaongeza kuwa mkuu wa mkoa wa Tabora,Fatma Mwassa amekuwa

mstari wa mbele zaidi katika kusukuma gurudumu la elimu kwa kuweka
mikakati madhubuti ya watoto hasa wa masikini waweze pata elimu
itakayosaidia kuondokana na umasikini.

Mkurugenzi huyo anasema kwa sasa chuo cha Musoma Utalii ni kimbilio la

wanyonge kwani kimaonekana ni mkombozi zaidi.

Ushauri.

Mkurugenzi huyo wa kampasi ya Tabora, aliishauri serikali ichukue hatua kadhaa kwa lengo la kuboresha sekta ya utalii katika mikoa ya kanda ya magharibi, hasa katika mkoa wa Tabora kwa kukuza hadhi mapori ya akiba hasa Pori la akiba la Ugalla kuwa Hifadhi ya Taifa ili kusaidia kukua kwa uchumi wa mkoa huo katika sekta ya wanyamapori. Hatua mbayo itasaidia pia iwapo kama vivutio vya utalii katika mkoa huo vitaboreshwa na kutangazwa vya kutosha.

Alisema hilo ni jambo kubwa zaidi ambalo kama likifanyiwa kazi linaweza kuleta mabadiliko makubwa katika sekta ya uchumi ya mkoa huo ambao kwa kweli bado uko nyuma sana na sekta hiyo haijatoa mchango mkubwa katika maendeleo ya mkoa huo.

Aliishauri pia serikali iongeze kasi ya utengenezaji wa barabara za lami zinazoounganisha mkoa huo na mikoa ya jirani ili suala la kufika ama kutoka katika mkoa huo liwe jepesi badala ya hali ya sasa ambapo watu wengi zaidi wamekuwa wakiukimbia mkoa huo katika masuala mbali mbali ikiwemo ya uwekezaji.

Aliiyataka mashirika na kampuni mbali mbali kutosita kuajiri vijana wanaosomea taaluma husika katika vyuo mbali mbali hapa nchini, ili waweze kupata fursa njema ya kuwatumikia watanzania na wageni wanaokuja nchini kwa ajili ya kujionea vivutio mbali mbali  na akimaliza kwa wazazi na walezi kuacha mtazamo potofu unaowafanya waendelee kudhani kwamba masomo ya Utalii na Hotel Management yanamfanya mtu awe muhuni, kwa sababu dhana hiyo haina ukweli wowote.

MWISHO

Sunday, January 20, 2013

SERIKALI KUTUMIA VIJIJI VYA MILENIA MBOLA KAMA MFANO WA KUONDOA UMASIKINI NCHINI

 

Na Lucas Raphael ,Uyui.

Vijiji vya Millenia

SERIKALI imesema inaangalia uwezekano wa kusambaza teknolojia na mbinu
zilizotumika katika kijiji cha millennia Mbola mkoani Tabora, zitumike
katika vijiji vyote hapa nchini, ili kuweza  kuutokomeza umasikini kwa
haraka na kutimiza malengo 8 ya milenia.

Waziri Fedha Dkt William Mgimwa, aliyasema hayo katika kijiji cha
Ilolangulu, wakati akifungua zahanati ya kijiji hicho iliyogharimu
shilingi milioni 49,iliyoko wilaya ya Uyui mkoani Tabora,wakati
akizungumza na wakazi wa vijiji  16 vya millennia Mbola , ambapo
aliwapongeza kwa kazi nzuri na jinsi walivyoupokea mradi huo, ambao
leo ni kielelezo, umekuwa wa mfano.

Alisema kwamba ni vema wananchi wakahakikisha miradi yote
iliyotekelezwa chini ya mradi wa vijiji vya millennia mbola, inatunzwa
vizuri ili iwe daraja la kufundishia vijiji vingine nchini katika
utekelezaji wa malengo 8 ya Milenia .

Waziri Mgimwa, aliyefika kijiji hapo kwa ajili ya kujifunza na
kujionea jinsi mradi huo shirikishi wa kijiji cha Milenia
unavyooendeshwa na Umoja wa mataifa ulivyoweza kupambana na umasikini
kwa wakazi wa vijiji 16 vya wilaya ya Uyui.

Awali Mratibu wa mradi wa kijiji cha Milenia cha Mbola mkoani Tabora,
Dkt Gerson Nyadzi, alisema kuwa wakazi wa kijiji hicho wameweza kupiga
hatua kubwa ya maendeleo baada ya kuwezeshwa na serikali na mradi wa
kijiji hicho kwa kupewa pembejeo ili kuweza kuondokana na umasikini
uliokithiri iliyowawezesha wakulima kulima na kuvuna zaid ya magunia
20 hadi 40 kwa heka moja ya mahindi .

Awali Mwenyekiti wa kijiji cha Ilolangulu Ali Magoha, alisema kuwa
mradi wa kijiji cha millennia unaojumlisha vijiji 16 umefanikiwa kwa
kutimiza malengo yote 8 yaliyokusudiwa kwa kiwango cha zaidi ya
asilimia 85.

Alitaja manufaa ambayo wameweza kupatikana toka mradi wa vijiji vya
milenia Mbalo ulipoanza ni pamoja na  ujenzi wa nyumba za kisasa za
matofari ya kuchoma na bati ,uzalishaji wa mazao ya chakula
umeongezeka .

Pia alisema kwamba mradi huo umesaidia kupunguza tatizo la vifo vya
watoto chini ya miaka 5 na vifo vya akina  mama wajawazito.

Alisema hapa awali vifo hivyo vilikuwa wastani wa watoto 3 nadi
5katika kipindi cha miezi mitatu na kinamama 5 kwa kila mwezi lakini
kwa sasa wastani huo ni kwa kipindi cha miezi 6 na wakati mwingine
hakuna kabisa.

Magoha alisema kwamba hatua hiyo imefikiwa baada ya wananchi kupata
elimu juu ya kutumia vyandarua na kuua mazalia ya mbuhivyo kupunguza
kasi ya maradhi yan malaria katika eneo hilo..

Mwenyekiti huyo wa serikali ya vijiji vya mrai wa vijiji vya Millenia
Mbola akizungumzia swala la elimu alisema kwamba kwa sasa kiwango cha
wanafunzi wanaoacha masomo imepungua tangu mradi huo umeanza na kuwa
sasa wanafunzi wengi wanamaliza masomo ua darasa la saba .

Alitaja mbinu hizo ni pamoja na kutoa chakula kwa wanafunzi na
kuhamasisha michezo mashuleni hivyo wakuwavutia watoto wengi kujiunga
na shule .

Kuhusu suala la maji alisema kwamba wanaendelea vizuri ambapo wastani
wa asilimia 60 ya wakazi wa eneo hilo wanapata maji safi na salama
tofauti na ilivyokuwa awali .

Naye Mbunge wa jimbo la Tabora kaskazini Shaffin Sumar, aliishukuru
serikali kwa kuendelea kuchochea maendeleo katika vijiji vyote 16 vya
millennia kwa kuanza mchakato wa kupeleka umeme katika vijiji hivyo
vyote ili kusaidia kukua kwa maendeleo ya haraka.

Friday, January 18, 2013

BAVICHA YASISITIZA KUMTIMUA SHONZA.




                                                             Juliana Shonza 
Na: Kelvin Matandiko

BARAZA la Vijana la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), limesisitiza kuwa Juliana Shonza amevuliwa nafasi aliyokuwa akiishikilia ya umakamu mwenyekiti wa baraza hilo baada ya kukamilisha taratibu zote za kumuondoa.

Kauli hiyo imekuja kufuatia Shonza kunukuliwa kwenye vyombo vya habari akisema yeye bado ni...
Makamu Mwenyekiti wa Baraza hilo kwa maelezo kuwa hakuwa amepewa barua yoyote ya kumsimamisha.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa BAVICHA, John Heche alisema Shonza alitumiwa barua ya kumvua nafasi hiyo kwa njia ya posta januari 6, hata hivyo amekuwa akikataa kuipokea.

“Lakini sio hivyo tu siku aliyokuwa anazungumza na vyombo vya habari, tulimtumia barua akakataa kuipokea, taratibu zinatuambia kumpatia barua lakini kama ameikataa bado haiwezi kubadili maamuzi ya chama,”alisema Heche.
Baada ya kumtafuta Shonza ili kutoa ufafanuzi juu ya tarifa za kupokea kwa barua hiyo zilishindikana.

Siku mbili zilizopita Shonza alikunukuliwa kwenye vyombo vya habari akisema kikao cha kamati ya utendaji cha Bavicha kilichokutana na kupitisha umamuzi wa kumfukuza kilikuwa sio halali huku akiwatupia lawama Heche na Mwenyekiti wa Chama hicho Freemon Mbowe kwa madai ya kumdhalilisha.

Shonza alisema yeye bado ni Makamu Mwenyekiti wa Bavicha na mwanachama halali wa chama hicho. Aidha alisema anafanya mkakati wa kuwashtaki wale anaowalalamikia kwa kumuita msaliti ndani ya chama hicho.

Shonza alimtuhumu Heche kutengeneza mipango ya kutukuza ukanda waziwazi ndani ya chama hicho huku akiwataka kutoa ufafanuzi wa kikatiba juu ya shutuma zinazotolewa dhidi yake.
 MWANANCHI