Saturday, February 23, 2013

MANENO OSWARD ATAMBA KUMCHAKAZA KASEBA MARCH 2

 

Bondia Maneno Osward akijifua kwa ajili ya mpambano wake wa ubingwa dhidi ya Japhert Kaseba March 2 katika ukumbi wa DDC Madomeni Kondoa Dar es salaam
Bondia Maneno Osward 'Mtambo wa Gongo' akifanya mazoezi ya kukaza misuli ya tumbo kwa ajili ya mpambano wake wa ubingwa dhidi ya Japhert Kaseba March 2 katika ukumbi wa DDC Madomeni Kondoa Dar es salaam
Mabondia Maneno Osward kushoto na Japhert Kaseba walipokutana kwa ajili ya kuzungumzia mpambano wao utakaofanyika March 2 katika ukumbi wa DDC Magomeni Kondoa Dar es salaam picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Na Mwandishi Wetu

BONDIA Maneno Osward ametamba kumchakaza mpinzani wake Japhert Kaseba kunako raundi za awali akizungumza na mwandishi wa habari hizi maneno maarufu kwa jina la Mtambo wa Gongo amesema yeye yupo fiti na anasubili hiyo March 2 katika ukumbi wa DDC Magomeni kondoa apate kumshikisha adabu 

Kaseba ni bondia mchanga sana kwangu nilimkaribisha katika masumbwi na sasa nitamstafisha masumbwi mimi mwenyewe kwa kipigo nitakacho mpa na atajua kwa nini nimepewa jina la mtambo wa Gongo

Katika mpambano huo kutakuwa na mpambano wa uzito wa juu kati ya Josefu Marwa na Alphonce Mchumiatumbo mpambano unaosubiliwa kwa hamu na mashabiki na wapenzi wa ngumi za uzito wa juu nchini 

Mbali na kuwepo mapambano ya ngumi kutakuwa na uuzwaji wa DVD zenye mapambano ya mabingwa wa Dunia akiwemo Manny Paquaio, Floyd Maywherth, Roy Jones,Miguel Cotto,Linox Lewis na wengine wengi DVD hizo zilizoandaliwa kwa ubora wa hali ya juu zitakuwa zikiuzwa kwenye mpambano huo na Kocha wa Kimataifa wa mchezo huo. Rajabu Mhamila ‘Super D’, alisema kuwa kutakuwa na DVD ili kuweza kuwauzia mashabiki kwa ajili ya kujifunza Kanuni na Sheria za mchezo huo.
“Ninatarajia kuwepo kwa ajili ya kuwauzia DVD mashabiki wa ngumi watakaokuwepo katika Mpambano  ili kuweza kujifunza mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na sheria za mchezo wa ngumi”, alisema Super D
.

MONTAGE CHARITY BALL YAENDELEA KUFANYA VIZURI USIKU HUU NDANI YA HOTELI YA SERENA

 

 Mkurugenzi Wa Kampuni ya Montage Bi Teddy Mapunda akifungua tafrija ya Kuchangisha Pesa kwaajili ya Wanawake wenye matatizo kwa Kumkaribisha Mgeni Rasmi ambaye pia Ni Mwenyekiti wa WAMA na Mke wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Salma Kikwete katika hafla inayofanyika Usiku huu katika Hoteli ya Serena
 Mwenyekiti wa WAMA na Mke Wa Raisi Wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Salma Kikwete akitoa neno wakati alipokaribishwa kusema chochote kama mgeni rasmi katika hafla ya kuchangisha pesa kwaajili ya wanawake Tanzania iliyoandaliwa na kampuni ya Montage Limited inayofanyika Usiku Huu katika Hoteli ya Serena
 Baadhi ya Wahudhuriaji wa Hafla hiyo
Msanii Kutoka Nchini Tanzania Barnaba akitumbuiza katika hafla ya kuchangisha pesa kwaajili ya wanawake Tanzania hafla inayoendelea kufanyika katika Hoteli ya Serena Usiku Huu

MAJANGILI MATATU YAUAWA MKOANI DODOMA LEO

 

Wameuawa kisha kuchinjwa na kuchomwa moto ndivyo miili ya marehemu wanaodhaniwa kuwa ni majangiri wa wanyama poli inavyoonekana ilipofikishwa kuhifadhiwa katika hospital ya Mvumi Dodoma.
Mwili wa Mtu anayedhani wa kuwa ni Jangili ukiwa umehalibika baada ya kuuawa kuchinjwa na kuchomwa moto katika chumba cha kuhifadhia maiti mvumi Dodoma.
Kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma David Misime akiwaonyesha waandishi wa Habari meno 73 ya tembo yenye thamani ya zaidi 225 mil ambayo ni sawa na tembo 36 pamoja na Gari aina ya Noah NO T 983 BZJ waliokamata juzi katika kijiji cha Miganga mvimi wilayani Chamwino Dodoma.
Kamanda wa polisi Mkoa wa Dodoma David Misime akifafanua jambo mbele ya waandishi wa Habri kuhusu tukio la vifo vya watu watatu wanaodhaniwa kuwa ni majangili waliouawa na wananchi katika kiji cha miganga Mvumi Dodoma pembeni ni Gari aina ya Noah No T 983 BZJ walilokuwa wakilitumia na kuku meno 73 ya Tembo.
Na John Banda, Dodoma

MAJANGILI watatu wa nyara za serekali wameuawa kwa mishale yenye sumu na kisha miili yao kuchomwa moto na wananchi katika purukushani na polisi walipokuwa wakijaribu kukimbia ili kutorosha meno  ya tembo.

Tukio hilo lilitokea jioni ya alhamis wiki hii katika kijiji cha Miganga kata ya mvumi wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma ambapo miili yao ilikutwa ikiwa imehalibika kutokana na kuchomwa moto.

Akizungumzia tukio hilo Kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma David Misime alisema majangili hayo yaliuawa na wanachi wenye hasira kali kwa zana mbalimbali za kijadi walipokuwa wanakimbilia polini ili kujiokoa na mkono wa polisi.

Misime alisema jeshi hilo lipokea taarifa kutoka kwa wananchi wema kuwa kulikuwa na Gali likitokea Manda likiwa na Meno ya Tembo  na kisha kuweka mtego katika kijiji cha mwitikila ambapo waliona gali aina ya NOAH T 983 BZJ na kulisimamisha na Dereva wa Gali hilo alifanya kama anapunguza mwendo na kisha kuondoka kwa mwendo wa kasi.

‘’Polisi wakishirikiana na wananchi walianza kulifukuza  walipofika kijiji cha Miganga Mvumi polisi walifanikiwa kupiga Risasi tairi moja ya kushoto na hivyo watu watatu waliokuwemo ndani gari hilo waliruka na kutawanyika, wananchi waliojichukulia sheria mkononi waliwashambulia kuasi cha kupoteza maisha yao’’, alisema
 
Aidha kamanda Misime alisema baada ya kulipekua Gari hilo walikutaMeno 73 ya Tembo yenye uzito wa kilo 255.9 yakiwa na thamani ya zaidi ya TSH 225 mil pamoja na hati ya mashitaka [CHARGE SHEET] ambayo ni kesi ya kuhujumu uchumi namba 4/2012 iliyokuwa imefunguliwa katika mahama yam panda mkoa wa katavi na Leseni ya Udereva na 4000692535 Aboubakar Peter huku wakihisi ni mmoja ya waliouawa.

Alisema walikuwa wameshitakiwa kwa kosa la kupatikana na Meno 3 ya Tembo Tarehe 17.06.2012 na maafisa wanyama poli  katika eneo la Msaginya Wilaya ya Mlele mkoa wa katavi majina ya walikuwa wameshatakiwa ni Joseph Marius [NGONDO] 59 mkazi wa maili mbili Dodoma, Aboubakar Mhina 25 mkazi wa Mkuhungu Dodoma, Msafiri Milawa 36 mkazi wa Nkuhungu Dodoma na Petro Mtipula 55 mkazi wa mpanda.

Kamanda alitoa wito kwa wananchi wasijichukulie Sheria mikononi kwani kwa kufanya hivyo ni kupoteza ushahidi na inawawia vigumu polisi kupata mtandao inayohusika na matukio kama hayo.PICHA NA JOHN BANDA WA PAMOJAPURE BLOG

Kongamano la Nane la Wanahabari na Wadau wa NHIF


Wednesday, February 20, 2013

MTOTO AHISIWA KUFA MAJI KWENYE MFEREJI WA MAJI MACHAFU KATA YA ISEVYA TABORA MJINI.

 Baadhi ya askari wa kikosi cha zimamoto mjini Tabora wakiwa katika harakati za kumtafuta mtoto aliyezama katika mfereji wa maji machafu kata ya Isevya manispaa ya Tabora,imeelezwa kuwa mtoto huyo alizama kwenye maji yaliyosababishwa na mvua kubwa iliyonyesha leo asubuhi,hadi sasa zoezi la kumtafuta mtoto huyo bado linaendelea ingawa hakuna mzazi aliyejitokeza kuwa amepotelewa na mtoto wake. 

MWANAFUNZI AJINYONGA KWA MATOKEO MABAYA YA KIDATO CHA NNE MWAKA HUU



 Na Lucas Raphael,Tabora


Siku chache baada ya matokeo ya kidato cha nne kutangazwa nchini  mkoani tabora mwananfunzi  aliyemaliza kidato cha nne katika shule ya Sekondari ya Kanyenye mjini Tabora, amejinyonga kufuatia matokeo mabaya ya kidato cha nne mwaka huu.

akizungumza na waandishi wahabari ofisini kwake kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora  ACP Anthony Rutta amemtaja mwanafuzi huyo kuwa ni Michael Fidelis (19) ambaye ni mkazi wa skanda mtaa Mwinyi kata ya chemchem Manispaa ya Tabora.

Alisema mwanafuzi huyo alienda kuangalia matiokeo ya kidato cha nne majira ya saaa 11 jioni Februari 18 mwaka huu na badaye kukutwa amejinyonga hadi kufa chumbani kwake kwa kutumia kamba ya manila.

Kamanda Rutta alieleza kuwa marehemu alipata darajala mwisho kwa maana ya sifuri aliacha ujumbe uliosomeka “Nisamehe sana mama usitafute mchawi, nakupenda sana, uwamuzi niliochukua nisababu ya matokeo mabaya, nakutakia maisha mema” ulisema sehemu ya ujumbe huo.

Mkuu wa shule ya sekondari ya kenyenye alipokuwa akisoma mwanafunzi Fidelis, Kapufi Patson alisema kuwa mwanafunzi huyo alikuwa ni mpole na mtaratibu na wameshangazwa na uwamuzi aliochukua wa kujinyonga.

Matokeo ya shule ya sekondari ya mwinyi yanaonyesha hakuna mwanafuzi aliyepata alama ya ya kwanza na  yapili huku waliopata darajala tatu wakiwa wanafuzi wawili, daraja la nne 14 na waliopata sifuri ni wakiwa wanafunzi 85, wakati wanafuzi 36 matokeo yao hayaktoka kwasababu walikuwa wanadaiwa ada ya mtihani.

 Mwisho

Sunday, February 17, 2013

WAISLAM NA WAKRISTO WAUNGANE;LOWASSA

 
Na,LUCAS RAPHAEL,,Nzega.
 
WAZIRI Mkuu Mstaafu  Edward Lowassa  amewataka waislam na wakristo wote Nchini kuungana kwa pamoja  kuitetea na kuilinda amani tuliyonayo kwa vitendo.
Akizungumza katika Harambee ya kanisa la Moraviani  kanda ya magharibi iliyofanyika katika wilaya ya nzega mkoani Tabora,kuwa waumini hao kwa pamoja wanapaswa kuungana na kuwa kitu kimoja katika kuitetea amani iliyopo kwa vitendo.
Lowassa aliendelea kusisitiza kwamba kwa sasa kuna baadhi ya watanzania wanaichezea amani iliyopo kwa sasa hapa nchini na kufanya mauaji ya watumishi wa mungu lakini isiyo Tanzania tunayoihitaji .
Hata hivyo alikuwa na kimwabingizo cha hii ni Tanzania tunayoihitaji ili kuwa na upendo na utulivu amani tunayoisema tutailinda amani kwa nguvu zote hapa Tanzania.
“hii ni Tanzania tunayoitaka kwa waislamu na wakristu kushirikiana katika ibada kama hii leo hapa kanisani “alisema Lowassa.
Alisema kwamba katika maisha yetu ya kila siku ni watu wakutengemeana kwa kila jambo kwani hakuna muda saa ambao uwezi kuacha kumuona muislam akipita njiani na hata mkristo pia katika mitaa nayo ni hivyo hivyo .
Lowassa aliendelea kusisitiza watanzania tunapaswa kuhakikisha kila siku tunamuomba mungu ili kuendeleza amani yetu hapa Tanzania inadumishwa kwa hali na mali.
Hata hivyo katika changizo hilo la harambee ya kanisa la morviani kanda ya magharibi alisema kwamba yeye ni tajiri wa watu nasio tajiri kama watu wanavyosema huko mitaani .
Alisema kwamba watu wanaomsema vibaya kila kukicha waendelea kufanya hivyo kwani kwafanya hivyo wanaendela kumuimarisha kiimani na nguvu kubwa ya ushawishi kwa watu wa mungu amboa ndio wamekuwa wakimuunga mkono kila siku katika kazi ya mungu.
“mimi nitajiri wa watu nasio tajiri wa fedha kama wanavyo sema huko mitaani  na watu wasiokuwa na mapenzi mema na mungu”alisema lowassa
Aidha katika harambee walikuwapo waislamu kutoka mikoa ya mwanza ,shinyanga na Tabora pamoja na viongozi mbalimbali wa siasa kutoka sehemu mbalimbli hapa  nchini.
Askofu Mkuu wa kanisa la moraviani kanda ya magharibi Issack  Nicodemo alisema kuwa waislam na wakristo hapa nchi ni ndugu kutokana na mahusiano yaliyopo toka hapo awali.
Alisema kuwa vitendo vinavyoendelea kufanyika hapa nchini vya mauaji kwa viongozi wa dini ni vyakulaniwa na kongeza kuwa upendo na amani inahitajika kupoteza suala hilo.
Wakati huo huo mbunge wa jimbo la kaliua Profesa Juma kapuya alisema kuwa kunabaadhi ya watu wamelewa na amani iliyopo nchini hivyo amani inapaswa iheshimiwe.
Naye mwenyekiti wa chama cha mapinduzi ccm mkoa wa shinyanga Hamis Mgeja aliwataka waislamu na wakristo kuliombea taifa hili ilikuweza kuwa na amani na upendo.
Awali Akisoma risala mbele ya Mgeni rasmi makamu mwenyekiti wa idara ya wanawake wa kanisa la Morania Agness Nsanto katika harambee hiyo ikiongozwa na waziri mstaafu Edward Lowassa ilifanikiwa kukusanya fedha million 110,168,250,fedha tathilimu zilikuwa Million 36,706,250 wakati ahadi zikiwa Million 71.
Hitaji harisi ilikuwa Millioni 80 ambapo wanawake hao walikuwa na Million 20 kama kianzio cha kukusanya fedha hizo.
Mwisho.
 
 

AUAWA KWA KUIBA MAHINDI MATATU -KILOLENI TABORA


 Baadhi ya wakazi wa kata ya Kiloleni manispaa ya Tabora wakishuhudia mwili wa mtu mmoja aliyekutwa amekufa baada ya kujeruhiwa vibaya kwa silaha zenye ncha kali na kusababisha kifo chake huko eneo la Ikindwa ambapo imedaiwa kuwa alikuwa akiiba mahindi katika moja ya shamba la mahindi.
 Mmoja kati ya askari Polisi mpelelezi wilaya ya Tabora PC Setty  akijaribu kupekua mwili wa mtu huyo ambaye imedaiwa kuwa alikuwa ameiba mahindi matatu.

BUNGE LA KIKOMONIST LAZINDULIWA HUKO DODOMA

 

 

2-wakipinga  3a972
Bunge la Kikomunist Lazinduliwa
Huko Dodoma
Ni habari za kusikitisha na kuhuzunisha kuona kwamba taratibu za ukomunist ambao ulipigwa marufuku kote duniani mwaka 1991 leo hii bunge letu limezindua mikakati ya kuliendesha bunge kwa kutumia taratibu za kikomunist! 

Baadhi ya makala zangu za nyuma nimewahi kuelezea kwamba moja ya silaha zinazotumiwa sana na wakomunist ni kutengeneza mazingira ya usiri kati ya watawala na watawaliwa, kwa vile watawal;a siku zote hawapo sahihi na wala hawajiamini mbele ya watawaliwa ambao ndiyo wananchi waliowaweka madarakani.
 
Wakomunist wanapangiwa waseme nini!? Waende wapi na wapi wasiende!? Wavae nini na nini wasivae!? Wale nini na nini wasile!? Wafikiri juu ya nini nakadhalika!

Siamini kwamba katibu wa bunge Dr. Thomas Kashililah alitafakari kabla hajaozungumzia hoja yake ya kutaka vikao vya bunge visirushwe moja kwa moja, nasema hivyo kwa vile sababu alizozitoa si sababu za kimsingi wala hazileti fikirishi kwa mtu yeyote anayejua maana bunge ni nini, na nani mwenye mamlaka na bunge!? 

Bunge ni mali ya umma, na umma ndiyo unalichagua bunge na kama umma ndiyo unalichagua bunge sioni sababu ya kuwafungia wabunge wasionekane au wasisikike wanachokiongea kwa kisingizio cha kukiuka maadili na kanuni za bunge!

Tena ni vizuri wabunge wanapopigana wananchi waone ili wajue kinachowapiganisha ni kitu gani? Kinachowapiganisha kinalenga maslahi ya umma au binafsi; wananchi wanataka kuona ni mbunge gani yupo tayari kupigana na hata kung’olewa meno kwa ajili yao! Hivyo npyo tunavyowapima wabunge wale wanaojitoa muhanga kwa ajili yetu, na pia kuwaona wale wanafiki wakisimama majukwaani wanatoa ahadi za uongo kwamba watasimamia haki lakini wakiingia bungeni ni waoga hata kunyosha kidole wanaogopa!

Wabunge kupigana bungeni ni jambo la kawaida kwa mabunge mengi duniani, tumewahi kushuhudia wabunge wa Uingereza, Urusi, Ukraine, Marekani, Brazili na kwingineko wabunge wakishindana kuhusu hoja na kuishia kurushiana matusi na mwishowe kupigana, hivyo na sisi tusione kitu cha ajabu wabunge kupigana, kwa vile kupigana kwa wabunge ni ishara ya kukua kwa democrasia. 

Ukikuta bungeni hakuna mizozo wala mivutano ya hoja, basi jua kwamba hakuna democrasia na bunge hilo ni bunge la mwelekeo mmoja.

Sababu alizotoa katibu wa bunge Dr. Thomas Kashililah za kwamba wabunge wanawake wanapojua kwamba watatoa hoja, huwa wanakuja wamevaa vizuri na kujipodoa akiitumia sababu hii kama kigezo cha kutorusha matangazo moja kwa moja; mimi naoni hii ni sababu isiyokuwa na msingi kwa vile mwanamke hata akienda gengeni kununua nyanya ni lazima ajipodoe! Sasa unataka akiingia bungeni awe amevaa ovyo ovyo wakati anaenda kusikilizwa na waajiri wake ambao ni wananchi! 

Wakimuona amevaa ovyo ovyo na hakujipodoa si wananchi
watamnyima kura uchaguzi ujao!?

Dr. Thomas Kashililah anaposema baadhi ya wabunge wanapochangia hoja huwa
wanazungumza mpaka mishipa inatoka, hivyo anataka kuitumia hoja hii kama sababu ya vikao vya bunge kutorushwa moja kwa moja; pia hii si sababu ya msingi ambayo inaweza kutolewa na katibu wa bunge; bungeni ndipo sehemu pekee ya kuonyesha umahiri wa kuongea kwa vile bungeni ni jukwaa pekee linalotambuliwa kikatiba katika kutetea maslahi ya umma; na kama mbunge atalitumia jukwaa hili kwa manufaa yake wewe muache tu kwa vile sisi wananchi tupo macho tunamuangali moja kwa moja kupitia runinga zetu. 

Akizidisha umimi 2015
tutampumzisha!
Dr. Thomas Kashililah anaposema waandishi wa habari wanampiga picha spika akiwa ameinama au amelala bungeni, na akitaka kukitumia kigezo hichoi kama kuunyima umma wa watanzania kutoshuhudia bunge lao ambalo wameliajiri na kuliruhusu kutumia kodi zao, pia ni sababu ambayo haina msingi na kulingana wadhifa aliokuwa nao katibu wa bunge hakustahili kutetea sababu kama hiyo, kwa vile bungeni ni jukwaa la kujadili matatizo ya wananchi na wala siyo sehemu ya kulala au kupumzika; 

kama spika analalalala bungeni inaonyesha hatekelezi wajibu wake kikamilifu na kama ndiyo hivyo ni kwanini bunge lisimuwajibishe!?

Bwana Kasililah anataka aturejeshe nyuma kwenye zile enzi za giza la kikomunist ambapo wabunge walikuwa wanajifungia na kuongea mambo waliyotaka na baada kuyachambua yale tuliyostahili kuyasikia na kutangaziwa kwa njia ya redio, na yale tusiyostahili walibaki nayo wenyewe! Bunge la kikomunist hupangiwa uvae nguo gani!? uulize swali gani!? utoe jibu gani!? mwandishi wa habari apige picha gani au akaandike kwenye gazeti kitu gani!? 

Huu ndiyo utaratibu wa mabunge ya kikomunist yalivyokuwa enzi hizo, sasa wewe na uelewa wako unataka uwarudishe watu kizani kwa maslahi yako binafsi, hatutakubali kwa hilo hata siku moja. 

Wewe waache wabunge wafanye wafanyavyo sisi ndiyo waajiri wao ukifika muda wa kusitisha ajira zao tutafanya hivyo mara moja, wewe tunachokuomba ukiona spika amelala na huku bunge linaendelea mwamshe ili azinduke usingizini asije akaidhinisha sheria za maangamizi!

Dr. Noordin Jella (Ph.D. in Economics)
Former Lecturer of Mzumbe, Open & KIU – Dar, Universities.
Currently: Freelance Journalist & Seasonal Political
Analyst
Email: norjella@yahoo.com
Mobile: +255 782 000 131

Sunday, February 10, 2013

HATUJAWAHI KUKAA KIKAO CHA KISHERIA KUPENDEKEZA KUWASIMAMISHA AMA KUFUKUZWA KAZI WATUMISHI



NA LUCAS RAPHAEL,TABORA


BARAZA la madiwani wa halmashauri ya manispaa ya Tabora,limemjia juu mkurugenzi wa manispaa hiyo Sipola Liana, kwa madai kuwa hawakuwahi kukaa kikao chochote na kupendekeza kusimamishwa ama kufukuzwa kazi, kwa watumishi watano wa manispaa hiyo kwani taratibu zimekiukwa.

Kauli hiyo ya pamoja ilitolewa leo kwenye kikao cha baraza la madiwani wa manispaa hiyo.

Wakichangia kwa nyakati tofauti,madiwani hao walisema mapema mwezi agosti 27,mwaka 2012,waliletewa taarifa kuwa watumishi watano wa manispaa hiyo wamesimamishwa kazi kwa muda usiojulikana kupisha uchunguzi wa tuhuma mbalimbali zinazowakabili.

Aidha waliongeza kuwa kwenye kikao cha baraza hilo,walijulishwa na ofisi ya mkurugenzi kuwa kuna tume itaundwa na mkuu wa mkoa wa Tabora,Fatma Mwassa,kuchunguza ukweli wa tuhuma zinazowakabili huku barua za kusimamishwa kwao zikisomeka kuwa 

“wamesimamishwa kazi kwa kutokutimiza majukumu yao”.
Waliongeza kuwa toka wamesimamishwa kazi hadi sasa muda wa kisheria ulishapita kuundwa tume na zaidi hakuna taarifa yoyote iliyotolewa na ofisi ya mkurugenzi juu ya hatua iliyofikia ya kuundwa tume hiyo.

Aidha waliongeza kuwa wao kama madiwani wameona mbele yao kuna hatari ya halmashauri kufikishwa mahakamani  kwani wanaotuhumiwa na kusimamishwa kazi hawakuwahi kupewa hati za mashitaka,kabla ya kusimamishwa na hadi leo hakuna cha tume wala nini.

Walisema kusimaishwa kazi kwa watumishi hao,mchumi wa manispaa Charles Mduma,afisa ardhi mteule Charles Mkalipa,kaimu afisa utumishi Joyce Masoga,mweka hazina Grace Manwinkwi na mhandisi wa manispaa Siraji Mbuta taratibu za utumishi kuwasimamisha hazikufuatwa.

“Tunachoona hapa vitu vinaamuliwa tu bila ya madiwani kukaa kwenye vikao halali vya kisheria kwani hatujawahi kupeleka mapendekezo yoyote TAMISEMI, juu ya kile kinachodai ni tuhuma za watumishi hao tumeletewa taarifa tu kuwa wamepewa barua za kusimamishwa……hatujawahi kukaa kikao chochote kuwasimamisha kazi tunakana kwa kauli moja.” Walisema.

Waliongeza kuwa mapema mwezi novemba 7,mwaka 2012 walisikia kuwa mkurugenzi wa manispaa Tabora Sipola Liana,amewaandikia barua watumishi waliosimamishwa kazi ikisema “wanapumnzishwa kazi kwa muda kupisha uchunguzi” hali ambayo wao kama madiwani hawakukaa kikao chochote kujadili na kupendekeza.

“Barua zote mbili ziliandikwa na mkurugenzi bila sisi kukaa vikao kuamua hayo yaliyoandikwa sasa leo hakuna kinachoendelea hakuna taarifa ya tume iliyoundwa wala hakuna majibu yoyote ya kusimamishwa kazi kwa hawa watumishi hii maana yake nini na tayari kuna kila dalili za halmashauri kufikishwa mahakamani kwani taratibu za utumishi zilikiukwa” walisema.

Walisema ikibidi kuwatetea ili kuinusuru manispaa hiyo kwani vitu vinaamuliwa kienyeji tu halafu hakuna mrejesho wowote hadi sasa hizo barua ziliandikwa kwa idhini ya vikao gani na kwamba afisa ardhi mteule,Charles Mkalipa, yeye ndiye anayesaaini baadhi ya faili sasa maamuzi yake yamesimama nani anafanya kazi hiyo.

Akijibu hoja za madiwani hao mkurugenzi wa halmashauri hiyo,Sipola Liana alisema yeye baada ya kufika kwenye kituo cha Tabora,alikuta barua ya kusimaishwa kazi kwa watumishi hao, na aliona kuna makosa makubwa yaliyopo na hivyo aliamua kuandika barua upya za kuwapumzisha kazi kwa muda badala ya ile ya mwanzo ya kuwasimamisha kazi.

Kuhusu uchunguzi alisema tayari ulishaanza na hati za mashitaka walishapewa na wamejibu  utetezi wao na hivyo ofisi yake imeshamwandikia katibu tawala(RAS),Kudra Mwinyimvua ili tume hiyo iletwe na inaweza toka mkoani ama TAMISEMI.

Mwisho-