Monday, May 13, 2013

WAANDISHI WA HABARI WAPO HATARINI - TUNDU LISSU


lisu1 fda6e
Mh Tundulisu akitoa Vyeti kwa wana chaso katika Haflahio,

WAANDISHI wa habari wapo katika hatari kubwa ya kutoweka nchini kutokana na kuandika maovu yanayofanywa na viongozi wa serikali.
Haya yamezungumzwa na Mbunge wa Singida Mashariki na mnadhimu Mkuu wa kambi ya upinzani Tundu Lissu katika mahafali ya shirikisho la wanafunzi wa vyuo vikuu Mkoa wa Iringa (CHASO) katika ukumbi wa Chuo Kikuu Huria kilichopo katika Manispaa ya Iringa.
Lissu alisema waandishi wa habari wapo katika hatari ya kutoweka hasa kwa kuuawa kutokana na ukweli wao wanaouandika hasa kuyaweka madudu ya baadhi ya viongozi wa serikali.
Alisema hasa katika ripoti ya uchunguzi ya mauaji ya mwandishi wa habari Daudi Mwangosi ya tume iliyoundwa na vilabu vya waandishi wa habari Tanzania (UTPC) inaonesha wazi juu ya hatari walionayo waandishi wa habari.

Alitaja chanzo cha kuwamaliza waandishi hao kuwa ni polisi wanaotumiwa na viongozi hao kama njia ya kuzuia kuendelea kuandika madudu yao.
Hata hivyo alisema waajiri wa waandishi ni chanzo moja wapo cha kinachochangia waandishi kuwa katika hatari hiyo kwa kuwatengenezea mazingira mabovu ya utendaji wao hasa wawapo kazini.
Lissu alisema waandishi wa habari ambao wapo katika hatari kubwa ni wa Iringa ambao tayari wapo katika listi ya kupotezwa kwa namna yoyote kwa kile kilichoelezwa kuwa hawaandiki habari zao kwa unafiki.
"Tuwalinde sana waandishi wa habari kwa kweli wapo katika hatali kubwa sana. Kila mmoja awe mlinzi wa waandishi hawa na ifike mahali tukasema hatutaki Mwangosi mwingine. Hasa waandishi hawa wa Iringa wapo katika wakati mgumu sana" alisema.
Pia aliwaasa wanafunzi waliomaliza kwenda kuungana na wananchi kuendeleza harakati za Mageuzi kuanzia katika Mashina,kata, na Majimbo ili kufanikisha mpango wa kuelekea ikulu vinginevyo ni ndoto hapondipo utatokea ukombozi wa Waalimu, Madaktari, na Wanasheria
Wasio na kazi kwasababu ya Mipango mibovu ya utawala uliopo kupata furusa ya kuitumikia nchihii kukiandaliwa mipango mizuri ya ajira,
Historia inaonyesha hakuna Mzee aliefanikisha mapinduzi ya kisiasa katika nchiyake kama hakuanza wakati akiwa kijana na kuelekea katika Mafanikio ndipo uzee unamkuta akiwemo ndani ya Harakati,

WAFANYAKAZI WA MRADI WA MILENIA MBOLA WAFANYA SHEREHE


 Kiongozi wa mradi wa vijiji vya Milenia Mbola Dr.Gerson Nyadzi akizungumza katika hafla fupi ya jioni ya wafanyakazi wa Mbola Mvp ilyofanyika katika ukumbi wa Polisi mjini Tabora.
 Hapa ni wakati ulipowadia kwa wafanyakazi hao kulisakata Rumba kwa kila mmoja kwa Staili yake na akionesha ufundi juu ya hilo.
 Ilikuwa vigumu kuvumilia kwa Kiongozi wa Mradi Dr.Gerson Nyadzi kuwaachia Staff peke yao kunyoosha viungo vyao akaamua kuwasindikiza kwa kucheza Kiduku kama inavyoonekana hapa ambapo ukumbi ukachangamka.
 Ikafikia hatua hata ya viatu kuwa vizito na uchangamfu ukakolea bila kujali muda wa kukamilisha hafla hiyo ya jioni.
 Wakati wa maakuli ulipewa kipaumbele cha kwanza kabla ya mambo mengine ili kusawazisha mambo.


"DR.KAFUMU NI MBUNGE HALALI WA JIMBO LA IGUNGA"-MAHAKAMA YA RUFAA


Dr.Dalali Peter Kafumu mbunge halali wa jimbo la Igunga - Mahakama ya Rufaa kanda ya Tabora.
Aliyekuwa mgombea wa nafasi ya Ubunge kwa tiketi ya Chadema  Mwalimu Joseph Kashindye mstari wa pili kutoka kulia ni mtu wa pili aliyevaa sare ya Chadema akizungumza jambo na mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Tabora muda mfupi kabla ya kutolewa kwa maamuzi ya Mahakama ya Rufaa dhidi ya kesi ya kutenguliwa Ubunge Dr.Dalali Kafumu.


Baadhi ya viongozi wa Chadema na CCM ngazi za wilaya wakiwa mahakamani kushuhudia kesi ya rufaa ya kutenguliwa kwa matokeo ya Ubunge wa Jimbo la Igunga Dr.Kafumu

Thursday, May 9, 2013

MAHAKAMA YA RUFAA YATENGUA MAAMUZI YAMREJESHEA DKT KAFUMU CCM UBUMGE‏


 

Na Lucas Raphael,Tabora

 
Mahakama ya rufaa nchini imetengua maamuzi ya mahakama kuu na kumrudishia ubunge wake Dkt Peter Dalali Kafumu – CCM wa jimbo la Igunga baada ya kuridhika ha hoja za upande wa mrufani kuwa jaji aliyesikiliza shauri hilo hakuzingatia matakwa ya kisheria.

Akisoma  uamunzi huo mwenyekiti wa jopo la majaji wa mahakama hiyo jaji Nathalia Kimaro akisaidiana na jaji William Mandia na jaji Semistrocles Kaijage amesema kuwa mlalamikiwa hakulipa ada ya mahakama kama sheria ya uchaguzi inavyoelekeza.

Aliongeza kuwa awali wakati shauri hilo namba  10/2011 linafunguliwa mahakama kuu jaji aliyelisikiliza hakusikiliza pingamizi la mrufani kwamba hakukuwa na ada iliyolipwa hivyo hakupaswa kuendelea na usikilzwaji wake.

“ kutolipwa ada ama kutokuwepo kwa kumbukumbu yoyote katika jalada la mahakama inayoonyesha kitu kiwekwa kama kinga ilikuwa ni sababu tosha ya kutosikiliza shauri hilo” walisema majaji hao katika maamuzi yao.

Katika hoja zake wakili  wa serikali Gabriel Malata  za kutaka yatenguliwe maamuzi ya mahakama kuu aliwaambia  majaji wa mahakama ya rufaa kuwa jaji aliyesikiliza kesi hiyo alikosea kuanza kuisikiliza kwani mlalamikaji hakutimiza matakwa ya kisheria.

Malata alidai kuwa mlalamikaji hakulipa ada ya mahakama kiasi cha shilingi milioni moja alizotakiwa kutoa au hati ya nyumba kabla kesi hiyo haijaanza kusikilizwa kama sheria ya uchaguzi kifungu na 111 inavyoelekeza.

Wakili Malata aliongeza kuwa kwa vile mjibu Rufaa Joseph Kashindye  na wenzake hakutekeleza sharti hilo  usikilizwaji wa shauri hilo pamoja na mwenendo mzima yakiwemo maamuzi vyote vilikuwa ni batili.

Aliongeza kuwa malalamiko yaliyopelekwa mahakama  ni ya kutengeneza kwani hayajawahi kuwasilishwa katika kamati ya maadili ya uchaguzi kama walivyofanya juu ya suala la mbunge wa Tabora mjini Ismali Aden Rage  ambaye alitozwa faini ya shilingi laki moja kwa kutembea na
silaha kwenye mkutano.

Hoja hizo na nyingine zilipingwa na wakili wa mjibu rufaa profesa Abdalah Safari ambaye aliitaka mahakama ya rufaa kuzitupilia mbali na kwamba Mahakama iliyosikiliza kesi hiyo iliridhika kuwa kulikuwa na ukiukwaji wa sheria wakati wa zoezi zima la uchaguzi wa jimbo la Igunga ndipo katengua matokea.

Kukatwa rufaa hiyo kunafuatia maamuzi ya Mahakama Kuu ya Tanzania iliyotengua matokeo ya uchaguzi mdogo wa jimbo la Igunga mkoani hapa baada ya kubainika kuwa uchaguzi huo ulitawaliwa na vitendo vya rushwa, kampeni chafu na vitisho dhidi ya wapiga kura.

Jaji Mary Nsimbo Shangali wa mahakama kuu Agasti 21 mwaka jana alitangaza kutengua matokeo hayo baada ya mahakama hiyo kuridhika na hoja saba  zilizowasilishwa na upande wa mlalamikaji  kati ya hoja  19 zilizowasilishwa katika mahakama hiyo.

Kesi hiyo ilifunguliwa na Mlalamikaji aliyekuwa mgombea wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)  Joseph kashindye, ambaye aliwakilishwa na wakili Maarufu nchini Profesa Abdallah Safari  ambapo alipinga matokeo ya uchaguzi huo akilalamikia kukiukwa kwa sheria ya uchaguzi mkuu.

Upande wa Utetezi  uliwakilishwa na  mawakili Mohamed Salum Malik na Gabriel Malata kutoka ofisi ya Mwanasheria mkuu wa serikali,Msimamizi wa Uchaguzi jimbo la Igunga,  na mawakili Antony Kanyama na Kamaliza Kayaga waliokuwa wakimtetea mbunge wa Igunga Dkt Peter Dalali Kafumu.

Akisoma hukumu jaji Shangali alizitaja baadhi ya kasoro zilizopelekea kutengeliwa kwa uchaguzi huo ni pamoja na  Ahadi  iliyotolewa na Waziri wa Ujenzi  Dk. John Pombe Magufuli, kuhusu  ujenzi wa daraja la Mbutu ambalo alidai kwamba  kama wananchi hawataichagua CCM daraja hilo halitajengwa, wakati ambapo katika kipindi hicho kulikuwa na shida kubwa ya usafiri katika eneo hilo.

Alisema Kitendo pia kilichofanywa na mbunge wa Tabora mjini Ismail Aden Rage, hakikuwa cha uungwana kwani alitumia lugha ya uongo kwa lengo la kupotosha wapiga kura ambapo alidai mgombea wa chama cha Demokrasia na Maendeleo  ( Chadema) amejitoa katika uchaguzi huo.

akizungumza na gazeti hili mara baada ya maamuzi hayo nje ya mahakama aliyekuwa mjibu rufaa  Joseph Kashndye  amekubali na kuridhika na maamuzi hayo  huku akiwalalamikia mawakili wake kwamba hawakumwelekeza kufanya hivyo.

“ Sikujua, sikuelezwa  hili ni tatizo la kiufundi  hivyo silaumu” alisema  Kashindye.

Umati wa wananchama wa chadema ambao ulijaa ndani ya chumba cha mahakama kwakweli uliondoka kwa uzuni eneo hilo la mahakama wakikibali matokeo huku wengine wakisema tukajipange kwa ajili ya uchaguzi mkuu ujao

Hata hivyo Dkt kafumu akuwepo mahakamani alipotafutwa kwa njia ya simu alisema kwamba hukumu iliyotewa na mahakama ya Rufaa ndio haki kamili kwani mwanzo alikuwa na wasiswasi na jaji yule lakini alionekana anaongopa kuangushwa .
Alisema kwamba amerejeshwa ubunge wake kwa ajili ya kuwatumikia wananchi wa Igunga bila kujali Itikadi ya chama chochiote cha siasa kwani waliompa kura na kumyima kura wote ni wananchi wa Igunga.

Dkt Kafumu alisema kwamba yale ambayo alikuwa hameyaanzisha ndio anataka kuendeleza kwa nguvu zake zote kwa ajili ya maendeleo ya Igunga na wananchi wake  kwa ujumla.

“mimi nijembe kama nilivyokuwa nasema wakati wa kampeni zangu kwamba mimi ni kwa ajili ya wananchi wa Igunga hasa vijana na wale wa vyama Rafiki na ccm “alisema Dkt Kafumu.

Aidha mwenyekiti wa ccm wilaya ya Igunga Costa Olomi alisema kwa ushindi wa kafumu ni wananchi wote wa Igunga sio wa chama bali ni kwajii ya maendeleo ya Igunga na mkoa wa Tabora .

Alisema kwamba baaada ya kurejeshwa umbunge wake chama cha mapinduzi kimepanga mapokezi makubwa ya kupokea mbunge huyo hapa mei 12 mwaka huu kwa ajili ya sherehe ya kupongeza .

MWISHO.


Wednesday, May 8, 2013

LHRC YATOA MAFUNZO KWA WAANDISHI WA HABARI WA MIKOANI KUHUSU HAKI ZA BINADAMU KWA UFADHILI WA EU -DAR ES SALAAM


Balozi wa nchi za Ulaya(EU)nchini Tanzania Filberto Sebregond(kulia )akizungumza kwenye ufunguzi wa semina ya waandishi wa habari kutoka mikoa mbalimbali nchi inayohusu masuala ya haki za binadamu,Kwenye ukumbi wa  Wanyama Hotesl Jijini Dar Es Salaam.

Picha ya pamoja Kati ya Balozi wa nchi za Ulaya(EU)nchini Tanzania Filberto Sebregond na washiriki na waandaji wa wa mafunzo ya haki za binadamu

Rose Mwalongo ambaye ni afisa habari wa kituo cha sheria na haki za binadamu(LHRC)akisalimiana na Balozi wa nchi za Ulaya(EU)nchini Tanzania Filberto Sebregond


waandishi wakimfanyia mahojiano Balozi wa nchi za Ulaya(EU)nchini Tanzania Filberto Sebregond

KISIMA CHAENDELEA KUUA WATU,WANANCHI WAKUMBWA NA HOFU KUBWA KILOLENI-TABORA MJINI

Askari wa kikosi cha zimamoto mjini Tabora wakiutoa mwili wa mwanamke ambaye amekutwa amekufa katika kisima cha maji maarufu Bombamzinga kilichopo kata ya Kiloleni Tabora mjini,Mwanamke huyo ametambulika kwa jina la Hawa Ramadhani Mzee ambaye alikuwa na umri wa miaka 42 ambaye pia inasemekana alikuwa na matatizo ya akili.
Diwani wa kata ya Kiloleni Bw.Juma Matalu (katikati)akishuhudia tukio la kifo cha mwanamke huyo katika kisima ambacho kimekuwa kikihusishwa na matukio ya mauaji ya watu kadhaa kwasasa hali inayotishia amani kwa wakazi wa kata ya Kiloleni.
Baadhi ya Askari wa Jwtz,Polisi na wa kikosi cha zimamoto Tabora mjini waliposhirikiana kuutoa mwili wa mwanamke huyo.



MAHAFALI YA CHUO CHA UTUMISHI WA UMMA TPSC YANAFANYIKA TABORA HIVI SASA.

 

 Mahafali ya 14 ya chuo cha utumishi wa umma TPSC yanafanyika hivi sasa mkoani Tabora.

AJALI KAZINI ?


 ASKARI HUYO AMBAYE JINA LAKE HALIKUPATIKANA MARA MOJA ALIKUWA ANATAKA KUSHUKA ILI HAWAI KAZINI NDIPOM GARI LIKAONDOKA NA KUNGUKA HUKU AKIWA NA BUNDUKI KIFUANI KAMA UNAVYOONA

CCM YA TUPILIA MBALI ZIARA ZA MADIWAN ZA MILL,82.3





 NA LUCAS RAPHAEL NZEGA



 

CHAMA cha mapinduzi ccm wilayani nzega mkoani Tabora kimetupilia mbali ziara iliyopangwa kufanywa na Baraza la madiwani la Halmashauri ya wilaya, iliyokadiliwa kutumia kias cha Mill,82.3 katika mikoa ya Arusha,Singida,Dodoma pamoja Moshi kwa muda wa siku kumi na nne(14) kwa malengo ya kujifunza mambo malimbali ya kimaendeleo.

Akizungumza na waandishi wa Habari mwenyekiti wa chama hicho wilaya Amosi Majire kanuda alisema kuwa kamati ya siasa wilaya ilikutana na kutoa uamzi huo kutokana na kuona wilaya inakabiliwa na changamoto mbalimbali za kimaendeleo.

Alisema kuwa mgodi wa dhahabu wa Resolute ulilipa halmashauri hiyo kias cha shilingi Bill 2.4 kama malipo ya ushuru wa huduma wa madeni nyuma,fedha hizo ziliwekwa kwenye akaunti ya amana hadi April 15 zilipo toa faida ya shilingi Mill 82.3

Alisema kwa kiwango hicho kilichotengwa kufanyia ziara kwa madiwani hao kimebadilishwa badala yake fedha hizo zielekezwe katika mambo ya maendeleo mengine yenye tija kwa wananchi.

Alisema Baraza hilo lilipanga kufungua Benki ya kijamii itakayo weza kukopesha wananchi lengo likiwa ni kuinua uchumi na kukuza wajasilia mali,kamati hiyo imetengua uanzishwaji wa benk hiyo badala yake fedha hizo kila kata itapatiwa kias cha shilingi Mill,50 hadi 61 iliwananchi waweze kufanya mambo ya maendeleo.

Kanuda alifafanua sababu za kuzuia benk hiyo ni kutokana na kuwepo kwa Taasisi mbalimbali za kibenk wilaya hapa hivyo wananchi wanafursa ya kukopo na kujiendeleza kiuchumi na kimaendeleo kwa ujumla.

‘’madiwani wanapaswa kuiangalia jamii kwanza inataka nini sio kujiangalia wao kwani ziara hiyo inatija lakini wananchi kwanza kunakero mbalimbali zipo hapa tumeamua fedha hizo wazigawe kwa kila kata na wananchi watasema wanataka nini kwani fedha hizo ni zawananchi’’alisema mwenyekiti huyo.

Alisema chama cha mapinduzi kina madiwani wengi kimeshauri mambo hayo ya msingi kwa kujali masirahi ya wananchi na kuongeza kuwa ziara za madiwani ni kwa mujibu wa kisheria hivyo ziara zao watakwenda ilikuweza kuleta maendeleo.

Alisema kabla ya kuanza ziara hiyo madiwani hao watapaswa kuwaeleza wananchi madhumuni ya ziara yao na kuwahakikishia mafanikio ya zaira hizo ili kuweza kushirikisha wananchi katika maamuzi thabiti tofauti na hili lilivyo kuwa limejitokeza pamoja na matumizi makubwa ya fedha huku wananchi wakikabiliwa na changamoto mbalimbali za kero.

Aliwataka wabunge na madiwani wote kwa ujumla kuwa Baraza la madiwani la halimashauri hiyo lijalo kubadilisha Bajeti ndogo ya fedha za ushuru wa Huduma shilingi Bill 2.4 zielekezwe kwenye mipango ya maendeleo itakayo gusa wananchi.

Hata hivyo mwenyekiti  huyo wa chama cha mapinduzi wilaya ya nzega alivitaka vyama vya upinzani kutowaposha wananchi juu ya fesha hizo bali kuwaeleza kweli wananchi hao matumizi sahihi juu ya fedha hizo kwani fedha hizo zilitowalewakwa ajili ya matumizi ya wananchi wa wilaya ya nzega.

Mkuu wa wilaya ya Nzega Bituni Msangi alipoulizwa suala hilo alisema kuwa serikali imechukua hatua za awari za kusimamisha ziara hiyo hadi pale uchunguzi na matumizi thabiti yatakapo patikana ya fedha hizo.

Alisema kuwa wilaya ya Nzega inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwa na uhaba wa madawa,madawati pamoja na zaidi ya nyumba 354 za wananchi kudondoka kutokana na mafuriko yaliyotokea mwezi March na April.

 Baraza la madiwani la halmashauri hiyo lililofanyika kati ya April 24 na 25 mwaka huu lilipitisha mchanganuo wa bajeti ndogo ya fedha za ushuru wa huduma zilizo lipwa na mgodi wa dhahabu wa resolute Bill,2.4 huku ziara ya madiwani na wabunge wawili kutumia Mill,82.3, Mill,300.7 kulipa madeni ya halmashauri pamoja na Bill,2 uanzishwaji wa Benk ya kijamii,aidha Fedha hizo zitaendelea kuwekwa kwenye akaunti ya amana hadi mchakato utakapo kamilika.

Mwisho.
 


WIALYA ZA URAMBO NA KALIUA KUKUMBWA NA BAA LA NJAA .



NA LUCAS RAPHAEL,URAMBO 

 
Wakazi wa wilaya za Urambo na Kaliua watakumbwa na baa la njaa iwapo serikali na wananchi wenyewe hawata siamamia ipasavyo utunzaji wa chakula walichovuna  kutokana na mvua kuharibu vibaya asilima  35 za hekta ya zao la mahindi  yaliyolimwa msimu huu.   Akijibu hoja za madiwani kuhusu hali ya chakula katika wilaya hizo afisa kilimo  Erasto Konga alisema kuwa  uzalishaji wa mazao ya chakula msimu huu hasa mahindi siyo mzuri kutokana na kuharibiwa na ukame  kutokana na kutonyesha mvua wakati wa mwezi   wa pili na watatu.   Konga amebainisha kuwa makadirio ya chakula kwa wakazi  564,895 wa wilaya hizo mbili ni tani 195,776  hivyo  akatoa  wito kwa madiwani hao  kuwaelekeza wananchi  kununua chakula  hasa mahindi  kutoka maeneo mengine hapa nchini.   Aliongeza kuwa zaidi ya tani 90,000 za chakula kinachozalishwa na wakulima wa wilaya hizo ni  cha wanga huku wananchi wakipendelea kutumia  kwa wingi mahindi  kama chakula   japo wananalima  mpunga ambao ufanywa kama zao la biashara.   Afisa kilimo huyo ameliambia gazeti hili kuwa kiashiria moja wapo ambacho  kinaonyesha kuwepo kwa tatizo la njaa ni kutokana na kutoshuka kwa bei ya mahindi hadi sasa kwani debe la mahindi kung’ang’ania  shilingi 9000/= badala ya thsh 3500/= au 4000/= wakati wa msimu wa mavuno hali ambayo inaonyesha kwamba mahindi hayapo.   Konga ameongeza kwamba bado wimbi la walanguzi linatishia hali ya chakula katika wilaya hizi mbili  kwani pamoja na serikali kuwahimiza wananchi wasiuze chakula lakini wengi wao ulazimika kufanya hivyo kwa ajili ya kujipatia mahitaji.   Amesema kuwa uzalishaji wa zao la muogo pia utapungua msimu huu kutokana na zao hilo kukumbwa na ugonjwa wa BATO BATO KALI  hivyo kuongeza .   Katika msimu wa kilimo wa mwaka 2012 / 2013 zilipangwa kulimwa hekta 
135, 704 za mazao ya  chakula  ambazo zilitarajia kuzalisha tani 325,465
ambapo hekta za mazao ya chakula zilizolimwa ni 131, 785 sawa na asilimia
 97 ya lengo.

 

Naye mkuu wa wilaya hiyo Anna  Magowa aliwataka watendaji kutafuta ni 
jinsi gani watakabiliana na tatizo hilo la upungufu wa chakula hasa mahindi 
ambao umekuwa ukiikumba wilaya hiyo mara kwa mara.

 

Aliongeza kuwa watafute uwezekano wa kuanzisha kilimo cha umwagiliaji
hasa utumiaji wa matone kwani ndio hatumii maji mengi kwenye mazao ya 
mahindi  kutokana na tatizo la upungufu wa mvua.

 

MWISHO.

SERIKALI YAWATAKA VIONGOZI KUWA NA NIDHAMU MAHALI PAKAZI

Na Lucas Raphael ,Siginda




SERIKALI imewataka viongozi wa kada mbalimbali pamoja na wananchi kuwa na nidhamu na uwajibikaji mahali pakazi ili iwesehemu kubwa ya mabadiliko ya kimaendeleo ya kiuchumi na sayansi na Teknolojia hapa nchini.

Hayo yamesemwa na Waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu Ubinafisishaji na uwekezaji Dkt,Merry Nagu wakati akifunga mkutano wa kuhamasisha matumizi ya sayansi na Tekinolojia kwa kuleta maendeleo ya kiuchumi kanda ya kati singida.

Alisema Serikali imelenga kukuza uchumi kwa wafanya Biashara wakubwa na wadogo kupitia sayansi na Tekinolojia ikiwa na kuzingatia nidhamu na uwajibikaji mahali pakazi.

Alisema kuwa baadhi ya viongozi hawatambui wajibu wao kwa kukosa ni dhamu na uwajibikaji mahali pakzi badala yake husababisha miradi mingi ya kimaendeleo kudorola.

Alesema viongozi wanapaswa kujitambua na kujua uwepo wao katika nafasi husika ili waweze kutekeleza kero za wananchi ikiwa na kuleta maendeleo dhabiti kwa maeneo husika.

Alisema kuwa Baraza la Biashara Tanzania (TNBC) linahakikisha mikutano hiyo inaendelea kupitia makundi mbalimbali ikiwepo na ngazi za mikoa,wilaya na kata lengo likiwa ni kuhamasisha wananchi watumie sayansi na tekinolojia katika kukuza uchumi wa ndani nje.

Waziri Nagu alisema kuwa yote hayo yanatokana na nidhamu kwa viongozi,wadau pamoja na uwajibikaji mahali pakazi ilikuweza kufikia malengo hayo.

Alisema Baraza la Biashara Tanzani TNBC limeweka malengo kuwa ifikapo mwaka 2025 litafikia malengo hayo ya kukuza uchumi kwa watanzania hususani wajasilia mali wa dogo na wa kubwa na kuondokana na umasikini.

Alisema Baraza hilo limeweka vipaumbele vitavyo changia kukuza uchumi huku vikiendelea kufanyiwa malekesho ilikufikia malengo hayo ni pamoja na upatikanaji wa maji safi,Kilimo na mifugo,miundombinu ambayo ni Barabara,Reli na Bandari lengo likiwa ni kuimalisha miundombinu hiyo.

Vipaumbele vingine ni pamoja na kuimalisha nisharti na madini ilikuweza kukuza uzalishaji,ukusanyaji madhubuti wa mapato ya ndani na je pamoja na kutoa elimu mbadala kwa wananchi dhidi ya miradi husika.

Kwaupande wake kamishina  msaidizi,mwandamizi wa polis makao makuu Dar es salaam Lucas Kusima akiwasilisha maada ya umuhimu wa usalama wa watu na mali zao katika mageuzi ya kiuchumi ya sayansi na tekinolojia kwa jamii.

Alisema kuwa jeshi hilo limejipanga kukabiliana na majambazi yanayotumia Tekinolojia  hiyo ikiwepo na huduma ya kibenki A T M,Simu za kiganjani,mitandao ya kijamii pamoja na mitandao mingne.

Kusima amewataka wananchi kutoa ushirikia wa kutosha kwa wahalifu hao kupitia Teknolojia za mawasiliano ilikuweza kukuza uchumi huo na kuimalisha ulinzi na usalama kwa mali za wananchi ikiwa na wananchi kwa ujumla.

Mkutano huo wa kuhamasisha matumizi ya sayansi na tekinolojia kwa kuleta maendeleo ya kiuchumi umeyakutanisha makundi mbalimbali wakiwepo wakuu wa wilaya,wakurugenzi wa halmashauri za wilaya na mikoa pamoja na wakuu wa mikoa kwa mikoa mitatu ikiwa ni Singida,Tabora na Dodoma.

Mwisho.