Wednesday, March 20, 2013

RHINO RANGERS YAREJESHA LIGI KUU TABORA

NA LUCAS RAPAHEL 
 

Baada ya miaka 12 kupita hatimaye mkoa wa Tabora umefanikiwa kupata timu itakayoshirikia katika  ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara  msimu ujao wa 2013/2014 kupitia timu ya Rhino Rangers inayamilikwa na jeshi la wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Kabla ya  timu hiyo kuweka rekodi mpya kwa mara ya mwisho timu ya Milambo ya Tabora ilishuka ligi daraja la kwanza Tanzania bara mwaka 2000 ,timu ambayo chanzo chake ni aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Tabora kwa wakati huo Dk Laurent Gama kwani alipoteuliwa kuwa katibu mkuu wa CCM ndio ukawa mwanzo wa timu hiyo kupoteza mwelekeo katika medani ya soka nchini.  .

Lakini historia ya soka la mkoa wa Tabora imechukua sura mpya kufuatia timu pekee ya Jeshi la wananchi Watanzania, Rhino Rangers  kujihakikishia nafasi ya kushiriki  ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara baada ya kuongoza kundi C la ligi daraja la kwanza lililokuwa na ushindani wa aina yake ikiwa imefikisha pointi 29 huku ikiwa na  mchezo mmoja,pointi ambazo hazitaweza kufikiwa na timu yoyote katika kundi hilo.

Timu ambazo zilizopo  katika kundi c ni Kanembwa JKT, Polisi Dodoma, Polisi Tabora, Mwadui, Pamba, Polisi Mara, Molani ya mkoa wa Manyara na Rhino ambaye ndio mbabe wa kundi hilo.

Akizungumza na mwandishi wa makala haya mlezi wa timu hiyo ya Rhino Mnadhimu Mkuu wa Mafunzo na Utendaji wa Kivita wa Faru ya Brigedi  Kanali Simon Hongoa amesema kwamba mafanikio ya timu hiyo hayakuja  kama mvua  bali wampitia vikwanzo vingi na hatimaye mafanikio ambayo yanaonekana hii leo .

Amesema kwamba Rhino Rangers ilianza mwaka 1994 baada ya kuvunjika kwa timu ya divisheni ya 20 mwaka 1993 na kuanzia hapo Rhino ilianza kusukwa ili iwe timu ya ushindani ndani na nje ya mkoa wa Tabora.


Kanali huyo wa JWTZ  amesema kwamba  timu hiyo ilianzia daraja la nne, kupanda  hadi kufikia daraja la tatu na la  pili kupitia mfumo wa zamani wa FAT kabla ya mabadiliko  ya ushiriki wa madaraja ya soka kufanywa na shirikisho la soka nchini TFF..

Amesema kwamba katika vipindi tafauti ya mashindano hayo kunzia mwaka 1995 hadi mwaka 1999 walishindana kwa kila hali kupanda daraja la kwanza lakini walikutano na vikwanzo vingi ingawa hawakukata tamaa ya kushiriki katika ligi hiyo licha ya kuwa mabingwa wa mkoa mara kadhaa .

Katika jitiada zao waliweza kufikia nafasi ya tano kwa makundi ,kwa mfano mwaka 1998 walishiriki ligi daraja la kwanza na kufakikiwa kushika nafasi ya tano na kuachwa na timu  zingine zikipanda ligi kuu.
Katika harakati za kufanya vizuri timu hiyo ilivunjwa kwa mara nyingine  mwaka 1999 hadi mwaka 2006 ilipofufuliwa tena  baada ya ujuo wa kanali huyo wa jeshi la wananchi kufika katika kanda hii ya Magharibi.

Kanali Hongoa amesema wakati timu hiyo ilikuwa na mambo mengi yaliyopelekea  kufutwa tena kwenye anga la soka.Mwaka 2007   ilishiriki ligi daraja la tatu ngazi ya taifa na kufanikiwa kuwa bingwa wa mkoa wa Tabora mwaka wa 2008.

Amesema jitiada zao zilianza mwaka 2009 na mwaka 2010 waliweza kushika nafasi ya tano kati ya timu zilizoshiriki katika ligi ya makundi wakati huo iilifanyikia mkoa wa tanga na kufaniwa kuingiza timu za Costal Union,Villa Squad,oljoro JKT na Moro utd ..

Lakini aliendelea kusema kwamba jitihada zao  walitegemea wangeweza kupanda ligi kuu mwaka 2011 lakini walitimuliwa vumbi na timu za Polisi moro ,JKT Mgambo,na Prison ya Mbeya ambazo zilifanikiwa kuingia ligi ya kuu ya Vodacom wakati huo ligi ya makundi ilifanyika nkoa wa Morogoro..

Pamoja na vikwazo hivyo hawakukata tamaa ya kuendelea kushiriki na kuwania nafasi ya kupanda ligi kuu huku  wananchi wa mkoa wa Tabora waliweza kuwatia moyo na jitiada za wachezaji wake wamefanikiwa kuingia ligi kuu hiyo ya Vodacom  Tanzania bara.

Amesema kwa hiyo ni faraja kwa Jeshi la Wananchi kwa kupata hata timu moja inayoshiriki ligi kuu ya soka  nchini kwani timu zinazoshiriki ligi hiyo zinamilikiwa na  Jeshi la Kujenga Taifa  JKT na zinafanya vizuri kwa sasa .

Kamanda huyo kwa jina maarufu “babu” amesema kwamba jitihada zilizopo ni kuhakikisha Rhino inafanya usajiri wa kufa mtu kwani wanataka kuwa na timu bora na sio bora timu.

“hatutaki kunusa tu katika ligi hiyo na mwaka unaofuata tusiwepo hilo kwetu hatulitaki kusikia bali mshikamano kutoka kwa wananchi wa mkoa wa Tabora kwani ndio nguzo kubwa  toka mwanzo kwa ligi hii inayotarajiwa kumalizika tarehe 17 mwezi huu” .Amesema kanali Hongoa.


Ametaja kikosi kilichoweza kupandisha timu hiyo ya Jeshi la wananchi wa Tanzania kuwa makipa ni Idd Kihulya,Charles Mpinki na Abdullakarim Mtumwa.

Mabeki wa pembeni kulia na kushoto ni Salum Mambo ,James Barton ,Frank Konye ,Ally Mwanyiro ,Stanley Mlay na Joseph Mapunda.

wengine ni viungo ambao ni Stanlaus Mwakitosi ,Ramadhani Sheweji ,Emanuel Noel ,Steven Maztudd ,Bakari Maadhi na Salum Majid.

Pia amewataja viongo wa kati ni Julias Masunga, Issa Salum, Ayub Iddy, Joseph Sangadata na Ussi Makeme ,hao wakifuatiwa na washambulia wa Timu hiyo ambao ni Shija Joseph ,Magesa omary ,Doi Mobi ,Msafiri Mbilinyi, Samwel Mwamasangura,shija Mvugo Abdallh Simba,Victor Anghaya Abbas  Mohamed  na Mchembi Maganga.

Hata hivyo kanali Hongoa  amewashukuru wakazi wa mkoa wa Tabora wakiongozwa na mwenyekiti wa CCM mkoa wa Tabora, Hassan Wakasuvi, mkuu wa mkoa, mkuu wa wilaya ya Tabora na wadau wote wa soka ambao wamejitolea kwa hali na mali ili kufanikiwa kwa timu hiyo kufika hapo ilipofika leo.

Aidha kocha wa timu hiyo ya Rhino Renatus Shija amesema kwamba halipofika katika timu hiyo aliangali history ya  Rhino na baada ya kuangali aliweka mkakati wa kuhakikisha wana maliza raun di  ya kwanza wakiwa wanaongoza ligi daraja la kwanza na hivyo kuhakikisha watoki katika nafsi hiyo hali iliyowasaidia sana kufika hapa walipofikia.

Mara baada ya kumaliza raundi ya kwanza na kuongoza kundi C  kwa pointi 17 wakapanga kuhakikisha wanashinda michezo mitano waliyopangiwa kucheza katika uwanja wa nyumbani  wa Ally Hassan Mwinyi katika mzunguko wa pili wa ligi hiyo ili waweze kuongoza na kupanda daraja jambo ambalo wamefanikiwa.

Amesema kwamba amependa ushirikiano kutoka kwa viongozi wa timu hiyo ya Jeshi na wananchi wa mkoa wa Tabora  kuwapa sapoti ya nguvu kwa wameina timu hiyo kama yako.

Kwa sasa wanampango wa kuhakikisha wanapata timu bora yenye wachezaji wenye uzoefu na ligi hiyo ,kwani ligi kuu ni mambo mengi ambayo yanabidi kuyafanyika kazi kabla ya ligi hiyo kuanza na kuongeza kwamba anataka tinu hiyo ya Rhino kuweka history ya kuchukua ubingwa wa bara mwakani .

Kapteni wa Timu ya Rhino  Shija Joseph amesema kwamba mafaniko ya timu hiyo ni mikakati ya viongozi wa jeshi hilo ,viongozi wa serikali pamoja na wananchi wa mkoa wa Tabora kwa kupatia ushirikiano mkubwa na kuhakikisha wanafika hapo walipofika leo.

Mwenyekiti wa chama cha soka mkoa wa Tabora (TAREFA)   , Yussuph Kitumbo alisema kwamba lengo la kukikisha timu mojawapo ambazo zilishirikia kwenye ligi daraja la kwanza mwaka huu mkooani hapa zinapanda  na hilo,limewezekana

 “Nina imani kuwa sisi kama TAREFA,serikali ya mkoa,wadau na wapenzi tukishikamana nina imani kubwa soka ya Tabora inakuwa kwa kasi kwani kuna vipaji vingi sana mitaani ambavyo vijana waliopo wanapaswa kuendelezwa katika michezo mbalimbali.” Alisema Kitumbo.

Amesema kwamba baada ya timu ya Rhino kufikia hapo ilipofikia basi uzalendo kwanza ili tuonyeshe mapenzi ya kweli na timu hiyo ambayo kwa sasa ni ya wana Tabora wote .

Mwisho

TAASISI ZA SERIKALI ZAONGOZA KWA MADENI YA ANKARA ZA MAJI TABORA

 
Na LUCAS RAPHAEL TABORA, 

MAMLAKA ya maji safi na maji taka Tabora (TUWASA), imetaja wateja wake
ambao ni wadaiwa sugu ambao ni taasisi 13 za serikali, binafsi na
taasisi za dini hadi kufikia februari 28,2013 ambao wanadaiwa zaidi ya
sh milioni 6.1.

Akisoma taarifa yake siku ya uzinduzi wa wiki ya maji katika manispaa
Tabora,mkurugenzi wa mamlaka hiyo, Injinia Bwire Mkama alisema wadaiwa
sugu waliowengi ni taasisi za serikali,mashirika ya umma na taasisi
binafsi.

Injinia Mkama alitaja jeshi la wananchi wa Tanzania,(JWTZ),sh milioni
506,766,028,ikifuatiwa na jeshi la polisi sh milioni 96,612,465,ofisi
za serikali sh milioni 18,126,401,vyuo vya umm ash milioni 12,327,670
na shule za msingi milioni 11,408,598.

Aidha alitaja taasisi nyingine kuwa ni jeshi la Magereza sh milioni
9,547,815,TRC sh milioni 5,339,274,taasisi za dini ya kiislamu sh
milioni 4,427,202,hospitali ya mkoa wa Tabora,Kitete sh milioni
3,738,380,halmashauri ya manispaa Tabora 3,261,140,shule za sekondari
sh milioni 3,084,984.58,taasisi za dini ya kikristo sh milioni
1,729,195 na ofisi ya RAS mkoa wa Tabora sh milioni 1587,690.

Aidha mkurugenzi huyo alizitaja shule za msingi zinazodaiwa hadi
kufikia mwezi machi 15,2013 kuwa ni shule msingi Kiloleni sh
903,000,shule msingi jamhuri sh 539,800,shule ya msingi Gongoni sh
2,073,000.

Alizitaja  taasisi nyingine kuwa ni shule ya msingi Mkoani sh 363,000
na shule msingi Uhuru sh 1,189,550, Cheyo shule ya msingi sh 706,500
na shule ya msingi Igambilo sh 409,355.
Injini Mkama alisema inafikia mahali huduma kama za madawa wanashindwa
kununua kwa wakati kwani fedha nyingi kwa ajili ya uendeshaji inatuwia
vigumu.

Alisema hivi sasa kuna operesheni ya kudai wadaiwa sugu na
tumewasiliana na serikali ya wilaya ili watusaidie kudai madeni kwa
wateja wetu ambao na taasisi za serikali ambazo sehemu kubwa ya deni
ni taasisi hizo.

UJENZI WA CHUO CHA MUSOMA UTALII TABORA WAENDELEA VIZURI


 Sehemu ya Jengo la utawala katika Chuo cha Musoma Utalii kilichopo mkoani Tabora ambacho kimejengwa kata ya Ipuli mjini Tabora,mara baada ya kukamilika chuo hicho kinatarajia kuongeza idadi ya wanafunzi.
Mkurugenzi mtendaji wa Chuo cha Musoma Utalii Bw.Shaban Mrutu akitembelea na kuangalia maendeleo ya ujenzi wa Chuo hicho unaoendelea kwa kasi huku ikikadiriwa kuwa huenda chuo hicho kikafunguliwa kati ya mwezi Juni na Julai.

TUWASA YATOA MSAADA WA MIL.3KATIKA WIKI YA MAJI

 Mkuu wa wilaya ya Tabora Bw.Suleiman Kumchaya akikabidhi mfano wa hundi ya shilingi mil.3 kwa mwalimu mkuu wa shule ya msingi Chemchem kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa darasa katika shule hiyo fedha zilizotolewa na Mamlaka ya maji Safi na Maji taka mjini Tabora Tuwasa wakati wa ufunguzi wa wiki ya maji.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Tuwasa Mchungaji Paul Misigalo akizungumza na wananchi wakati wa wiki ya maji.
 Watumishi wa Tuwasa  Mwanasheria na mhasibu wakijaribu kushauriana jambo katika picha waliokuwa wakiangalia kwenye kamera ya Digital
 Watalaam wa Tuwasa wakisikiliza kwa makini hotuba ya mkuu wa wilaya katika uzinduzi wa wiki ya maji
 Mkuu wa wilaya Bw.Suleiman Kumchaya akizungumza na wananchi katika uzinduzi huo wa wiki ya maji
 Afisa habari wa Tuwasa akimsikiliza kwa  makini mkuu wa wilaya na huku akitafakari namna atakavyowezesha Mamlaka hiyo kujitangaza kwa mwaka huu wa 2013 kwa maana ya uboreshaji wa huduma kwa wananchi.
Kutoka kushoto ni Meya wa manispaa ya Tabora Bw.Ghulam Dewji pamoja na mjumbe wa bodi ya Tuwasa na Mwenyekiti wa UWT mkoa wa Tabora Bi.Mwanne Mchemba.

"VIONGOZI WA IGUNGA WALIMDANGANYA RAIS KIKWETE KUHUSU KERO YA MAJI IGUNGA"CHADEMA

 
 Baadhi ya wananchi wa wilaya ya Igunga wakiwa katika mkutano wa hadhara ulioitishwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema kuzungumzia kero ya maji wilayani humo iliyodumu kwa muda mrefu.
 Kiongozi wa Chadema Kamanda Mwita Waitara akizungumza na wakazi wa wilaya ya Igunga ambapo alitumia fursa hiyo kumuomba Rais Kikwete kuliangalia upya suala la kero ya maji wilayani humo ambapo alidai kuwa baadhi ya viongozi ngazi ya wilaya hawakumwambia ukweli Rais Kikwete juu ya kero hiyo ya maji inayoendelea kusumbua wakazi wa Igunga.

 Mkurugenzi wa Chadema anayeshughulikia Bunge na halmashauri Bw.John Mrema akizungumza katika mkutano huo wa hadhara ambao ulihudhuriwa na idadi kubwa ya wakazi wa Igunga.
 Wakazi wa Igunga wakichangamkia kununua kadi za Chadema mara baada ya mkutano huo wa hadhara.
 Mkurugenzi wa Organaizesheni makao makuu ya Chadema Bw.Benson Kigaila naye alipataa fursa ya kuzungumza katika mkutano huo.

CHUO CHA MUSOMA UTALII CHAIPIGA TAFU TIMU YA RHINO FC

 

 Mkurugenzi wa Chuo cha Musoma Utalii Tabora Shabani Mrutu akikabidhi msaada wa shilingi mil.moja kwa kiongozi wa timu ya Rhino Fc Hajin Kubeja ambayo inatarajiwa kuanza kucheza ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara kwa msimu ujao,aidha Mkurugenzi huyo ameahidi kuendelea kutoa msaada kwa timu hiyo.

TABORA TUNAJIPENDA NA RHINO YETU...LIGI KUU HIYOOOOOO LIGI KUU VODACOM"

 

Mmoja kati ya wachezaji wa Rhino akibebwa na washabiki baada ya mechi kali dhidi ya Polisi Dom

Baadhi ya mashabiki wa Rhino wakiwa jukwaani wakishangilia timu yao katika mtanange kati ya Rhino na Polisi Dom.

Baadhi ya watangazaji wa Radio CG FM ya hapa mkoani Tabora wakitangaza mechi kati ya Rhino na Polisi Dodoma ambapo Rhino iliicharaza Polisi bao moja kwa sifuri katika uwanja wa Ally Hassan Mwinyi mjini Tabora

"ASKARI POLISI WANNE WANAODAIWA KUFANYA MAUAJI YA MTU MMOJA URAMBO WAREJESHWA KAZINI KIMTINDO"


 

"INAUMA SANA SIJUI HAWA ASKARI POLISI NI WATOTO WA VIGOGO?"



HALI HALISI YA MAUAJI YA HASSAN MGALULA:

Askari Polisi hao wakati wakimchukua kwenye usafiri wa Bajaji ya mizigo huku wakiwa  wamemkanyaga bila kujali hali mahututi aliyokuwanayo marehemu Hassan Mgalula mara baada ya kipigo kikali kilichosababisha kifo chake hapo baadaye,INASEMEKANA KUWA  WALIPOFIKA  KITUONI  WALIFUNGUA  JALADA  LILILOONESHA  KUWA HASSAN  AMEPIGWA  NA  WANANCHI  WENYE  HASIRA  KALI......(Picha hii kwa hisani ya Nassor Wazambi-Aliyekuwa Mwenyekiti UVCCM wilaya ya Tabora mjini.) 

POLISI wanne waliokuwa wanaodaiwa kuhusika na tuhuma za  mauaji ya mtu mmoja huko Wilayani Urambo ambao walifukuzwa kazi baada  ya kufikishwa mahakamani imedaiwa kuwa wamerejeshwa kazini huku yakizuka maswali mengi yasiyo na majiibu  juu ya kuachiwa kwao.

Askari Polisi hao ambao walifukuzwa kazi mnamo March 5 mwaka 2012 baada ya kubainika wamehusika na tukio hilo la kinyama la kumpiga hadi kupoteza fahamu marehemu Hassan Mgalula ambaye baade alipoteza maisha ni namba  G 3037 Pc Aidano, namba G 3836 Pc Jonathan, namba G 4836 Pc Mohamed na mwingine ni namba G 5382 Pc Khakimu.

Kuachiwa na kurejeshwa kazini  kwa askari Polisi hao wanne kumezua hali ya sitofahamu kuanzia  kwa askari Polisi wenzao hadi kwa wananchi wa wilaya ya Urambo ambao waliobahatika kulishuhudia tukio la kumpiga raia huyo wa Urambo marehemu Hassan Mgalula na baadae kufariki dunia kabla ya kufikishwa kituo cha Polisi ambako lilifunguliwa jalada kwamba ameuawa na wananchi wenye hasira kali.

Aidha juhudi za kumtafuta kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora ACP Athony Rutha ili kutolea ufafanuzi juu ya kurudishwa kazini kwa askari hao zinaendelea lakini kumekuwa na dalili za utata kutokana na askari hao imeelezwa kuwa kuna mikono ya vigogo wa Jeshi la Polisi ngazi ya juu.

Baadhi ya wananchi wa wilaya ya Urambo kutokana na tukio la kurejeshwa kazini kwa askari hao wanaodaiwa kufanya unyama huo mnamo Februari 29 mwaka 2012 wameonesha dalili za kukosa imani na Jeshi hilo huku wakilalamikia uongozi wa Polisi ngazi za juu kwa kuendelea kuwabeba baadhi ya askari wanaotenda makosa kinyume cha sheria. 

RADI YAJERUHI WANAFAMILIA NA KUSAMBARATISHA MAKUNDI YA MBUZI SIKONGE

 

Na Lucas Raphael  Sikonge

MVUA zinazoendelea kunyesha katika wilaya ya Sikonge, zimeleta madhara kadhaa, baada ya watu wanne wa familia moja kulazwa hospitalini kutokana na mshituko wa radi.

Akizungumza na gazeti hili diwani wa kataka Kilolelo Boniface Mlimakala Mtani, alisema tukio hilo la radi lilitokea hivi karibuni, ambapo familia hiyo ilipata mshituko na kulazwa hospitalini huku mbwa wanne na mbuzi mmoja wa familia hiyo wakipigwa radi na kufa hapohapo.

Mtani alisema kuwa tukio la radi lilitokea ,ajira ya saa nane mchana,mwezi machi 8,mwaka huu katika kitongoji cha Maweni B,kijiji cha Kanyamsenga,kata ya Kiloleli.

Aliwataja waliojeruhiwa na kulazwa hospitali,(DDH),wilayani Sikonge,kuwa ni Aloyce Masima,(45),ambaye alijeruhiwa sehemu ya mguuni kama amemwagiwa maji ya moto,Paulo James(18), Hoka Kazinza (16),na Gabriel Aloyce (2).

Mtani aliongeza kuwa familia hiyo ililazwa hospitali kwa siku moja kabla ya kuruhusiwa kurejea nyumbani,kati yao watoto watatu walipata mshituko wa radi huku baba yao akibabuliwa mguuni na radi hiyo.

Akiongea zaidi diwani huyo alisema baada kupata taarifa hizo alifika nyumbani walipokuwa wakiishi na kukuta wamepoteza fahamu huku mbwa wanne na mbuzi mmoja wakiwa wameshakufa kwa kupigwa na radi hiyo.

Hata hivyo diwani huyo alisema kuwa licha ya familia hiyo moja kupigwa na radi,hakukuwa na mvua yoyote kijijini hapo zaidi ya kuwepo mawingu,huku mvua ikiwa inanyesha kilomita moja toka eneo la tukio.

Katika hatua nyingine Mtani aliongeza kuwa zoezi la kuwasaka watoto wanaotakiwa kuingia sekondari baada ya kufaulu bado linaendelea na limeanza kuzaa matunda.

DC NZEGA AWATAKA WALIOVAMIA HIFADHI YA MISITU IPALA KUONDOKA MARA MOJA.

Na Lucas Raphael, Nzega.

Serikali wilayani Nzega katika mkoa wa Tabora imeagiza wananchi wote waliovamia misitu ya hifadhi ya Ipala iliyoko katika kijiji cha Ugembe, kata ya Mwakashanhala wilayani humo kuondoka mara moja kwa hiari yao, vinginevyo wataondolewa kwa nguvu.

Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa wilaya ya Nzega, Bi. Zaituni Msangi wiki iliyopita katika doria maalumu ya kutembelea misitu hiyo ambayo iliripotiwa kuvamiwa na wananchi hao na kuendesha shughuli za aina mbalimbali kinyume na taratibu.

DC alisema kuwa wameamua kuchukua hatua hiyo baada ya kuona vitendo vya uvamizi wa maeneo maalumu yaliyohifadhiwa na serikali vikiendelea kuongezeka hapa nchini hali inayochangia kwa kiwango kikubwa uharibifu wa mazingira.

‘Hawa watu hawastahili kuishi katika maeneo haya, uwepo wao ni kinyume na sheria, lakini pia wanaharibu mazingira ya hifadhi hizi za serikali, kwa sababu wanakatakata miti ovyo kwa ajili ya shughuli zao za kilimo, ufugaji na uchomaji mkaa sambamba na uvuvi wa samaki’, alisema DC.

Aidha, DC alibainisha kuwa wananchi waliovamia hifadhi hiyo ya Ipala wamekuwa wakidanganywa na baadhi ya watu wanaojifanya kuwa ni maofisa wa serikali ili watoe hela kwa kisingizio cha kuwamilikisha maeneo hayo bila kutambua kuwa mtu yeyote haruhusiwi kuweka makazi katika maeneo ya misitu ya hifadhi.

‘Tayari tumeweka kikosi kazi cha kufanya doria katika maeneo hayo, na tumeshapewa taarifa za uwepo wa mtu mmoja anayewarubuni wananchi hao kwa kujifanya kuwa yeye ni ofisa wa serikali na ameahidi kuwagawia viwanja katika maeneo hayo ya hifadhi, tumeshaweka mtego wa kumkamata’, aliongeza DC.

DC alibainisha kuwa doria hiyo inayofanywa na watu 18 kutoka vikosi vya FFU, wanyama pori, wataalamu wa maliasili na mgambo, tayari imefanikisha kukamatwa kwa magunia 400 ya mkaa ambao ulikuwa umehifadhiwa katika nyumba zilizoko ndani ya msitu huo wa hifadhi, japo watuhumiwa wote walifanikiwa kukimbia.

Katika msako huo mbali na kukamatwa kwa magunia hayo ya mkaa, kikosi hicho pia kilifanikiwa kukamata gobole 1 na silaha zingine za kijadi zilizokuwa zikitumiwa na wavamizi hao katika msitu huo na bado msako unaendelea, mpaka wahakikishe wavamizi wote wamerudi kwao sambamba na kukomesha usafirishaji wa mkaa.

Aidha, DC aliongeza kuwa katika jitihada za kuhakikisha kuwa uvamizi huo wa hifadhi unadhibitiwa, wameamua kuitisha kikao cha ujirani mwema ili kuweka mikakati ya pamoja na kulifanya zoezi hili kuwa endelevu kwa kuwashirikisha wakuu wa wilaya jirani za Shinyanga, Kishapu na Nzega yenyewe.

KIBANDA APELEKWA AFRIKA KUSINI KWA MATIBABU

 


Mhariri Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya New Habari (2006) Limited, Absalom Kibanda, akiwa ndani ya Ndege ya Flightlink.


 Absalom Kibanda akiwa na mkewe ndani ya Ndege, Anjella Semaya, tayari kuanza safari ya kuelekea nchini Afrika ya Kusini kwa matibabu.(Picha na Amanitanzania)

 Baadhi ya waandishi na viongozi wa jukwaa la wahariri wakiwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbi kwa ajili ya kumjulia hali.

 Absalom Kibanda akiwa amelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kabla ya kusafirishwa kwenda Afrika ya kusini.

 Wafanyakazi wa Kampuni ya Ndege ya Flightlink wakimpandisha Absalom Kibanda ndani ya Ndege.

 akiwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimili


 Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya New Habari (2006) Limited, Hussein Bashe akizungfumza na waandishi wa habari kuhusiana na tukio la kutekwa kwa, Absalom Kibanda

 Mwenyekiti wa CHADEMA, Freema Mbowe akimjulia hali Absalom Kipanda katika Hospitali ya Taifa ya Mhumbili Dar es Salaam. Picha na Amanitanzania

MAAFISA KILIMO WAGEUKA WAZURULAJI TABORA"WAILILIA SERIKALI KWA KUWAWEKEA VIKWAZO KATIKA AJIRA"

 

 

Baadhi ya maafisa kilimo  na  mifugo  wakiwa mitaani  baada  ya  kukosa ajira Serikalini,Imeelezwa  kuwa  wamejaribu  pia kutafuta ajira kwenye mashirika binafsi lakini wamekataliwa kwa kigezo kuwa mashirika hasa yanayojihusisha na ununuzi wa zao la tumbaku yamepigwa marufuku na serikali kuajiri maafisa kilimo waliosomeshwa kwa gharama  za serikali na hivyo kwasasa maafisa hawa wamejikuta kila siku wakizurula mitaani pasipo ajira.