Wednesday, October 9, 2013

SERIKALI INATAMBUA FURSA ZA WALEMAVU WILAYANI UYUI MKOANI TABORA

MRATIBU WA WAJASILIAMALI NA HAKI ZA KAZI KWA WALEMAVU WILAYA YA UYUI MKOANI TABORA HUSSEIN GEYA AKISOMA RISALA MBELE YA NKUU WA WILAYA YA UYUI LUCY MAYENGA

MWENYEKITI WA CHAMA CHA WALEMAVU MANISPAA YA TABORA JOHN KUKA AKIMKARIBISHA MKUU WA WILAYA YA UYUI KWA AKIJI YA KUFUNGUA MAFUNZO

MKUU WA WIALAYA UYUI LUCY MAYENGA AKIFUNGUA MAFUNZO YA UJASILIAMALI NA HAKI YA KAZI KWA WATU WENYE ULEMAVU KATIKA  UKUMBI WA KITUO CHA WANAFUNZI MJINI HAPA LEO

PICHA YA PAMOJA KATI YA MKUU WA WILAYA YA UYUI LUCY MAYENGA NA WATU MALI WENYE ULEMAVU MARA BAADA YA KUWAFUNGULIA MAFUNZO YA UJASILIA MALI NA HAKI YA KAZI KWA WATU WENYE ULEMAVU


NA LUCAS RAPHAEL TABORA




Halmashauri ya wilaya uyui mkoani Tabora kwa mwaka huu imetenga kiasi cha shilingi milioni 40 kwa ajili ya kuwakopesha  vijana na wanawake ili kuweza kujiongezea kipato na kujiunga katika vikundi  .
Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa wilaya ya Uyui Lucy mayenga wakati akifungua mafunzi ujasiliamali na haki za kazi kwa walemavu iliyofanyika katika ukumbi wa kituo cha wananafunzi mjini hapa .
Alisema kwamba fedha hizo zitolewa katika makundi hayo ambapo vijana wametengewa kiasi cha shilingi milioni 20 na wanawake wametengewa kiasi kama hicho.
Alisema kwamba fedha hizo ukopeshwa kwa riba nafuu ili kuwawezesha vijana na kinamama  kufanya marejesho bila maumivu  .
Mkuu huyo wa wilaya aliwataka walemavu hao kujiunga katika vikundi ambavyo vimesajiliwa na kuandaa andiko sanjari na kuwa na wathamini.
Awali mratibu wa mafunzo hayo Hussein Geya alisema kwamba mafunzo hayo yanalengo la kuboresha maisha ya watu wenye ulemavu kupitia vikundi vya wajasiliamali vya watu wenye ulemavu kutoka katika wilaya hiyo ya uyui vilivyowezeshwa kikamilifu na kutambulika kisheria.
Alisema kwamba katika kipindi cha utekelezaji mradi huo shughuli mbalimbali zitafanyika ikiwemo kutoa elimu kwa ajia ya redio na televishini ,kuendesha mafunzo mbalimbali ya ujasiliamali kwa watu wenye ulemavu .

 Mafunzo hayo yameandaliwa na chama cha walemavu wilaya ya uyui mkoani Tabora na kufadhiliwa na shirika la Akiba Uhaki Foundation la nchini kenya




Wednesday, October 2, 2013

SIKU YA WAZEE DUNIANI,WAZEE TABORA WANAHITAJI WAPATIWE MAENEO YA KUPIGIA STORY


Maandamano ya Wazee wa mkoa wa Tabora wakisheherekea Siku ya Wazee Duniani. 

"POLISI ATAKAYEWASUMBUA BODABODA SASA KUKIONA"-RC FATMA MWASSA


Mkuu wa mkoa wa Tabora Bi.Fatma Mwassa  akizungumza na wananchi wakati wa ufunguzi wa Ofisi ya Chama Cha Waendesha Bodaboda mkoa wa Tabora TTMA zilizopo eneo la Bachu kata ya Gongoni manispaa ya Tabora.Katika ufunguzi wa Ofisi hiyo pamoja na mkuu huyo kuwataka waendesha Bodaboda kufuata sheria za usalama barabarani lakini akatumia fursa hiyo kukomesha vitendo vya baadhi ya askari Polisi wasio waaminifu kutowafanya waendesha Bodaboda kuwa sehemu ya kipato chao kwa kuwalazimisha kutoa rushwa baada ya kuwabambikiza makosa wasiokuwa nayo.Aidha  Bi.Fatma Mwassa alisema serikali haitakubali kuvumilia vitendo vya kuwanyanyasa  Bodaboda ambao wamekuwa wakijitafutia riziki zao kwa kufanya shughuli hiyo ya halali.
 Mkuu wa mkoa wa Tabora Bi.Fatma Mwassa akikata utepe ikiwa ni ishara ya ufunguzi wa ofisi hiyo ya  Chama cha Waendesha Bodaboda Tabora,kushoto ni Mwenyekiti wa Chama hicho Bw.Waziri Kipusi.

Mkuu wa mkoa wa Tabora Bi.Fatma Mwassa akipata maelezo ya uendeshaji wa ofisi ya Chama cha Waendesha Bodaboda Tabora,hapa alikuwa akiangalia orodha ya wanachama ambao inaonesha mahali wanapoishi,takwimu za ajali pamoja na mahusiano yao na Jeshi la Polisi mkoa wa Tabora.
Mkuu wa mkoa wa Tabora Bi.Fatma Mwassa,mkuu wa wilaya ya Tabora mjini Bw.Suleiman Kumchaya,viongozi wa chama cha Waendesha Bodaboda Tabora  pamoja na wanachama hai wa Chama  hicho muda mfupi mara baada ya ufunguzi rasmi wa ofisi hiyo.  

TAMASHA LA MUNDE STAR SEARCH LIMEGHARIMU ZAIDI YA SHILINGI MIL.TISA

 
Maelfu ya baadhi ya  wananchi mjini Tabora wakishuhudia fainali ya Tamasha la kuibua vipaji kwa wasanii mbalimbali lililojulikana kama MUNDE STAR SEARCH lililofanyika katika viwanja vya Stand ya zamani ya mabasi.
Mabondia wawili kutoka Camp mbalimbali za Boxers wa Tabora walipokutana jukwaani kwa ajili ya kutafuta ushindi katka mashindano hayo yaliyodhaminiwa na Mbunge wa Vitimaalum mkoa wa Tabora Mh.Munde Tambwe ambaye pia ni mjumbe wa halmashauri kuu ya CCM Taifa. 
Mdhamini mkuu wa Tamasha la Munde Star Search ambaye pia ni Mbunge wa vitimaalum mkoa wa Tabora Bi.Munde Tambwe akisalimiana na wapiga masumbwi wanawake wakati wa Tamasha hilo ambalo linatajwa kuwa litakuwa likifanyika kila mwaka lengo likiwa ni kuibua vipaji vya wasanii chipukizi mkoa wa Tabora.
 Wapiga masumbwi uzito wa juu katika Tamasha la Munde Star Search wakichuana vikali na kuonekana kuwa kivutio kikubwa katika Tamasha hilo lililogharimu zaidi ya shilingi Milioni tisa.
Wachezaji wa Karate ambao nao walipambana vikali katika Tamasha hilo kwa muda wa dakika sita