Friday, June 27, 2014

SUMATRA TABORA YAJIPANGA KUELIMISHA ABIRIA JUU YA HAKI ZAO WAWAPO SAFARINI




 
NI DHAHIRI abiria walio wengi hawajui haki zao ni zipi wanapokuwa safarini na hata ajali inapotokea au gari kuharibika au kukatishwa safari kabla ya kufika mwisho wa safari iwe kwa usafiri wa majini au nchi kavu hawajui haki zao ni zipi au wafanye nini.

Kwa mantiki hiyo Mamlaka ya Usafiri wa Nchi Kavu na Majini  ( SUMATRA) mkoani TABORA  imedhamiria  kutoa elimu ya matumizi bora ya vyombo vya usafiri na haki za abiria wanaotumia vyombo hivyo.

Afisa  mfawidhi  wa SUMATRA mkoani Tabora  Joseph  Michael  anabainisha kuwa mamlaka hiyo imeamua kuchukua hatua hiyo ili kupunguza kero mbalimbali zinazowakabili watumiaji wa vyombo hivyo vya moto ambazo zinapelekea wengi wao kupoteza haki zao za msingi ikiwemo kupoteza mali, kupata ulemavu au kifo.

Michael anaongeza kuwa kama watumiaji wa vyombo hivyo watakuwa na  uelewa wa kutosha juu ya haki zao na uelewa wa sheria na kanuni za usalama wa barabarani ajali na misuguano kati ya abiria, makondakta au mwenye chombo itapungua kwa kiasi  kikubwa.

Aidha  anasema katika  mwaka  wa fedha  wa 2014/2015 SUMATRA imeweka  mkakati wa  kutoa mafunzo kwa watumiaji wa vyombo vya usafiri ili wasafiri hao waweze kujua wajibu na haki yao ya kupata taarifa mbalimbali pindi wanapokuwa safarini.

Anasema kama wasafiri hao wakijua haki zao pindi wanapokuwa safarini watakuwa na uwezo wa kugomea chombo hicho cha usafiri  pale watakapoona hakina vigezo vya kusafirisha abiria  pia watakuwa na ufahamu wa kutosha juu ya nauli stahiki wanazostahili kulipia ambazo pia  zimeidhinishwa na SUMATRA.

Haki za abiria safarini;
Akifafanua baadhi ya haki za msingi kisheria kwa watumiaji vyombo vya barabarani kwa mujibu wa mamlaka hiyo, Michael anasema;

Abiria ana haki ya  kurudishiwa nauli yake chombo cha usafiri kinapochelewa kuanza safari saa mbili baada ya muda uliopangwa kwenye ratiba na tiketi (kanuni No.21-(2)),  pia ana haki ya kupewa tiketi  ndani ya ofisi ya  mtoa huduma ya usafiri husika na siyo  vinginevyo (kanuni ya  17- (1p ) na ya 24–(1 ).

Anataja haki nyingine kuwa ni kutonyanyaswa au kutumia lugha  za matusi au vitendo vyovyote kinyume na taratibu au kwa mujibu wa haki za binaadamu iwe kwa abiria  mtu mzima au mwanafunzi kama kanuni ya 18-(1a,g,h ).

 Haki nyingine ni ya kufikishwa mwisho wa safari yaani kituo husika anakoelekea abiria (kanuni ya 18-(1d), haki ya kutosimamishwa ndani ya chombo cha usafiri hasa kwa mabasi ya mikoani   awapo  safarini  (kanuni 17- 1f) ), Haki  ya kulipa nauli   iliyoidhinishwa  na mamlaka  ya  SUMATRA na  si zaidi  ya  kiwango husika   (kanuni ya 34-1, 2, 3) ).

Haki ya  kutoendeshwa na dereva mmoja (kwa mabasi ya mikoani ) zaidi  ya saa nane (kanuni ya 17-1g), kulindwa kwa mikanda ya usalama  (Passengers seat belt ) wakati wote wa  safari (kanuni ya 17-1i ), kupata huduma muhimu  za usafiri, afya na taarifa  zinazohusiana na safari yake (kanuni ya 17- 11,m,n).

Pia anaongeza kuwa abiria ana haki ya kurudishiwa nauli pungufu ya 15% tu ya kiasi alicholipa kama ilivyoainishwa  kwenye  tiketi endapo abiria atavunja  safari ndani ya muda chini ya saa 24  kabla ya muda wa chombo cha usafiri kuanza safari (kanuni ya 24-3).

Wafanyakazi katika  gari la abiria wanakatazwa nini;
Michael anaeleza kuwa kanuni ya 18 ya sheria za SUMATRA [GN] NO.218/2007 inaelezea wafanyakazi katika gari la abiria wakiwa kazini wanakatazwa kutofanya mambo yafuatayo;

Kutumia lugha  chafu  ya  uhasama  kwa abiria, kuwaziba  au kuwazuia  kwa makusudi wahudumiaji wenyewe wa usafiri,
kuendesha  gari zaidi ya vikomo vya spidi kwa kushindania  abiria au kukatisha safari kabla ya  kufika  kituo cha mwisho.

Mfanyakazi au dereva wa gari haruhusiwi  kuendesha  gari  la abiria akiwa amekunywa pombe au kutumia madawa ya kulenya kiasi chochote kile pia haruhusiwi  kuendesha gari la abiria kwa uzembe au namna ya hatari au kinyume na sheria ya usalama  barabarani au sheria nyinginezo.

Aidha haruhusiwi kubughudhi au kusumbua abiria kwa namna yoyote ile hata kama ni mwanafunzi, kuendesha gari la abiria hali dereva anazungumza na simu za kiganjani  na kupakia wanyama hai au vitu vya hatari kwenye gari la abiria.

Aidha Michael anabainisha kuwa mmiliki wa leseni ya gari la abiria au mtumishi wake ambaye atavunja au kushindwa kutekeleza kanuni ndogo  ya [1] atakuwa anatenda kosa  la jinai na  anapaswa, kutiwa  hatiani, kutozwa faini isiyo chini ya laki tano, au kufungwa jela  kwa muda usiyopunguwa mwaka  1  na usiozidi miaka miwili au vitu kwa pamoja.

Gari la abiria likiharibika njiani abiria afanye nini;
Michael anaeleza kuwa Kanuni ya 22 ya sheria za SUMATRA [GH] No. 218/2007 inayohusu kuharibika kwa gari la abiria inasema ikiwa gari la abiria litaharibika au haliko katika  hali ya  kuanza au kuendelea na safari, mmiliki wa leseni ya gari au mfanyakazi wake lazima atafute mbadala wa usafiri ndani ya dakika 10 au arudishe nauli.

Anaongeza kuwa gari likiharibika linatakiwa kuondolewa barabarani na kama gari hilo linatoa huduma ndani ya mji na mji basi litengenezwe ndani ya muda usiozidi masaa.

Ikiwa  baada ya matengenezo ya gari la abiria kwa mujibu wa kanuni ndogo ya 1[b] gari hilo bado  haliko katika hali ya kuanza au kuendelea  na safari, mmiliki wa leseni au mfanyakazi lazima atoe usafiri mbadala.

Haki ya kulipia Mzigo.
Michael anaeleza kuwa kanuni ya 23 ya sheria  za SUMATRA [GN] No. 218/2007 inasema abiria  ana haki kubeba mzigo wenye uzito wa kilo 20 na mtoto mzigo wenye uzito wa kilo 10 bila malipo ila akibeba mzigo zaidi ya ule unaoruhusiwa kubebwa bila malipo mmiliki wa leseni ya gari la abiria ana haki ya kumtoza kwa kilo ya ziada kwa mujibu wa viwango vilivyoruhusiwa.

Haki ya Kufuta oda ya safari na Kurudishiwa Nauli.
Michael anasema Kanuni ya 24 ya sheria  za SUMATRA [GN] No 218/2007 inatoa haki kwa abiria kufuta oda yake ya safari ndani ya masaa 24  au zaidi kabla ya muda wa kuanza safari ya gari la abiria na kurudishiwa nauli yake.

Abiria  ana  haki ya kurudishiwa nauli baada  ya kukatwa asilimia 15  ya nauli hiyo endapo oda ya safari itafutwa ndani ya muda  unaopungua masaa 24 kabla ya muda uliopangwa.

Haki ya Kupewa Tiketi.
Michael anabainisha kuwa Kanuni ya 25 ya sheria  za SUMATRA [GN] No.218/2007 inazungumzia haki ya abiria kupewa tiketi yenye jina lake  pamoja na namba ya kiti chake na haki ya kufahamu muda wa kuwasili kituoni na kuanza safari.

Abiria  pia ana haki ya kufahamu  kituo aendacho, tarehe ya  kutolewa tiketi na tarehe ya safari, kufahamu  namba  ya usajili wa  gari hilo la abiria, kufahamu  nauli ya safari hiyo, kufahamu jina la njia  ihudumiwayo, na kufahamu anuani  na namba ya simu  ya mmiliki wa leseni ya gari hilo.

 ‘Kwa huduma za usafiri ndani ya mji, mmiliki wa gari la abiria atatoa tiketi zilizochapishwa ambazo zinaonesha namba  ya usajili wa gari lenye leseni, njia, nauli iliyoidhinishwa, jina na anuani ya gari au mmiliki wake  na tarehe ya kutolewa’, aliongeza.

Nauli za Watoto na Wanafunzi.
Anafafanua kuwa Kanuni ya 26 ya  sheri za SUMATRA [GN] No.218/2007 inabainisha kuwa kila mtoto na mwanafunzi atakayepanda gari la abiria atakua na haki ya kusafiri kwa kulipa nusu ya nauli  anayotozwa mtu mzima kwa safari hiyo hiyo.

‘PROSPER PROJECT’ APPLAUDED FOR A GOOD JOB


 

SIKONGE district council Chairman, Robert Kamoga, has extended his congratulations toward the efforts made by the Eliminating Child Labour in Tobacco Growing Foundation (ECLT) by financing the PROSPER Project which is implemented by Winrock International, TAWLAE and TDFT) in Urambo and Sikonge Districts in Tabora region focusing on combating  child labour in tobacco growing districts of Tanzania.

Speaking during the event held at Udongo village in Sikonge districtin Tabora region to mark the ‘World Day Against Child Labour’ on 12 June 2014, Mr. Robert Kamoga said, he felt highly   privileged to have such endeavors to address incidences of child labor in his district and he is very proud of recorded achievements by the project in his district.

He clarified that the project has accelerated efforts to address child labour in the region through prevention and withdrawal of more than 4590 children from hazardous forms of child labor in agriculture and precisely in tobacco growing.

Apart from creating awareness to the entire community on the importance of education to children and on theadverse effects of child labour, Kamoga said the project has also improved social services such as construction of water wells and improvement of learning and teaching
environment through rehabilitation of classrooms, provision of text books, desks and construction of latrines.

Not only that, the project has also provided conditional loans ranging from Tshs100, 000 to Tshs 200, 000 to more than 983 women entrepreneurs aiming at starting or boosting their small businesses as a gear to empower them economically hence enable them to provide their children with school learning materials as well as meeting house hold needs such as food and clothing, he said.

‘The two districts have more than 200 villages, out of these only 20 villages 10 from each district have benefited from the project, it’s my sincere request to PROSPER project and their donor  to extend their help and services to other villages for the betterment of our children’, he said.

As a matter of assuming responsibility, Kamoga said the government should not rely on donors for everything. ‘We should play our part by setting our strategies’, the issue of providing basic social services to our people has to be done by the government, while donors can take
part on big issues only, he added.

PROSPER project director from Winrock, Bahati Nzunda said the project is funded by the ELCT Foundation aiming to protect children aged between 5-17 from child labour involvement in tobacco growing areas, which is implemented in Urambo and Sikonge districts only in Tabora region.

He said the maximum support from government, implementing partners  (TAWLAE and TDFT), community,the tobacco sector itself, and other stakeholders has paved a way for the project to perform successfully.

Christopher Luyenga, Project Community Outreach Coordinator, noted that the project has set to maximize the means of access to education to all vulnerable children from poor families for the targeted areas within the two districts as a strategy  to ‘extend social protection and combat child labour’. He emphasized that the project is aiming at combatting of all forms of child labor as stipulated in the ILO Convention 182.

PROSPER Project’s interventions entirely focus on combatting child labor by providing proper responses such as access to quality education through improvement of the learning and teaching environment and addressing poverty by improving the livelihoods of women and youth.

This project supports the Government at District and National levels so that there is a strong national commitment and all agricultural sectors join efforts against child labour.

According to a public statement on occasion of the World Day Against Child Labour from the ECLT Executive Director, Sonia Velazquez, “ECLT joins in the WDACL 2014 featured theme: ‘Extend Social Protection; Combat Child Labour’ which spells out the critical role of universalization of social protection and the fulfillment of ILO minimum standards of social security in the fight against child labour”.

She said child labour results from various multifaceted factors such as poverty and lack of quality education, that’s why each year the International Labour Organization draws attention to a specific angle of child labour and the policies and actions that can make a difference in eliminating it.

Founded in 2001, ECLT is a global leader in preventing and addressing child labour in tobacco agriculture with the primary purpose of protecting and improving the lives of children and eliminating child labour in tobacco-growing.

ECLT is a partnership between farmers - represented through the International Tobacco Growers’ Association (ITGA) and the major multi-national tobacco companies, advised by the International Labour Organization (ILO) and Save the Children Switzerland, dedicated to protecting children from child labour wherever tobacco is grown.

ECLT has supported key child labour elimination programmes in Tanzania since 2004. Specifically, through the efforts of our implementing partners ILO-IPEC and Winrock International, to build partnerships with local stakeholders, including government, tobacco companies and the tobacco farmers, to implement area based approaches to combat child labour within the Urambo and Sikonge districts of Tanzania, and contribute to the National Action Plan.
 
PROSPER project complements the activities of the local tobacco companies in fighting child labour, their activities include training farmers on the hazards of child labour and other work abuse, monitoring them, helping them increase their yields, researching ways to reduce labour.

"WAISLAMU TABORA KUMBURUZA MAHAKAMANI SHEIKH MKUU WA TANZANIA"



Katika hali ambayo haikutarajiwa na wengi,baadhi ya waislamu Tabora kwa kushirikiana na viongozi wa Msikiti mkuu wa Ijumaa Tabora mjini wamekusudia kumfikisha mahakamani Sheikh mkuu wa Tanzania Mufti Shaaban Simba kufuatia mgogoro uliopo baina ya viongozi wa msikiti huo na baraza kuu la Waislam Tanzania Bakwata ambao umesababisha mgawanyiko wa waislamu wa mkoani Tabora.

Taarifa zilizotufikia zimeeleza kuwa tayari taratibu za mahakamani zimekwishafanyika katika kufungua mashtaka dhidi ya kiongozi huyo mkubwa wa dini ya kiislamu hapa nchini na kwamba wakati wowote kuanzia sasa atafikishwa katika mahakama kuu kanda ya Tabora kukabiliana na shitaka lake ambalo inadaiwa limemuunganisha yeye(Mufti),Bakwata na Katibu mkuu wa Bakwata.

Aidha ikumbukwe kwamba katika siku za hivi karibuni Sheikh mkuu wa Tanzania Mufti Shaaban Simba aliwasimamisha madaraka viongozi wa msikiti mkuu wa ijumaa na kumvua wadhifa wake Sheikh wa mkoa wa Tabora Shaaban Salum jambo ambalo lilipingwa na idadi kubwa ya waumini wa dini ya kiislamu na hivyo kusababisha   kuwa chanzo cha vurugu katika msikiti mkuu wa Ijumaa Gongoni Tabora mjini.

Katika muendelezo wa mgawanyiko na mgogoro huo wa waislamu Tabora mjini ambao ukielezwa kuwa ni wa kwanza kutokea ndani ya miaka zaidi ya 80 iliyopita ambapo Sheikh mkuu wa Tanzania Mufti Shaaban Simba alimteua Sheikh Ibrahim Mavumbi kuwa Sheikh wa mkoa katika kipindi cha miezi Sita hadi hapo uchaguzi utakapofanyika hatua ambayo pia iliendelea kuleta mzozo  mkubwa hata kufikia hatua kwa baadhi ya waumini kupinga kuongoza ibada kwa Sheikh mteule katika msikiti mkuu wa Ijumaa Gongoni na hivyo kusababisha aliyekuwa Sheikh mkuu Shaaban Salumu kukamatwa na Polisi na hatimaye kufikishwa mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa Tabora akituhumiwa kwa kosa la kutaka kuleta fujo eneo la kuongozea Ibada msikiti mkuu wa Ijumaa Gongoni akiwa na wafuasi wengine watano.

Hata hivyo hali hii bado imeendelea kuzua mashaka makubwa kutokana na kuwepo kwa tetesi kwamba wapo baadhi ya viongozi wa Serikali na wanasiasa wamesimama nyuma ya pazia la Mgogoro huo unaoendelea kuwagawa waislamu ingawa hadi sasa hakuna kiongozi yeyote wa Serikali aliyejipambanua kuwa anashiriki katika vuguvugu la sakata hilo la waislamu lililoingia katika sura mpya ya mgongano wa maslahi binafsi kwa baadhi ya kikundi cha watu.  

ZAIDI YA ROBO TATU YA WANAKIJIJI WARUDISHA KADI ZA CHADEMA,WAJIUNGA NA CCM-NZEGA


Katibu wa Itikadi,Siasa na Uenezi CCM mkoa wa Tabora Bw.Idd Kapama akiangalia kadi zilizorejeshwa na  waliokuwa wanachama wa Chadema katika Kijiji cha Ugembe 2 kata ya Mwakashahala wilayani Nzega ambapo zaidi ya robo tatu ya wakazi wa Kijiji hicho walirudisha kadi wakidai kuchoshwa na Porojo za baadhi ya viongozi wa Chadema ambao wamekuwa wakifika mara chache na kutoa ahadi hewa za matumaini. 
Wakati wanakijiji wa Ugembe wakichangamkia kurejesha Kadi za Chadema baada ya kukosa matumaini
Katibu wa CCM wilaya ya Nzega Bw.Kajoro akisoma majina ya wanachama wapya wa CCM huku Katibu wa CCM mkoa wa Tabora Bw.Idd Ali Ame akigawa kadi kwa wanachama hao waliohama kutoka Chadema katika mkutano wa hadhara uliofanyika kijiji cha Ugembe
Wanachama wapya wa CCM wakifanya kiapo cha kujiunga na chama hicho.
Katibu wa CCM Bw.Kajoro akisoma kanuni za mwanachama wa CCM ikiwa ni ishara ya kiapo cha uanachama baada ya kujiunga na chama hicho.
Mwanachama mpya wa CCM akiisoma vizuri kadi yake baada ya kupatiwa na Katibu wa CCM mkoa wa Tabora Bw.Idd Ali Ame. 
Katibu wa CCM mkoa wa Tabora Bw.Idd Ame akizungumza na wananchi katika Kjiji cha Ugembe wilayani Nzega ambapo pamoja na mambo mengine Bw.Ame alisisitiza msimamo wa Chama cha Mapinduzi kuhusu Katiba mpya juu ya umuhimu wa Serikali mbili  zilizoboreshwa kama msingi imara utakaosaidia kuondoa kero wa wananchi.
Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Nzega Bw.Amos Kanuda akizungumza na wakazi wa Kijiji cha Ugembe 2 ambapo aliwataka kuendelea kukiamini CCM kwa madai kuwa ndio chama pekee chenye muelekeo wa kuleta maendeleo.

Tuesday, June 17, 2014

MGOGORO WA WAISLAMU TABORA:-ALIYEKUWA SHEIKH MKUU AFIKISHWA MAHAKAMANI,AACHIWA KWA DHAMANA

NA LUCAS RAPHAEL,TABORA.

 
Shehkh wa mkoa wa Tabora Salum Shaban Salum  na waumini wenzake wa dini ya kiislam watano wamefikishwa mahakama ya hakimu mkazi mfawidhi wa mkoa wakikabiliwa na shitaka la kutishia kufanya fujo.
 
Mbele ya hakimu mkazi mfawidhi wa mkoa wa Tabora Issa Magoli ilidaiwa na wakili wa serikali Juliana Changalawe kuwa watuhumiwa kwa pamoja walitenda kosa hilo tarehe 14/06/2014 katika msikiti mkuu wa mkoa uliopo eneo la Gongoni mjini hapa.
 
Wakili huyo aliiambia mahakama kuwa siku hiyo majira ya mchana watuhumiwa Shaban Salum, Mgude Ahmed, Said Maganga, Kassim Shomary, Abubbakar Ludenga na Kassim Rajab walimtoa sehemu ya ibada  Shehkh Ibrahim Mavumbi.
 
Watuhumiwa ambao wanawakilishwa na wakili msomi Mussa Kwikima wa miji hapa mara baada ya kusomewa shitaka hilo waote walikana na kesi hiyo imeahirishwa hadi tarehe 30/06  kwa ajili ya kuanza kusikilizwa kwani upelelezi umeisha kamilika na wote walipata dhamana.
 
Kukamatwa hadi kufikishwa mahakamani kwa shehkh huyo na wenzake kunafuatia mgogolo ambao umekuwa  ukiendelea na kupelekea Mufti wa Tanzaniia  Shaban Simba kutangaza kumuengua shehkh wa mkoa wa Tabora
Shaban Salum kitendo ambacho kinapingwa na baadhi ya waislamu.
 
Katika mgogolo huo baadhi ya waislamu wanapinga uhamzi huo ambapo Mufti alimtangaza shehkh Mavumbi Ally kuwa kaimu shehk wa mkoa wakati kwenye uchaguzi alishindwa .
 
Hata hivyo habari kutoka ndani ya waumini wa dini ya kiislam mkoani hapa wanadai kuwa mgogolo huo unachochewa na viongozi wa serikali ambao wanalazimisha shehk mavumbi ndiye awe kiongozi wa mkoa wa dini hiyo.
 

Aliyekuwa Sheikh mkuu wa mkoa wa Tabora Sheikh Shaaban Salumu(aliyevaa shati jeusi) wakati alipokuwa barabarani akisindikizwa na waumini wa dini ya kiislamu baada ya kuachiwa kwa dhamana katika mahakama ya hakimu mkazi Tabora akituhumiwa kwa kosa la kutaka kuleta fujo msikiti mkuu wa Ijumaa Gongoni mjini Tabora  akiwa na waumini wengine watano.
Sheikh Shaaban Salum akiwa na baadhi ya waumini waliounganishwa naye katika kesi moja mahakama ya hakimu mkazi Tabora mjini.

HAKIKISHENI TUNAKUWA NA CHAKULA CHA KUTOSHA DKT. BILAL AWAAMBIA G77+CHINA


SA 3
…………………………………………………………………………..
 
 
 
Na Mwandishi Maalum, Santa Cruz, Bolivia
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal amezitaka nchi wanachama wa G77+China, kuhakikisha zinaboresha kilimo ili ziwe na hifadhi ya kutosha ya chakula kwa wananchi wake. 
 
Akihutubia mkutano wa mwaka kwa nchi za G77+China ambao pia ni kilele cha maadhimisho ya miaka 50 ya umoja wa nchi hizi, unaofanyika jijini St Cruz De Sierra, Dkt Bilal alisema nchi za umoja huu zina maeneo mazuri kwa kilimo na hivyo ni muhimu kuyatumia maeneo haya katika kuzalisha chakula kwa lengo la kuhifadhi na kuwa na usalama wa chakula nyakati zote.
 
Dkt. Bilal alisema, nchi hizi kwa pamoja zinahitaji kuwa na kauli moja kuhusu masharti yanayowekwa na nchi kubwa hasa katika kilimo na kuelezea kuwa ili mafaniio makubwa yapatikane, lazima uwepo uwekezaji wa ndani katika kilimo sambamba na serikali za nchi hizi kuchangia shughuli za uzalishaji ili kuwa na kilimo chenye tija kwa wakulima na kinachoweza kuchangia usalama wa chakula.
 
Kuhusu suala la mazingira, Mheshimiwa Makamu wa Rais aliwaeleza wajumbe wa G77+China kuwa, maazimio yaliyofikiwa Rio+20 na mapendekezo kuhusu ‘Kesho tunayoitaka’ yanazihitaji nchi hizi kupaza sauti zake kwa pamoja kuhusu kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi kwani suala hili kwa sasa haliwezi kutatuliwa na nchi moja bali linahitaji nguvu ya kila mtu duniani.
 
Makamu wa Rais alifafanua kuwa bila kuwa na mazingira bora maendeleo endelevu yatabakia ndoto na pia kufanikisha Malengo ya Milenia kwa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa itakuwa vigumu kama suala la mazingira litaachwa kwa kila nchi kufanya inavyotaka.
 
“Kundi hili lina kazi kubwa iliyo mbele yetu na hasa kuhusu malengo mapya ya maendeleo baada ya kukamilika kwa muda wa Malengo ya Milenia mwakani. Tunahitajika kubuni njia za kuzipatia nchi zetu maendeleo katika Nyanja za uchumi, kijamii na mazingira ili tufanikiwe vema,” alisema Mheshimiwa Makamu wa Rais.
 
Katika hotuba hiyo Mheshimiwa Makamu wa Rais pia alizungumzia kuhusu umuhimu wa nchi hizi kuweka msisitizo wa kuwapa wananchi maji safi na salama, umuhimu wa kuwa na nishati inayotosheleza matumizi ya uzalishaji, uwepo wa huduma bora za afya na elimu ili kupiga hatua kwa haraka baina ya wananchi wa nchi hizi. “Nafahamu kufanikisha haya yote ni kazi kubwa lakini hatuna muda wa kusubiri. Ni lazima tufanye kazi ili kubadili hali iliyopo,”alifafanua.
 
Mkutano huo ambao umekamilika jana kwa mwenyeji wake Rais Evo Morales kuwashukuru wanachama wa G77+China walioweza kushiriki mkutano huo, pia ulionesha nia kwa wanachama wa nchi hizi kutafuta majibu ya changamoto ya ukosefu wa ajira unaokabili wananchi wengi wa nchi hizi. Viongozi wengi walisisitiza kuwa, suala la ajira hasa kwa vijana linatakiwa kutazamwa upya na hasa ukizingatia rasilimali zilizopo katika nchi za G77+China ili zitumike katia kutengeneza ajira mpya zitakazoweeza kusaidia kuboresha maisha ya watu wa nchi hizi kwa miaka mingi ijayo.

UDA YASISITIZA NIA YAKE YA KUBORESHA USAFIRI DAR ES SALAAM



Na Mwandishi Wetu,
KAMPUNI ya Simon Group Limited imesisitiza dhamira yake ya kuboresha sekta ya usafiri katika Jiji la Dar es Salaam licha ya kampeni zinazoendelea kutoka kwa washindani binafsi ikiwa na lengo la kuvuruga mpango unaoendelea wa uwezekezaji katika Shirika la Usafiri Dar es Salaam (UDA) ili waweze kuitawala biashara ya usafiri.

Kwa mujibu wa taarifa ya UDA, mpango unaendelea wa kuifanya Dar es Salaam liwe jiji lenye urahisi katika usafiri kwa kufanya kazi kwa karibu na Serikali na Jiji.

“Tumeona taarifa ambazo zimekuwa zikichapishwa katika vyombo mbalimbali vya habari ikiwamo mitandao ya kijamii kutoka katika kundi linalojiita Consortium of Concerned Tanzanians International wakijaribu kuwafanya watu waamini kila uwekezaji unaofanywa katika kuboresha mfumo wa usafiri jijini Dar es Salaam kupitia UDA hauna maana.

“Hili ni hatua inayosikitisha sana, tunajaribu kuuboresha mfumo wa usafiri Dar es Salaam kutoka katika msongamano ili kuwa katika hali inayoridhisha kwa kuongeza idadi ya magari na kuboresha huduma za usafirishaji lakini watu wengine wanatumia muda mwingi kufanya kampeni zenye lengo la kuhakikisha malengo hayo hayatimii,’’ ilisema taarifa hiyo kutoka kwa mwenyekiti ambaye pia ndiye Ofisa Mtendaji Mkuu, Robert Kisena.

Aliitaja kampeni hiyo iliyopewa jina la “Kampeni ya Kurudisha Shirika la Usafiri Dar es Salaam (UDA) Mikononi mwa wananchi” inajaribu kuligeuza mtaji suala la kujivunia umiliki wa kampuni hiyo kwa umma bila ya kuangalia ni vipi kampuni inaweza kusimamiwa kwa namna bora na kufanikiwa kutimiza malengo ya kurahisisha usafiri Dar es Salaam.

Alisema kwamba kampuni yake iliamua kuwekeza UDA baada ya kutangazwa kubinafsishwa kwake kwa sababu kampuni ya Simon Group Limited ilitaka kuleta mabadiliko yenye maana katika mfumo wa usafiri katika Jiji la Biashara la Dar es Salaam hasa katika mabasi ya abiria na usafirishaji kwa ujumla.

“Mpango wa kuboresha usafiri umeelezwa vizuri katika mipango yetu ya muda mfupi na muda mrefu inayoonyesha ni jinsi gani tuna mpango wa kusimamia mabadiliko haya hatua kwa hatua. Katika mpango wetu pia tumebainisha ni vipi tunajipanga kuihusisha Serikali na Jiji katika mpango mzima wa usafiri Dar es Salaam. Naamini hii ndio maana hasa ya uzalendo, kufanya kazi na serikali yako ili kutoa huduma bora kwa wananchi wake,’’ alieleza Kisena katika taarifa hiyo.

Katika taarifa hiyo ofisa huyo mtendaji mkuu alibainisha kwamba mpango walioudhamiria wa kampuni hiyo kuboresha huduma ya usafiri Dar es Salaam uko pale pale ukihusisha mradi wa kuwa na mabasi zaidi ya 3,000 pamoja na mabasi mengine ya kifahari 50 yenye viyoyozi na huduma ya internet.

Alisema kwamba sambamba na mpango huo, kampuni itasimamia sera ya kuwaajiri wataalamu wazawa badala ya kuwapa wataalamu wa kigeni kazi ambazo Watanzania wanazimudu.

“Kampuni ya Simon Group Limited inamilikiwa na Watanzania, katika hilo nitakuwa mtu wa mwisho kumkubali mtaalamu wa kigeni kuajiriwa  katika nafasi ambayo inaweza kushikwa na Watanzania wenzangu. Kama hatutopata mtaalamu Mtanzania, tutaleta wataalamu wa kuwapa mafunzo Watanzania ili baadaye wazichukue nafasi hizo. Kampuni yetu inalifanya hilo kama njia mojawapo ya kuwawezesha wazawa kiuchumi na kuwapa utaalamu.

Alisema kwamba tathmini inaonyesha kuwa ili kuwezesha mabasi yapatayo 3000 kufanya kazi hapo baadaye wataalamu wapatao 7800 watahitaji kupewa mafunzo na kuajiriwa.

Aliongeza kwamba mara baada ya mpango huo kukamilika, unyanyapaa miongoni mwa wanajamii kuhusu utumiaji wa mabasi ya uma hautokuwepo tena na watu wataacha kupaki magari yao katikati ya jiji, watanunua tiketi za UDA kwa njia ya mtandao jambo ambalo litapunguza msongamano Dar es Salaam.

“Ninataka kuwahakikishia Watanzania wote na wale wanaoendelea na kampeni zao kwamba mpango wa UDA kuboresha mfumo wa usafiri Dar es Salaam ni jambo linalowezekana, Tutafanya kazi kwa karibu na Serikali pamoja na Jiji ili kuona wakazi wa Dar es Salaam wanapata huduma rahisi na ya uhakika ya usafiri,’’ alisema