Saturday, February 14, 2015

TABORA WAZINDUA MPANGO MKAKATI WA KUPUNGUZA VIFO VYA MAMA WAJAWAZITO NA WATOTO WACHANGA





Mkuu wa mkoa wa Tabora Bw.Ludovick Mwananzila akizindua Mpango mkakati wa kupunguza vifo vya akina mama wajawazito na watoto wachanga,uzinduzi uliofanyika katika Ukumbi wa Isike Mwanakiyungi ofisi ya mkuu wa mkoa wa Tabora ambao umehudhuriwa na wadau mbalimbali wa afya.

Baada ya kuzinduliwa mpango mkakati huo,wakuu wa wilaya za mkoa wa Tabora walipatiwa kwa ajili ya kusimamia utekelezaji,Mkuu wa mkoa wa Tabora Bw.Mwananzila akimkabidhi mkuu wa wilaya ya Sikonge Bi.Hanifa Selengu.
Mkuu wa mkoa wa Tabora Bw.Mwananzila akimkabidhi mpango mkakati huo mkuu wa wilaya ya Nzega Bituni Msangi
Mkuu wa mkoa wa Tabora Bw.Mwananzila akimkabidhi mpango mkakati huo unaolenga kuimarisha afya za akinamama wajawazito na watoto wachanga na kupunguza vifo.
Meya wa halmashauri ya Manispaa ya Tabora Bw.Ghulam Dewji akipokea mpango mkakati huo kwa niaba ya mkuu wa wilaya ya Tabora kutoka kwa mkuu wa mkoa wa Tabora Bw.Mwananzila.
Mganga mkuu mkoa wa Tabora Dr.Gunini Kamba akitoa maelezo mafupi kuhusu changamoto za huduma ya afya zinazoukabili mkoa wa Tabora na namna ambavyo mpango mkakati huo utakavyosaidia kuboresha huduma za afya kwa kupunguza vifo vya akinamama wajawazito  na watoto wachanga.
Mkuu wa mkoa wa Tabora Bw.Ludovick Mwananzila akifungua mkutano wa uzinduzi wa mpango mkakati huo wa kupunguza vifo vya akinamama wajawazito na watoto wachanga.
Baadhi ya wadau wa Afya kutoka sekta mbalimbali waliohudhuria katika mkutano huo wa uzinduzi wa mpango mkakati wa kupunguza vifo vya watoto wachanga na kinamama wajawazito.


 
NA LUCAS RAPHAEL,TABORA

MKUU wa Mkoa wa Tabora Ludovick Mwananzila ameonya vikali waganga wakuu wa wilaya na waratibu  wa huduma ya Afya ya mama na mtoto wanaoshindwa kutekeleza wajibu wao ipasavyo hali inayosababisha kuendelea kuongezeka kwa vifo vya akina mama wajawazito na watoto wachanga mkoani humo.

Mkuu huyo wa mkoa alitoa onyo hilo katika mkutano wa uzinduzi wa mkakati wa kupunguza vifo vya wajawazito na watoto uliofanyika jana katika ukumbi wa Mtemi Isike Mwanakiyungi mjini Tabora
uliohudhuriwa na wadau mbalimbali wa afya kutoka wilaya zote za mkoa huo, taasisi, mashirika na waandishi wa habari.

Alisema takwimu za idadi ya akinamama wajawazito na watoto wanaofariki kwa kukosa huduma au kutohudumiwa kwa wakati inazidi kuongezeka mkoani Tabora na vifo vingine vinavyotokea hata wataalamu
wa afya hawana taarifa, jambo hili sio zuri, lingeweza kuthibitiwa na watoa huduma katika vituo vya afya.

Alisema hakuna sababu ya mama mjamzito kupoteza maisha anapojifungua au mtoto wake kufariki
 kisa amekosa huduma wakati uwezekano wa kujifungua salama upo, rasilimali chache zilizopo zinaweza kutumika kuokoa maisha ya mama na mtoto wake kama watoa huduma watafanya kazi yao ipasavyo.

‘Kuanzia leo waganga wakuu wa wilaya (DMO’s) ni lazima mtoe taarifa za kifo chochote cha mama
mjamzito kitakachotokea katika kituo chako na utoe sababu kwa nini kimetokea ili mhusika aliyezembea achukuliwe hatua mara moja’, alisema.

Mwananzila aliwapongeza madaktari wote wanaotoa huduma za uzazi katika mradi wa Millenium ulioko
 katika vijiji 16 mkoani humo ambapo taarifa za utendaji zinaonyesha kwamba katika kipindi cha mwakamzima hakuna kifo hata kimoja cha mama mjamzito kilichotokea katika vijiji hivyo.

‘Nawapongeza madakatri na watoa huduma wote walioko katika mradi huu, mmekuwa mfano wa kuigwa,wataalamu wa afya katika kila halmashauri acheni kufanya kazi kwa mazoea, tumieni rasilimali zilizopo ipasavyo, alionya Mwananzila .
 
Mkuu wa mkoa aliwataka wakurunguzi , wakuu wa wilaya , waganga wa wilaya , waratibu wa afya ya uzazi,  makatibu Tawala wa wilaya na ,madiwani, watendaji, madaktari na wauguzi wote kusimamia zoezi hiloipasavyo  katika maeneo yao ili kuepusha vifo vyote vitokanavyo na uzazi.

Aidha aliagiza halmashauri zote kuweka utaratibu mzuri wa kuwapokea wataalamu wapya wa afya na
kada nyinginezo wanaopelekwa katika halmashauri hizo ili wafurahie mazingira ya kazi na waweze kuwa msaada mkubwa katika maeneo hayo.

Kuondoka kwa wataalamu wengi katika halmashauri nyingi kunachangiwa na halmashauri zenyewe kutoandaa
mazingira mazuri ya kuwapokea wataalamu wapya wanaoletwa na serikali.

Akitoa neno la shukrani Mratibu wa Huduma ya Uzazi kwa mama na mtoto Kanda ya Magharibi .
Martha Mlimba aliwataka waganga wakuu, waratibu wa afya na watoa huduma ya uzazi kwa mama na mtoto katika kila halmashauri kuzingatia agizo la RC katika utendaji kazi wao ili kupunguza vifo hivyo.

 
mwisho



Friday, February 6, 2015

MKUTANO MKUU WA SABA WA CHAMA CHA MAJAJI WANAWAKE TANZANIA(TAWJA) WAFANYIKA JIJINI DAR


 
 Jaji Fredrick Wambali akitoa mada katika mkutano huo.
 Wanachama wa Chama cha Majaji Wanawake Tanzania (TAWJA), wakiwa kwenye mkutano wao mkuu uliofanyika Dar es Salaam jana. Mkutano huo ulihudhuriwa na wanachama kutoka mikoa yote.
Wanachama wa Chama cha Majaji Wanawake Tanzania (TAWJA), wakiwa kwenye mkutano wao mkuu uliofanyika Dar es Salaam jana. Mkutano huo ulihudhuriwa na wanachama kutoka mikoa yote.

Dotto Mwaibale
JAJI Mkuu Mohamed Chande, amewataka wanawake nchini kutoa taarifa katika ngazi husika pindi  wanapoombwa rushwa ya ngono ili sheria ifuate mkondo wake.

Akizungumza wakati wa Ufunguzi wa Mkutano wa saba wa Chama cha Majaji Wanawake Tanzania (TAWJA), alisema kunaidadi kubwa ya wanawake ndani ya jamii wanaoombwa rushwa ya ngono lakini wamekuwa wahoga kutoa taarifa.

"Katika rushwa ya ngono lazima sheria mahususi zichukuliwe,hivyo tunawasihi wanawake baada ya kufanyiwa matukio hayo wafikishe malalamiko mahakamani au sehemu husika na sheria itafuatwa," alisema Jaji Chande.

Kadhalika, serikali itaendelea kuboresha mazingira ya majaji wanawake ili kukabiliana na mabadiliko yanayoendelea ndani ya mahakama katika ngazi zote.

Mwenyekiti wa TAWJA, Engera Kileo, alifafanua katika kesi za rushwa ya ngono mahakama kupitia kifungu cha 25,muhusika atakayebainika kujihusisha na kitendo hicho atatozwa faini au adhabu ya kifungo cha miaka 30.

"Mahakama imeweka adhabu hiyo kutokana na ongezeko la matukio  kufanyika ndani ya jamii na wanawake kujengewa woga wa kutoa taarifa kwa wakati, hivyo tunachokifanya kuangalia namna ya kuongeza adhabu kwasababu ngono imetawala katika sekta mbalimbali," alisema Kileo.

Lakini kwa sasa  chama hicho kinatoa elimu juu ya rushwa ya ngono katika jamii na matumizi mabaya ya ngono zembe ili kuwalinda na magonjwa ya kuambukizwa kama Maambukizi ya Ukimwi(VVu), na yale ya zinaa. (Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za jamii.com)

ASKARI POLISI ALIYEULIWA KIKATILI MKOANI DODOMA AAGWA LEO, MUUAJI NAYE AULIWA NA WANANCHI

Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) Ernest Mangu akiongoza jana waombolezaji katika kutoa heshima za mwisho kwa Askari  Namba G. 7168 PC JOSEPH ISACK SWAI aliyeuwawa huko Chango’ombe ya juu Mkoani Dodoma na mtu aliyefamika kwa jina la TISSI SIRIL MALYA.
Wasifu wa marehemu ukisomwa 
Maombolezo wakati wa shughuli ya kuaga mwili wa askari huyo shujaa

Na Sylvester Onesmo wa  Jeshi la Polisi Dodoma. 
 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Kama Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa Polisi DAVID MISIME – SACP amesema kama alivyotoa taarifa jana tarehe 04/02/2015 kuhusiana na kuawa kwa Askari  Namba G. 7168 PC JOSEPH ISACK SWAI huko Chango’ombe ya juu Mkoani Dodoma na mtu aliyefamika kwa jina la TISSI S/O SIRIL MALYA.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Dododoma lilianza msako wa kumtafuta mtuhumiwa huyo baada ya kufanya kitendo hicho cha kinyama cha kumkata kata kwa panga kichwani na mikononi Askari huyo.

Kamanda MISIME amesema majira ya saa 23:00hrs usiku wananchi walimuona maeneo ya Mti Mkavu Mailimbili Mkoani Dodoma akiwa bado na lile panga alilotumia kumuua Askari. 

 Hata hivyo walichukua sheria mkononi na kumshambulia sehemu mbalimbali za mwili wake, Polisi walifika eneo la tukio na kumchukua kisha kumkimbiza Hospitali ya Mkoa lakini daktari akagundua ameshafariki. 
 Aidha Kamanda MISIME amesema mtuhumiwa huyo katika kumbukumbu tulizonazo ni kwamba mwaka 2006 aliwahi kufungwa miaka mitatu (3) kwa kosa la kujeruhi, Pia mwaka 2009 alifungwa tena miezi sita (6) kwa kosa la kutishia kuua. 
 Ametoa pongezi kwa wananchi kwa kuonyesha kuchukizwa na kitendo alichomtendea Askari wetu lakini waache kujichukulia sheria mkononi. 
Pia ametoa wito kwa wananchi tuanze kuchukua hatua kurekebisha maadili kuanzia ngazi ya familia kwani tumeelezwa kuwa mtuhumiwa alikuwa ni mvutaji bangi kiasi kwamba ilimfanya awe anafanya vitendo ambavyo ni kinyume na maadili na sheria za nchi.

WAZIRI WA UJENZI AKAGUA BARABARA MKOANI KATAVI


Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akiagana na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Eng. Stella Manyanya mara baada ya kukagua barabara za mkoa wa Rukwa.

Mkuu wa Wilaya ya Mlele Col.Ngemela Eslom Lubinga akisoma taarifa ya mafanikio ya Serikali ya wilaya hiyo  kwa Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli.
Sehemu ya barabara ya Sumbawanga-Kanazi km 75- ambayo ujenzi wake umekamilika kwa zaidi ya asilimia 60.
Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akiimba pamoja na wanafunzi wa shule ya msingi Wilayani Nkasi mara baada ya kuwasalimia alipokuwa njiani kukagua mradi wa barabara unaopita  karibu na shule hiyo.
Sehemu ya barabara ya Sumbawanga-Matai-Kasanga km 112 ambayo ujenzi wake unaendelea kujengwa kwa kiwango cha lami.
Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akiwahutubia wakazi wa Kibaoni kuhusu kuwasimamia makandarasi wanaojenga barabara za Kanazi-Kizi-Kibaoni kwa kiwango cha lami.
Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akiagana na wakazi wa Kibaoni Wilayani Mlele katika mkoa wa Katavi.
Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akiwa na Mama mzazi wa  Waziri Mkuu Mheshimiwa Mizengo Pinda nyumbani kwake Kibaoni mkoani Katavi. Waziri wa Ujenzi alipita kumsalimia mara baada ya kuwahutubia wakazi wa Kibaoni kuhusu masuala mbalimbali ya barabara na nyumba za Serikali.
Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akihutubia mamia ya wakazi wa Katavi kuhusu miradi mikubwa ya barabara katika mkoa huo.
Waziri wa Ujenzi akiagana na wananchi wa Katavi mara baada ya kuwahutubia.Picha zote na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Wizara ya Ujenzi.

Thursday, February 5, 2015

DKT. NCHIMBI ASEMA CCM HAINA TATIZO LA KIMUUNDO WALA MFUMO


 

nchimbi 3



nchimbi 4




nchimbi 2



nchimbi 1

CCM TABORA YAWATUNUKU VYETI MAKADA WAKE WALIOKISAIDIA CHAMA HICHO KUPATA USHINDI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA


Katibu wa CCM mkoa wa Tabora Bi.Jannat Kayanda akimkabidhi cheti mmoja kati ya makada wa chama hicho Bw.Emmanuel Mwakasaka waliokisaidia kupata ushindi wakati wa uchaguzi wa Serikali za mitaa,vijiji na vitongoji wilaya ya Tabora mjini ambapo CCM ilipata ushundi mkubwa dhidi ya vyama vya upinzani.
Katibu wa CCM mkoa wa Tabora Bi.Jannat Kayanda akizungumza katika maadhimisho ya 38 ya kuzaliwa kwa CCM yaliyofanyika kijiji cha Mwisole wilayani Uyui ambapo aliwataka wananchi kuendelea kukiamini chama hicho kwakuwa kimewaletea maendeleo ikiwa ni pamoja na kudumisha amani na utulivu wa Taifa.
Hawa ni makada mahili wa CCM mkoa wa Tabora("MAJEMBE YA CCM TABORA")ambao wametambulika michango yao katika kukisaidia chama kwa hali na mali na kuhakikisha chama kinaendelea kujenga heshima yake katika kuwaongoza wananchi.
Mjumbe wa halmashauri kuu ya CCM wilaya ya Tabora mjini ambaye ni kada wa chama hicho  Bw.Emmanuel  Mwakasaka akionesha heshima ya utii mbele ya viongozi baada ya kupokea cheti cha kumpongeza na kutambua mchango wake katika kukisaidia chama kupata ushindi uchaguzi wa Serikali za mitaa,vijiji na vitongoji wa mwaka 2014 ambapo CCM iliibuka mshindi dhidi ya vyama vya upinzani.



POLISI TABORA WAFANIKIWA KUMTIA NGUVUNI KIJANA MMOJA AKIWA NA RISASI 356 ZA SMG


Jumla ya risasi 356  za SMG zilizokamatwa askari Polisi  kwa kijana mmoja aliyefahamika kwa jina la Wolfram Msemwa(32) huko katika mtaa wa Kazehill kata ya Ng'ambo manispaa ya Tabora.
Kitambulisho cha mtuhumiwa aliyekutwa na risasi hizo ambaye kabla ya kukamatwa tarehe 2/2/2015 aliwahi kuwakimbia askari Polisi  mnamo tarehe 23/11/2014 na kutelekeza begi alilokuwa amehifadhi bunduki aina ya SMG na risasi 17 katika eneo la Mazinge hospitali ya wilaya ya Sikonge

Kaimu kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora ACP Juma Bwire akiwaonesha waandishi wa habari risasi zilizokamatwa katika operesheni maalumu iliyofanikiwa kumtia nguvuni kijana huyo Wolfram Msemwa anayedaiwa amekuwa na mtandao na baadhi ya waharifu kutoka nchi jirani na Tanzania kwa upande wa Magharibi.


Tuesday, February 3, 2015

BONDIA CHEKA AHUKUMIWA KWENDA JELA MIAKA 3

cheka
Bondia Francis Cheka leo February 2 2015 amehukumiwa kwenda jela miaka mitatu na faini ya Milioni moja laki sita kwa kosa la kumpiga mmoja kati ya wafanyakazi wake kwenye bar yake iliyopo Morogoro.

Muda mfupi uliopita Francis Cheka ameongea na millardayo.com na kusema ndio alikua anajiandaa kuachia simu yake na vitu vingine muhimu ili achukue karandinga kuelekea gerezani ambapo namnukuu akisema ‘imeshakua hivi tayari ila hamna noma, niko na wanangu wengine wamepigwa miaka 10 nitakua nao fresh tu ila hamna noma ni miaka mitatu tu mimi’
Hukumu imetolewa na Hakimu Mkazi Said Msuya ambapo baada ya hayo upande wa Francis Cheka unasemekana kujiandaa kukata rufaa.

MBUNGE FILIKUNJOMBE ALAZAMIKA KULALA KATIKA “PAGALE” AKITEKELEZA AHADI YA UMEME KIJIJI CHA KILONDO

 

Mbunge  wa  jimbo la  Ludewa Deo Filikunjombe akiwahutubia  wananchi wa  kijiji  cha Kilondo Ludewa
Mbunge  Filikunjombe  akisisitiza jambo  wakati akizungumza na  wananchi wa kijiji cha Kilondo
Mwenyekiti wa kata ya  Kilondo wa Chadema Bw  Edgar Kyula  akimpongeza  mbunge wa  wa Ludewa  Deo Filikunjombe kushoto  wakati wa mkutano wake  kijijini Kilondo
Baadhi ya  viongozi wa kata ya  Kilondo  wakimpongeza Filikunjombe  kulia
Mbunge  Filikunjombe akikabidhi nyavu za  kuvulia  samaki kwa ajili ya vikundi  vya vijana  wote  Kijiji cha  Kilondo na Lusisi Ludewa
Filikunjombe kushoto akikabidhi vifaa  vya  michezo kwa  vijana  kijiji cha Kilondo ili baada ya kazi kufanya  michezo
 
Mbunge  Filikunjombe wa tatu  kulia akiwa na viongozi wa kijiji  cha Kilondo na Lusisi ambao aliwapa nyavu na vifaa vya  michezo
Mbunge  Filikunjombe akiwa amembeba mmoja kati ya  watoto  kijiji cha Kilondo  wakati wa mkutano wake kijijini hapo
Kikongwe  mkazi wa kijiji cha Kilondo  akisalimiana na mbunge wa  Ludewa Deo  Filikunjombe baada ya  kumalizika kwa mkutano  wake kijijini hapo
 
Mtaalam  wa  umeme akimuelekea  mbunge Filikunjombe mambo ya kitaalam baada ya  kutembelea  maporomoko ya mto Makete ambao utatumika kuzalisha  umeme  kushoto ni katibu wa mbunge Filikunjombe Bw Stany Gowele
Mtaalam akimwonyesha maporomoko hayo ya maji mbunge Deo  Filikunjombe
Huu  ndio mto  utakao  zalisha umeme kijiji cha Kilondo Ludewa
Mbunge Filikunjombe akitazama mto huo
Huu ni mto  Makete  unaomwaga maji yake ziwa nyasa
Mbunge  Filikunjombe akitazama mto Makete
Wataalam  wakimwaga maji  yenye  chumvi mto  Makete  ili kupima  nguvu ya maji katika mto huo kwa ajili ya kuanza uzalishaji  wa umeme katika kijiji cha Kilondo Ludewa
Kipimo kwa ajili ya  kujua kasi ya maji katika mto Makete
Wakazi wa kijiji  cha Kilondo Ludewa
Mbunge  Filikunjombe akiongoza  msafara  wake kwenda  kupanda  bodi baada ya  kuamka alfajiri katika kijiji  cha Kilondo Ludewa
Mbunge wa  jimbo la  Ludewa Deo Filikunjombe (kulia) akiwa katika  boxhuku ameshika tama  eneo la kando ya  ziwa  nyasa juzi alfajiriakisubiri  usafiri wa bodi kuelekea  Matema wilayani Kyela baada ya kufanya  ziara ya  siku  mloja  kijijini Kilondo  wengine  pichani nimkurugenzi wa kampuni ya Kilondo Investment  Bw Erick Mwambeleko  wapili  kushoto ,katibu mwenezi mkoa wa Njombe Honolatus Mgaya na katibu
mwenezi wilaya ya Ludewa Bw  Felix
Msafara  wa mbunge  Filikunjombe ukijiandaa kupanda katika  bodi  Ziwa nyasa
Mwanahabari  Emmanuel Msigwa wa Chanel  Ten akipanda katika bodi
Baadhi ya  wasafiri  wa ziwa nyasa  wakisafiri kutoka Matema Kyela  kwenda Manda Ludewa
Na matukiodaimaBlog
WANANCHI
wa  kijiji  cha KIlondo kata ya  Kilondo  wilayani Ludewa
mkoani Njombe
wamempongeza  mbunge wa  jimbo la  Ludewa Deo Filikunjombe  kwa  kuwa
mbunge  pekee  katika  jimbo  hilo kufika kulala chini ardhini kwenye
nyumba isiyo na mlango wala dirisha (Pagale) katika
kijijini hicho
toka  nchi ipate uhuru wake mwaka 1961.Mbunge
Filikunjombe na  msafara  wake  wa watu  zaidi ya 15  walifika katika
kijiji  hicho  cha Kilondo kilichopo mwambao mwa ziwa nyasa  kwa lengo
la mbunge  huyo kuwaanzishia  mchakato  wa kupatiwa umeme  kupitia
shirika  lisilo la  kiserikali la Kilondo Investment linalofadhiliwa na
mradi  wa usambazaji  vijijini (REA)
Akizungumza
kwa niaba ya  wananchi  wa kijiji   hicho mwenyekiti wa  serikali ya
kijiji   hicho Bw Laurian Kyula alisema  kuwa  jimbo  hilo  limepata
kuwa na  wabunge zaidi ya  5 ila   hakuna  mbunge  ambae  alifika na
kukubalia  kulala  katika  kijiji  hicho  kutokana na  kuwa na miundo
mbinu mibovu na  kutokuwa na nyumba  ya  kisasa  ya
kulala  wageni zaidi
ya  nyumba  za  wananchi ambazo  nyingi  zipo kienyeji  zaidi hazina hadhi .
“Kweli tumeshindwa  kuamini  kuona  mbunge anaamua  kulala  kijiji  hapa
hata  bila kuwepo kwa maandalizi mazuri ya  kulala tumekuwa na wabunge  wengi  sana ila  wapo  baadhi yao hata kukejeli  kuwa  kijiji  hakina  hadhi ya  kulaza  waheshimiwa  hadi  watakapoboresha mazingira kati ya  viti ambavyo hatukupata  kufikiria  ni pamoja na
kuja  kupokea  mgeni  wa  kiwilaya kuja  kulala  hapa  kijijini ila wewe  mheshimiwa wetu Filikunjombe umekuwa ni kiongozi wa aina yake”
alisema  mwenyekiti   huyo 
Akimpongeza mbunge  huyo kwa jitihada  zake za  kuwasogezea  huduma  ya  umeme
kijijini hapo  mwenyekiti  huyo    alisema kijiji  hicho   ni moja kati vijiji ambavyo  vipo mwambao  mwa  ziwa nyasa na  uwezekano  wa kuunganishwa na  umeme  wa gridi ya  Taifa   kutoka  Ludewa mjini ama
Kyela mkoani Mbeya ni  vigumu  kutokana na kuzungukwa na milima  na maji
hivyo  kwa  upande  wao  waliamini kabisa kamwe hawatakuja  fikiwa na
huduma  za umeme.
“Tunashindwa kujua ni  kiasi gani mbunge  wetu  unavyotuhangaikia  kwa
mambo ambayo  wengine  waliotangulia  walituhakikishia  kuwa ni  vigumu
kufikiwa na huduma ya  umeme kwa  kuwa ni porini labda  haditutakaposogea karibu na vijiji  vya nje ya  Mwambao kauli ambazo vilitufanya  kukata tamaa kabisa kwa  umeme kwetu ni huduma  isiyo wezekana ila  tunashangazwa leo kupitia mbunge wetu Jembe
Filikunjombe unatuletea wataalam wa kuanza kujenga mradi wa umeme hapa
kijijini”
 
Bw Kyula  alisema kati ya  mambo ambayo  wao  hawata kuja  kusahau maishani mwao ni utendaji kazi wa mbunge  huyo na  maendeleo makubwa
aliyoyafanya katika  jimbo  hilo la  Ludewa kwa kipindi  cha miaka minne ya  ubunge  wake huku  wapo waliokaa miaka  mitano  bila  kufanyajambo linaloonekana kwa   wananchi  wao.
Hivyo alisema  iwapo  chama  cha mapinduzi (CCM)  kitataka  kulipoteza  jimbo
hilo la Ludewa ni pamoja na  kujaribu  kufanya maamuzi yasiyo hitajika
kwa  wananchi yakiwemo ya  kukata  jina la mbunge  wao katika mchakato
wa kuomba  kugombea ubunge    jimbo  hilo la Ludewa na kumpa nafasi  mtu
wa kwao watashangazwa na maamuzi magumu ya  wananchi kwa  kulitoa
jimbo hilo upinzani kama  fundisho kwa CCM kupenda wanachopenda  wao na
sio wananchi.
Awali mkurugenzi mtendaji wa  mradi wa Kilondo Investment Bw  Erick
Mwambeleko akielezea  mradi huo alisema  kuwa  mpango  wa kuwaunganisha
wanakijiji  hao na umeme  ulikuwepo toka  wakati mbunge Profesa Raphael
Mwalyosi akiwa madarakani  ila cha kushangaza kila alipomfuata  kutaka
kusaidia kufanikisha kuanzishwa  kwa mradi huo  aliishia  kutoa kauli
za kukatisha tamaa  kuwa haweza  kusaidia  kupeleka  umeme kijijini hapo
kwa kuwa ni gizani sana hakuna faida yoyote .
“Ni  kweli kijiji  hiki cha Kilondo  kipo porini  zaidi  ila  kuna
watu  wanaishi hata  mimi Mwambeleko ni mzaliwa wa hapa  hivyo
nimesoma  sayansi na kutumia elimu yangu nikaona  ngoja  nishirikiane na
mbunge Filikunjombe  kuleta ukombozi  wa  umeme  huku kwa kupitia
kampuni yangu ya Kilondo Investment kampuni ambayo mchango wa mbunge  ni
mkubwa zaidi hadi leo tunaanza mchakato wa kuleta  umeme hapa”Alisema
kuwa tayari  fedha kiasi cha  zaidi ya Tsh milioni 300  zimepatikana
kwa ajili ya kuanza  utekelezaji wa mradi huo ambapo  fedha  hizo kiasi
zimetoka REA na nyingine ni fedha  ambazo ni mchango wa mbunge
Filikunjombe .
Pia alisema  umeme   huo  utazalisha  kijijini hapo  kupitia maporomoko ya
maji ya mto Makete  ambayo yanaingia katika  ziwa nysa  na kuwa
maporomoko hayo yana nguvu  ya  kuzalisha  umeme KV 50 na  kasi ya maji
katika maporomoko hayo ni lita  za ujazo 9312 kwa  sekunde maji ambayo
yanatosha kabisa kwa  uzalishaji wa umeme  wa kutosha kaya  zote
kijijini hapo na kijiji cha jirani.
 
Kwa upande  wake  mbunge  Filikunjombe akielezea  sababu ya  kulala kijijini hapo alisema  kuwa moja kati ya ahadi yake kwa  wananchi wa
Ludewa ni  kufikisha maendeleo kila  kona ya  jimbo  hilo na kuwa akiwa katika  ziara  pale ambapo  jua litazamia ndipo atakapolala  bila kujali uwepo wa maandalizi ama lah.
 
“Wananchi wote wa Ludewa ni  wapiga kura  wangu hivyo imekuwa ni kawaida  yangu
kuwa nao  wakati  wote na  kulala popote na  kula  chochote ambao  wao
wanakula  siku  zote hivyo  jua linapozamia nikiwa
ziarani
nitalala hapo bila  kujali maandalizi lengo  kuona  nashirikiana na wananchi wangu kwa mazingira  yoyote yale nimefurahi  sana  leo kulala katika  nyumba  hii inayojengwa ambayo haina sakavu ,milango wala
madirisha (Pagale) mimi ni siufanyi ubunge kama ufalme kuwa nikija mimi ziarani  wananchi wangu  wasumbuke kufanya maandalizi yasiyo ya
kawaida”
Kuhusua mradi  huo wa umeme Filikunjombe alisema  kuwa lengo lake kuona
wananchi hao  wanapatiwa umeme mapema  zaidi  ikiwezekana ndani ya mwaka
huu wananchi hao  waweze na  umeme  katika makazi yao  hivyo  kuwaomba
wananchi kutoa  ushirikiano kwa mafundi  waliofika kijijini  hapo
kuanza  utekelezaji wa mradi huo pamoja na kuwasaidia  kufanya tathimini
ya mahitaji ya taa na ufungaji  umeme katika  nyumba  zao.