Saturday, April 18, 2015

VIJANA WA CCM IRINGA WAMPA NGUVU KATIBU WA MKOA HASSAN MTENGA KUKOMBOA JIMBO, LA IRINGA MJINI


Katibu wa CCM Mkoa wa Iringa, Hassan Mtenga katika kikao na baadhi ya vijana hao












KIU ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Manispaa ya Iringa kukomboa jimbo la Iringa Mjini katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba mwaka huu inazidi kuongezeka, baada ya umoja wake wa vijana (UVCCM Manispaa ya Iringa) kuahidi kuongeza nguvu ili kuufanikisha mkakati huo.



CCM ililipoteza jimbo hilo katika Uchaguzi Mkuu wa 2010 kwa Mchungaji Msigwa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) anayekaribia kumaliza muda wake.



Katika kikao kilichozikutanisha sekretarieti za umoja huo kutoka katika kata zote 18 za manispaa ya Iringa, Mwenyekiti wa UVCCM wa manispaa hiyo, Kaunda Mwaipyana alisema; “katika kukisaidia chama kushinda uchaguzi huo, kauli mbiu yetu ni chama kwanza mtu baadaye.”



“Tutapita katika matawi na kata zetu zote, tutafanya vikao, mikutano ya hadhara na kuwakumbusha vijana wajibu wa kukipigania chama chao ili mkakati wa kulikomboa jimbo ufanikiwe,” alisema.



Katibu wa CCM wa Mkoa wa Iringa, Hassan Mtenga aliwaongezea hamasa vijana hao kwa kuwapa seti 60 za jezi na mipira watakazozitumia kuwahamasisha vijana hao kupitia mchezo wa soka.



“CCM ina vijana wengi sana katika jimbo hili, mnahitaji kukutana na kujipanga, tumieni mbinu zote za kukutana, iwe  vikao, mikutano na hata michezo na ndio maana nimewapa msaada huu,” alisema.



Aliwataka vijana wa chama hicho kujitokeza kwenye vikao visivyo rasmi vya maeneo yao wanayoishi na kuitetea CCM kwasababu majibu ya hoja nyingi za wapinzani wanayo.



Akiwakabidhi jezi hizo, Mwenyekiti wa Umoja wa Wazazi wa CCM Mkoa wa Iringa, Ephraim Mhekwa alisema  CCM inayo nafasi ya kulikomboa jimbo hilo kama itajipanga vizuri.



“Pamoja na kwamba wapinzani walipata viti 65 katika uchaguzi wa serikali za mitaa wa mwaka jana, wasisahau kwamba CCM ilipata viti 126; hesabu hiyo inadhihirisha chama chetu kinaungwa mkono mara mbili yao,” alisema.



Aliwataka vijana hao kuweka bendera za chama hicho kila panapostahili katika mitaa yote na akawasihi wasikubali kutumika na kukigawa chama kwa maslai ya wachache.



Naye Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM, Mahamudu Madenge alisema CCM itaendelea kuwepo hata kama watu wasiotaka kufuata utaratibu wataondoka.


“Wameondoka wengi, wengine hii leo ni viongozi wa vyama vikubwa vya siasa. Pamoja na kuondoka kwao CCM ipo pale pale na inaendelea kupata wanachama,” alisema

KIWANDA CHA TUMBAKU MOROGORO CHAFANYA SHERERE KUFUNGA MSIMU NA KUFUNGUA MSIMU MPYA

 

Mkurugenzi Mkuu wa Makampuni ya Tumbaku ya Tanzania Tobacco Procesing Limited (TTPL) na Tanzania Leaf Tobacco Company (TLTC) David Crowhorst Akitoa hotuba yake wakati wa sherehe za kumaliza msimu uliopita na kukaribisha msimu mwingine pamoja na kutoa zawadi kwa wafanyakazi waliotumikia kampuni hizo kwa muda mrefu pamoja na wafanyakazi bora zilizofanyika Kiwandani hapo.Katika Hotuba yake Mkurugenzi Huyo alisema Makampuni hayoyamesaidia Mkoa wa Morogoro kuanza kuinuka kiuchumi kutokana na kutoa ajira za msimu takribani 3000 kila mwaka na kusaidia kupunguza matatizo ya uhalifu yaliyokuwa yakifanywa na vijana wasio kuwa na shughuli  za kujiingizia kipato. 
Mkurugenzi mkuu wa Makampuni ya Tumbaku ya Tanzania Tobacco Procesing Limited (TTPL) na Tanzania Leaf Tobacco Company (TLTC) David Crowhorst Akikabidhi zawadi kwa wafanyakazi waliofanya kazi kwa muda mrefu Ambao wamefanya kazi kwa zaidi ya Miaka 15 Mfululizo.
Mkurugenzi mkuu wa Makampuni ya Tumbaku ya Tanzania Tobacco Procesing Limited (TTPL) na Tanzania Leaf Tobacco Company (TLTC) David Crowhorst Akiwapakulia Chakula waliokuwa wafanyakazi wa kiwanda hicho wakati wa tafrija hiyo
Mkurugenzi wa Ufundi wa Makampuni ya Tumbaku ya Tanzania Tobacco Procesing Limited (TTPL) na Tanzania Leaf Tobacco Company (TLTC) Henry Lembert Akiwahudumia wafanyakazi wa kiwanda hicho wakati wa Sherehe ya Kufunga Msimu.

Mkurugenzi mkuu w David Crowhorst akiwa na baadhi ya wafanyakazi wa Kiwanda hicho
 Picha ya Pamoja ya waliokuwa wafanyakazi wa kiwanda cha Tumbaku  cha Mkoani Morogoro

MABARAZA YA WAFANYAKAZI TAASISI ZA ELIMU YA JUU YATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI

Naibu Waziri wa Fedha (Sera) Mhe. Mwigulu Nchemba (katikati) akiwa ameambatana na Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania Dkt. Joseph Kihanda (kulia) na Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Wizara Prof. Isaya Jairo kabla ya kuzindua Baraza la Pili la Wafanyakazi wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) lililojumuisha wawakilishi kutoka matawi 6 ya taasisi hiyo katika mikoa ya Kigoma, Singida, Mwanza , Mtwara, Dar es salaam na Mbeya.
Naibu Waziri wa Fedha (Sera) Mhe. Mwigulu Nchemba wakati akizindua Baraza la Pili la Wafanyakazi wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) leo mjini Bagamoyo.
Wajumbe wa Baraza la Pili la Wafanyakazi wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) wakiimba wimbo wa mshikamano daima kabla ya kuanza kwa mkutano wao leo mjini Bagamoyo.

Wajumbe na viongozi wa Baraza la Pili la Wafanyakazi wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) wakiwa katika picha ya pamoja na Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Mwigulu Nchemba (katikati) mara baada ya kuzinduliwa kwa baraza hilo leo mjini Bagamoyo. Picha na Aron Msigwa/MAELEZO.

Na. Aron Msigwa –MAELEZO.

SERIKALI imeyata Mabaraza ya wafanyakazi wa Taasisi za Elimu ya juu kote nchini kufanya kazi kwa bidii na kuzingatia weledi, kanuni na sheria zinazosimamia  mabaraza hayo ili yawe chachu katika kuleta maendeleo ya Elimu  na mabadiliko ya kiuchumi ya taasisi hizo.

Kauli hiyo imetolewa  na Naibu Waziri wa Fedha (Sera) Mhe. Mwigulu Nchemba wakati akizindua Baraza la Pili la Wafanyakazi wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) lililojumuisha wawakilishi kutoka matawi 6 ya taasisi hiyo  katika mikoa ya Kigoma, Singida, Mwanza , Mtwara, Dar es salaam na Mbeya.

Mhe. Mwigulu amesema kuwa iwapo mabaraza hayo yatazingatia weledi katika kusimamia masuala mbalimbali ya taasisi hizo nchini  yataleta mabadiliko ya kiutendaji katika usimamizi wa mapato na matumizi  na kutoa  ushauri utakaoisaidia Serikali kutekeleza mipango mbalimbali ya  maendeleo.

Mhe. Mwigulu ameeleza  kuwa endapo mabaraza hayo yataacha kufanya kazi kwa mazoea na kujikita katika kuzingatia kanuni na taratibu zilizowekwa, taasisi hizo zitaongeza uzalishaji, zitakuza mapato na kutatua kero mbalimbali za wafanyakazi mahali pa kazi.

“ Napenda niweke wazi kuwa mabaraza haya  ni muhimu sana kwa wafanyakazi, hayana tofauti na bunge ,kazi yake  kubwa ni kusimamia mapato na matumizi, kushauri taasisi na Serikali juu ya utekelezaji wa  mipango mbalimbali ikiwemo ajira kwa watumishi wapya” Amesisitiza.

Akizungumzia changamato ya uhaba wa walimu na watumishi wa kada mbalimbali  katika taasisi hiyo na taasisi nyingine za Umma za Elimu ya juu amesema Serikali inaendelea  kutenga fedha katika bajeti ya kila mwaka ili kuondoa tatizo hilo.

Aidha, amesema Serikali inaendelea kulishughulikia suala la usimamizi wa ziada ya mapato yanayozalishwa na taasisi za umma ili yaweze kupelekwa  katika maeneo mengine yenye uhitaji.

“Serikali tunaendelea kuangalia utaratibu wa kutumia ziada ya mapato inayozalishwa na taasisi mbalimbali za umma ili iweze kupelekwa katika maeneo mengine yenye uhitaji maana fedha hizi ni za umma,taasisi moja ya Serikali haiwezi kung’ania ziada ya mapato iliyozalisha, hizo ni fedha za umma lazima zikafanye kazi maeneo mengine yenye uhitaji hasa kwenye kugharamia mahitaji ya wodi za akina mama kote nchini”

Pia amesisitiza mkakati wa Serikali wa kuzifanya taasisi hizo za elimu ya juu kuwa na mamlaka yake katika kuajili watumishi wake na kjitegemea.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Baraza hilo ambaye ndiye Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania Dkt. Joseph Kihanda  akizungumza na wajumbe wa baraza hilo amesema kuwa taasisi hiyo katika kipindi cha miaka 5 imepata mafanikio makubwa ya kuongeza  ukusanyaji wa mapato kutoka shilingi Bilioni 6 za mwaka 2010 hadi kufikia shilingi Bilioni 18 mwaka 2014/2015.

Amesema Taasisi hiyo licha ya kukabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ya uhaba wa miundombinu, ufinyu wa bajeti , uhaba wa walimu wenye shahada za uzamivu (PhD)  na watumishi kimeendelea kupata idadi kubwa ya wanafunzi wanaodahiliwa kutoka  7635 waliodahiliwa mwaka 2011/2012 hadi kufikia 14974 mwaka 2014/2015.

“Licha ya kuendelea kufanya vizuri taasisi yetu inakabiliwa na tatizo la waalimu katika matawi yetu yaliyo mikoani ,jambo hili hutufanya tutumie gharama kubwa kuwasafirisha kutoka makao makuu kwenda kufundisha wanafunzi wetu wanaochukua michepuo ya Biashara, Uhasibu, Rasilimali Watu, Ununuzi na Ugavi,Uhasibu katika Sekta ya Umma na Masoko na Mahusiano kwenye matawi yetu” Amesisitiza.  


Naye Mwenyekiti wa Bodi ya ushauri ya wizara ya Fedha wa Taasisi hiyo Prof. Isaya Jairo akizungumza na wajumbe waliohudhuria mkutano huo amesema kuwa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA)katika kukuza na kuongeza mapato ya ndani na kupunguza utegemezi kutoka serikalini itaendelea kufanya shughuli kibiashara ,kufanya utafiti, kutoa ushauri katika Nyanja za uhasibu, ununuzi na ugavi kote nchini.

MAMLAKA YA MAJI SAFI NA USAFI WA MAZINGIRA MJINI MOSHI(MUWSA) YAKAMATA WEZI WA MAJI

Watumishi wa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi,MUWSA,wakiwa katika nyumba moja ambayo inadaiwa mmiliki wake alikuwa akiiba maji baada ya kujiunganishia kinyemera licha ya kukatiwa huduma hiyo kwa muda mrefu.
Wafanyakazi hao wakiongozwa na afisa uhusiano wa mamlaka hiyo ,Frolah Nguma na mkuu wa kanda ya Rau ,Selemani Zabron na fundi Aminiel Swai baada ya kufuatilia katika eneo hilo walibaini wapi wizi wa maji unafanyika.
Hivi ndivyo ilivyooonekana katika mauongio ya mteja wa mamlaka hiyo ambaye mtuhumiwa wa wizi wa maji alifanya usanii wa kujiungia maji bila ya kulipia huku mzigo wa kulipia ankala ya maji ikibaki kwa jirani yake aliyeunganisha bomba kwenye line yake.
Fundi wa Mamlaka ya Maji safi na usafi wa Mazingira mjini Moshi,MUWSA,Aminiel Swai akiondoa bomba liliunganishwa kwa wizi .
Mkuu wa kanda ya Rau wa mamlaka ya Maji safi na usafi wa mazingira mjini Moshi Selemani Zabron akifukia eneo ambalo hujuma ya kujiunganishia maji ilikuwa imefanyika.
Mmiliki wa nyumba hii ndiye line ya kupeleka maji kwake imekutwa ikiwa imefanyiwa hujuma na kulazimika kulipa bili ya matumizi ya maji kwa nyumba mbili.
Watumishi wa MUWSA wakitizama kama maji yanatoka katika nyumba hiyo mara baada ya kuondoa bomba ambalo lilikuwa likitumika kupeleka maji katika nyumba nyingine kwa njia ya wizi.Hata hivyo katika operersheni hiyo Mtuhumiwa pamoja na mkewe walilazimika kuikimbia nyumba yao na kutelekeza watoto wao wawili wakiume wenye umri wa kati ya miaka miwili na minne.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

WAZIRI LUKUVI AHITIMISHA ZIARA YA SIKU MBILI,ASHUHUDIA UTENDAJI WA NHC


Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Vangimembe Lukuvi akikagua mradi wa nyumba za gharama nafuu za makazi za Kibada, Kigamboni alipokuwa akikagua mradi huo mchana wa leo. Nyumba za gharama nafuu za NHC Mwongozo, Kigamboni Dar es Salaam zinavyoonekana leo wakati Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Vangimembe Lukuvi alipozitembelea. Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Vangimembe Lukuvi akisikiliza maelezo ya Injinia wa NHC, Elisante Ulomi anayesimamia Mradi wa Mwongozo Housing Estate mchana wa leo. Mojawapo ya Nyumba za gharama nafuu za NHC Kibada, Kigamboni Dar es Salaam inavyoonekana leo wakati Waziri Lukuvi alipozitembelea. Nyumba za gharama nafuu za NHC Kibada, Kigamboni Dar es Salaam zinavyoonekana leo wakati Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Vangimembe Lukuvi alipozitembelea. Waziri Lukuvi akikagua mradi wa nyumba za gharama nafuu za makazi za Kibada, Kigamboni alipokuwa akikagua mradi huo mchana wa leo. Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Vangimembe Lukuvi akikagua mradi wa nyumba za gharama nafuu za makazi za Kibada, Kigamboni alipokuwa akikagua mradi huo mchana wa leo. Waziri Lukuvi akikagua mradi wa nyumba za gharama nafuu za makazi za Kibada, Kigamboni alipokuwa akikagua mradi huo mchana wa leo. Nyumba za mradi mkubwa wa NHC Morocco Square, Dar es Salaam zikiwa zinajengwa katika hatua ya msingi, zinavyoonekana leo wakati Waziri Lukuvi alipozitembelea. Nyumba za mradi mkubwa wa NHC Morocco Square, Dar es Salaam zikiwa zinajengwa katika hatua ya msingi, zinavyoonekana leo wakati Waziri Lukuvi alipozitembelea. Nyumba za mradi mkubwa wa NHC Morocco Square, Dar es Salaam zikiwa zinajengwa katika hatua ya msingi, zinavyoonekana leo wakati Waziri alipozitembelea. Nyumba ya mfano itakayojengwa katika kitalu nambari 300 kona ya kuelekea kwenye Hospitali ya Mikocheni jijini, Dar es Salaam leo wakati Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Vangimembe Lukuvi alipozitembelea. Waziri Lukuvi akipata maelezo ya Nyumba ya mfano itakayojengwa katika kitalu nambari 300 kona ya kuelekea kwenye Hospitali ya Mikocheni jijini, Dar es Salaam leo. Waziri Lukuvi akikagua mradi wa nyumba za NHC Victoria zinazojengwa na NHC alipokuwa akikagua mradi huo mchana wa leo. Waziri Lukuvi akipata maelezo ya mradi wa nyumba za NHC Victoria zinazojengwa na NHC alipokuwa akikagua mradi huo mchana wa leo. Waziri Lukuvi akipata maelezo ya mradi wa nyumba za NHC Victoria zinazojengwa na NHC alipokuwa akikagua mradi huo mchana wa leo. Waziri Lukuvi akipata maelezo ya mradi wa nyumba za NHC Victoria kutoka kwa Mkurugeni wa Ubunifu wa NHC, Issack Peter alipokuwa akikagua mradi huo mchana wa leo. Mmojawapo wa mafundi wajenzi wanaojenga nyumba hizo za Victoria akiwa kazini wakati wa ziara ya Waziri.

MWAKASAKA ACHAGULIWA KUWA MJUMBE WA MKUTANO MKUU TAIFA,AMBWAGA MWENYEKITI WA UWT

 

Bw.Emmanuel Adamson Mwakasaka akiwashukuru wajumbe wa Halmashauri kuu ya CCM wilaya ya Tabora mjini baada ya kuchaguliwa kuwa Mjumbe wa Mkutano mkuu Taifa kwa kupigiwa kura 130 kati ya 149 huku akifuatiwa na mtu wa pili ambaye ni Mwenyekiti wa UWT ambaye alipata kura 5.
Mjumbe wa mkutano mkuu Bw.Emmanuel Mwakasaka akiahidi kufanya kazi kwa pamoja na wanaccm wenzake katika kuendeleza shughuli za Chama hicho.

Katibu wa CCM wilaya ya Tabora mjini Bw.Bakari Mfaume akimpongeza Mjumbe wa Mkutano mkuu wa CCM Taifa Bw.Emmanuel Mwakasaka kufuatia kushinda uchaguzi huo uliofanyika katika uwanja wa Ally Hassan Mwinyi.