Wednesday, October 9, 2013

SERIKALI INATAMBUA FURSA ZA WALEMAVU WILAYANI UYUI MKOANI TABORA

MRATIBU WA WAJASILIAMALI NA HAKI ZA KAZI KWA WALEMAVU WILAYA YA UYUI MKOANI TABORA HUSSEIN GEYA AKISOMA RISALA MBELE YA NKUU WA WILAYA YA UYUI LUCY MAYENGA

MWENYEKITI WA CHAMA CHA WALEMAVU MANISPAA YA TABORA JOHN KUKA AKIMKARIBISHA MKUU WA WILAYA YA UYUI KWA AKIJI YA KUFUNGUA MAFUNZO

MKUU WA WIALAYA UYUI LUCY MAYENGA AKIFUNGUA MAFUNZO YA UJASILIAMALI NA HAKI YA KAZI KWA WATU WENYE ULEMAVU KATIKA  UKUMBI WA KITUO CHA WANAFUNZI MJINI HAPA LEO

PICHA YA PAMOJA KATI YA MKUU WA WILAYA YA UYUI LUCY MAYENGA NA WATU MALI WENYE ULEMAVU MARA BAADA YA KUWAFUNGULIA MAFUNZO YA UJASILIA MALI NA HAKI YA KAZI KWA WATU WENYE ULEMAVU


NA LUCAS RAPHAEL TABORA




Halmashauri ya wilaya uyui mkoani Tabora kwa mwaka huu imetenga kiasi cha shilingi milioni 40 kwa ajili ya kuwakopesha  vijana na wanawake ili kuweza kujiongezea kipato na kujiunga katika vikundi  .
Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa wilaya ya Uyui Lucy mayenga wakati akifungua mafunzi ujasiliamali na haki za kazi kwa walemavu iliyofanyika katika ukumbi wa kituo cha wananafunzi mjini hapa .
Alisema kwamba fedha hizo zitolewa katika makundi hayo ambapo vijana wametengewa kiasi cha shilingi milioni 20 na wanawake wametengewa kiasi kama hicho.
Alisema kwamba fedha hizo ukopeshwa kwa riba nafuu ili kuwawezesha vijana na kinamama  kufanya marejesho bila maumivu  .
Mkuu huyo wa wilaya aliwataka walemavu hao kujiunga katika vikundi ambavyo vimesajiliwa na kuandaa andiko sanjari na kuwa na wathamini.
Awali mratibu wa mafunzo hayo Hussein Geya alisema kwamba mafunzo hayo yanalengo la kuboresha maisha ya watu wenye ulemavu kupitia vikundi vya wajasiliamali vya watu wenye ulemavu kutoka katika wilaya hiyo ya uyui vilivyowezeshwa kikamilifu na kutambulika kisheria.
Alisema kwamba katika kipindi cha utekelezaji mradi huo shughuli mbalimbali zitafanyika ikiwemo kutoa elimu kwa ajia ya redio na televishini ,kuendesha mafunzo mbalimbali ya ujasiliamali kwa watu wenye ulemavu .

 Mafunzo hayo yameandaliwa na chama cha walemavu wilaya ya uyui mkoani Tabora na kufadhiliwa na shirika la Akiba Uhaki Foundation la nchini kenya




Wednesday, October 2, 2013

SIKU YA WAZEE DUNIANI,WAZEE TABORA WANAHITAJI WAPATIWE MAENEO YA KUPIGIA STORY


Maandamano ya Wazee wa mkoa wa Tabora wakisheherekea Siku ya Wazee Duniani. 

"POLISI ATAKAYEWASUMBUA BODABODA SASA KUKIONA"-RC FATMA MWASSA


Mkuu wa mkoa wa Tabora Bi.Fatma Mwassa  akizungumza na wananchi wakati wa ufunguzi wa Ofisi ya Chama Cha Waendesha Bodaboda mkoa wa Tabora TTMA zilizopo eneo la Bachu kata ya Gongoni manispaa ya Tabora.Katika ufunguzi wa Ofisi hiyo pamoja na mkuu huyo kuwataka waendesha Bodaboda kufuata sheria za usalama barabarani lakini akatumia fursa hiyo kukomesha vitendo vya baadhi ya askari Polisi wasio waaminifu kutowafanya waendesha Bodaboda kuwa sehemu ya kipato chao kwa kuwalazimisha kutoa rushwa baada ya kuwabambikiza makosa wasiokuwa nayo.Aidha  Bi.Fatma Mwassa alisema serikali haitakubali kuvumilia vitendo vya kuwanyanyasa  Bodaboda ambao wamekuwa wakijitafutia riziki zao kwa kufanya shughuli hiyo ya halali.
 Mkuu wa mkoa wa Tabora Bi.Fatma Mwassa akikata utepe ikiwa ni ishara ya ufunguzi wa ofisi hiyo ya  Chama cha Waendesha Bodaboda Tabora,kushoto ni Mwenyekiti wa Chama hicho Bw.Waziri Kipusi.

Mkuu wa mkoa wa Tabora Bi.Fatma Mwassa akipata maelezo ya uendeshaji wa ofisi ya Chama cha Waendesha Bodaboda Tabora,hapa alikuwa akiangalia orodha ya wanachama ambao inaonesha mahali wanapoishi,takwimu za ajali pamoja na mahusiano yao na Jeshi la Polisi mkoa wa Tabora.
Mkuu wa mkoa wa Tabora Bi.Fatma Mwassa,mkuu wa wilaya ya Tabora mjini Bw.Suleiman Kumchaya,viongozi wa chama cha Waendesha Bodaboda Tabora  pamoja na wanachama hai wa Chama  hicho muda mfupi mara baada ya ufunguzi rasmi wa ofisi hiyo.  

TAMASHA LA MUNDE STAR SEARCH LIMEGHARIMU ZAIDI YA SHILINGI MIL.TISA

 
Maelfu ya baadhi ya  wananchi mjini Tabora wakishuhudia fainali ya Tamasha la kuibua vipaji kwa wasanii mbalimbali lililojulikana kama MUNDE STAR SEARCH lililofanyika katika viwanja vya Stand ya zamani ya mabasi.
Mabondia wawili kutoka Camp mbalimbali za Boxers wa Tabora walipokutana jukwaani kwa ajili ya kutafuta ushindi katka mashindano hayo yaliyodhaminiwa na Mbunge wa Vitimaalum mkoa wa Tabora Mh.Munde Tambwe ambaye pia ni mjumbe wa halmashauri kuu ya CCM Taifa. 
Mdhamini mkuu wa Tamasha la Munde Star Search ambaye pia ni Mbunge wa vitimaalum mkoa wa Tabora Bi.Munde Tambwe akisalimiana na wapiga masumbwi wanawake wakati wa Tamasha hilo ambalo linatajwa kuwa litakuwa likifanyika kila mwaka lengo likiwa ni kuibua vipaji vya wasanii chipukizi mkoa wa Tabora.
 Wapiga masumbwi uzito wa juu katika Tamasha la Munde Star Search wakichuana vikali na kuonekana kuwa kivutio kikubwa katika Tamasha hilo lililogharimu zaidi ya shilingi Milioni tisa.
Wachezaji wa Karate ambao nao walipambana vikali katika Tamasha hilo kwa muda wa dakika sita

Sunday, September 29, 2013

TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 LIKIENDELEA USIKU HUU NDANI YA UWANJA WA CCM KIRUMBA JIJINI MWANZA.

Muigizaji wa filamu lakini pia ni msanii wa muziki wa kizazi kipya,aitwaye kwa jina la kisanii Shilole akiimba mbele ya maelfu ya wakazi wa jiji la Mwanza na vitongoji vyake ndani ya tamasha la Serengeti fiesta 2013,ndani ya uwanja wa ccm kirumba usiku huu.
Anaitwa Christian Bella ambaye alikuwa akifanya vyema sana kwenye bendi ya muziki wa dansi ya Acudo,akiwaimbisha mashabiki wake usiku huu ndani ya tamasha la serengeti fiesta 2013.
Anaitwa Neylee,msanii wa bongofleva ambaye kwa sasa anafanya vyema sana kwenye anga ya muziki huo,akiimba kwa hisia mbele ya mashabiki wake usiku huu wakati tamasha la serengeti fiesta likiendelea 2013.
Pichani kati ni Meneja Mawasiliano wa kampuni ya simu za mikononi ya Zantel akiwa na marafiki zake wakilifuatilia tamasha la serengeti fiesta 2013 usiku huu ndani ya uwanja wa ccm kirumba,ambapo wakazi wa jiji la Mwanza wamejitokeza kwa wingi.
Kila kona ni ileee full maraha tuu,huku wakiburudika na vunywaji mbalimbali kutoka kampuni ya bia ya Serengeti ambao ndio wadhamini wakuu wa tamasha la serengeti fiesta wakishirikiana na PSI kupitia bidhaa yao ya Salama kondom.
Vijana machachari kabisa kutoka kinondoni wakitambulika kwa jina la KINOKO wakionesha umahiri wao wa kucheza ngoma za Michael Jackson mbele ya maelfu ya wakazi wa jiji la Mwanza.
Mmoja wa sanii waliofanya vyema sana katika shindano la BSS,Walter Chilambo,akiimba usiku huu kwenye jukwaa la Serengeti fiesta.
Mashabiki wa fiesta kibao usiku huu ndani ya ccm kirumba.
PICHA ZAIDI INGIA MICHUZIJR.BLOGSPOT.COM

MAGAZETI YA MWANANCHI NA MTANZANIA YAFUNGIWA



Serikali imeyafungia  kutochapishwa Magazeti ya MWANANCHI na MTANZANIA kuanzia  27 Septemba,2013  kutokana na mwenendo wa magazeti hayo kuandika habari  na makala  za uchochezi na uhasama kwa nia ya kusababisha wananchi  wakose imani kwa vyombo vya dola hivyo kuhatarisha amani na mshikamano  ulipo nchini.

Gazeti la MWANANCHI limefungiwa  kutochapishwa kwa siku kumi na nne(14) kuanzia 27 Septemba,2013.Adhabu  hii imetangazwa kwa Tangazo la Serikali(Government Notice )Namba 333 la  tarehe 27 septemba,2013.

Gazeti la MWANANCHI limepewa  adhabu hiyo kutokana na hivi karibuni kuchapisha habari zenye mwelekeo  wa uchochezi na uvunjifu wa amani,mfano tarehe 17 Julai,2013 katika toleo Namba 4774 ilichapisha habari isemayo “MISHAHARA MIPYA SERIKALINI
2013”  kwa kuchapisha waraka uliozuiliwa kwa matumizi ya vyombo vya
habari waraka huo ulikuwa wa Siri  haukupaswa kuchapishwa Magazetini.

Aidha, katika toleo la Jumamosi,tarehe 17 Agosti,2013 lilichapisha habari
yenye kichwa kisemacho “WAISLAM WASALI CHINI YA ULINZI MKALI”  habari  hiyo ilikolezwa na picha ya mbwa  mkali mwenye hasira.Habari na picha  hiyo ilitoa tafsiri ya kuwa Jeshi la Polisi lilipeleka Mbwa katika
maeneo ya ibada ya waumini wa dini ya kiislam.Jambo ambalo halikuwa la
 ukweli.

Jeshi la Polisi katika doria siku hiyo  halikupeleka mbwa katika maeneo ya Misikiti.Serikali na jeshi la Polisi  linaheshimu na kuzingatia maadili ya dini ya Kiislamu na kwa hiyo Jeshi  lake haliwezi kupitisha au kuingiza mbwa katika maeneo ya ibada.

Hivyo basi,kwa gazeti hili kuchapisha habari iliyokolezwa na picha ya mbwa ni uchochezi wa kulichonganisha Jeshi la Polisi na waumini wa dini ya
kiislam  mbwa ni najisi hapaswi kuingia  katika maeneo ya ibada.

Gazeti la MTANZANIA limefungiwa kutochapishwa kwa siku tisini(90) kuanzia  tarehe 27 Septemba,2013 kwa kuchapisha habari zenye uchochezi.Gazeti  hili limeonywa mara nyingi  lirekebishe mtindo wake wa uandishi wa   kichochezi na lizingatie maadili na Sheria na Kanuni za  fani ya
Habari.

Pamoja na kuonywa gazeti hili halikuonyesha kuzingatia  maelekezo ya Msajili wa Magazeti, mfano ;katika toleo na 7262 la 20  Machi,2013 liliandika habari yenye kichwa kisemacho “URAIS WA  DAMU”,tarehe 12 Juni,2013,toleo Namba 7344 lilichapisha makala isemayo  “MAPINDUZI HAYAEPUKIKI”.

Aidha, siku ya Jumatano,tarehe 18  Septemba,2013 katika toleo Namba 73414 ukurasa wa mbele lilichapisha  Kichwa cha habari kisemacho “SERIKALI YANUKA DAMU” taarifa hiyo  ilikolezwa na picha zilizo unganishwa kwa ustadi mkubwa kwa kutumia  kompyuta  kutapakaza rangi nyekundu mithili ya damu nyingi kumwagika  .Katika habari hiyo gazeti hilo limedai bila uthibitisho kuwa Jeshi la  Polisi linahusika  na wahanga waliomizwa na watu wasiojulikana kwa  kumwagiwa tindikali na  waliyovamiwa na kujeruhiwa vibaya.

Vile vile gazeti hilo limeishtumu serikali kuwa goigoi katika kushughulikia matukio yenye sura ya kigaidi.

Kwaujumla wake habari hiyo ni ya kichochezi ina lengo la kuwafanya
  wananchi wavichukie vyombo vya ulinzi na usalama  wavione kuwa
haviwasaidii.

Kutokana na makosa yalitajwa hapo juu serikali  imelifungia gazeti la Mtanzania  kutochapishwa kwa muda wa siku  tisini(90) kwa Tangazo la Serikali Namba 332(Government Notice No.332)  la tarehe 27 septemba,2013,. Serikali inawataka wamiliki,wahariri  na wanahabari kwa ujumla kuwa makini,kuzingatia weledi,miiko na madili  yataaluma uandishi wa habari.

Serikali inawataka wamiliki na hasa  wahariri kuhakisha kuwa habari wanazoziandika na vipindi wanavyoviandaa  vinazingatia taaluma,kuweka mbele maslahi ya taifa letu kwa kuwa na  uzalendo wa hali ya juu.

Serikali inavionya vyombo vya habari  vinavyoutumia uhuru wa habari bila wajibu kuwa haitasita kuvichukulia  hatua kali ikiwemo ya kuvifungia .Serikali haitakubali kuona vyombo vya  habari kuwa chanzo cha uvunjifu wa amani  nchini.
Imetolewa na

MKURUGENZI IDARA YA HABARI
WIZARA YA HABARI,VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO
28 SEPTEMBA,2013

"KIWANDA CHA NYUZI TABORA KINAKABILIWA NA UCHAFU WA MAZINGIRA,NI HATARISHI KWA WATUMISHI"

 

Mmoja kati ya wafanyakazi wa kiwanda cha nyuzi Tabora ambaye ni mjamzito amekutwa akifanya kazi huku akiwa amekaa chini  kulingana na mazingira mabaya ya kikazi ambapo pamoja na watumishi kudai maslahi bora lakini bado wamekuwa wakifanya kazi katika mazingira magumu.
Naibu Waziri wa viwanda na biashara Bw.Gregory Teu akimuhoji Meneja wa kiwanda cha nyuzi Tabora kuhusu uendeshaji wa kiwanda hicho ambacho kwasasa kimekuwa kikikabiliwa na mazingira yasiyostahili huku yakitishia usalama wa watumishi wa kiwanda hicho.
Mmoja kati ya watumishi wa kiwanda cha nyuzi