Sunday, April 27, 2014

RAIS KIKWETE AONGOZA SHEREHE ZA MAADHIMISHO YA MIAKA 50 YA MUUNGANO

CCM WILAYA YA TABORA MJINI WAADHIMISHA MIAKA 50 YA MUUNGANO KWA VITENDO!!!

Mjumbe wa kamati ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi wilaya ya Tabora Bw.Emmanuel Mwakasaka akibeba udongo kwa ajili ya kuwasogezea mafundi katika ujenzi wa ofisi za chama hicho kata ya Kitete ikiwa ni sehemu ya kusherehekea Maadhimisho ya miaka 50 ya Muungano.
Baadhi ya viongozi wa CCM wilaya ya Tabora ambao walishiriki shughuli za ujenzi wa ofisi za CCM kata ya Kitete
Katibu wa siasa na uenezi wa CCM wilaya ya Tabora mjini Bw.Rashid Ramadhani au maarufu Kamanda Tolu

DIWANI LUZILA ASHIRIKIANA NA WANANCHI WA KATA YAKE KUCHIMBA MITARO KWA AJILI YA HUDUMA YA MAJI SAFI


Diwani wa Kata ya Tambukareli Bw.Salumu Luzila akishirikiana na wananchi wa kata hiyo mtaa wa Nkonkole kuchimba mtaro wa kuweka bomba la maji safi kwa ajili ya wananchi wa eneo hilo ambapo Mamlaka ya Maji Safi Tabora mjini wamelazimika kuweka huduma hiyo ya maji kwa wakazi hao.

Friday, April 25, 2014

MKUU WA MAJESHI AFUTWA KAZI SUDAN KUSINI


Generali James Hoth Mai amefutwa kazi na Salva Kiir ingawa Rais huyo hajatoa sababu ya hatua yake
Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir amemfuta kazi mkuu wa majeshi yake.
Amri iliyotolewa na Rais kupitia kwa televisheni, ilisema kuwa Generali James Hoth Mai ataondolewa katika wadhifa wake mara moja.
Hata hivyo Rais Kirr hakutoa sababu ya kumfuta kazi generali huyo.
Nchi hiyo imekuwa ikikumbwa na vurugu tangu mwezi Disemba.
Wiki jana waasi waliuteka mji ulio na utajiri mkubwa wa mafuta Bentiu.
Mbali na hayo, umoja wa mataifa ulitoa ripoti iliyohusisha wapiganaji waasi na mauaji ya kikabila.
Na pia imekosoa serikali kwa kutoa taarifa za kupotosha kuhusu mauaji ya halaiki yaliyofanyika mjini Bentiu punde waasi walipouteka mji huo. Mamia wanaaminika kuuawa.
Waziri wa mambo ya nje wa Sudan Kusini,Michael Lueth, hakuwa mkweli alipowaambia wandishi wa habari kuwa wakazi waliokuwa wanatafuta hifadhi katika makao ya Umoja wa Mataifa walizuiwa kuingia katika hifadhi hiyo.
Baada ya waasi kuuteka mji wa Bentiu waliwalenga mamia ya raia wasio na hatia na ambao walikuwa wametafuta hifadhi ndani ya msikiti, kanisa na hospitali na kuwaua kwa misingi ya ukabila
Hata hivyo waasi wanaomuunga mkono makamu wa zamani wa Rais Riek Machar wamekanusha madai ya UN kuwa walihusika na mauaji ya mamia ya raia wasio na hatia huku vituo vya redio katika mji huo vikitumiwa kueneza chuki.

RAIS KIKWETE AZINDUA UJENZI WA HOSPITALI KUBWA NA YA KISASA YA CHUO KIKUU CHA AFYA NA SAYANSI SHIRIKISHI MUHIMBILI KISASA KIJIJINI MLOGANZILA

Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete na Balozi wa Korea nchini Mhe. Chung IL wakikata utepe kuashiria uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa Hospitali kubwa na ya kisasa ya Chuo Kikuuu cha Afya na Sayansi Shirikishi cha Muhimbili kijijini Mloganzila maeneo ya Kwembe, Kilometa 24 kutoka jijini Dar es salaam, baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa hospitali hiyo itakayokuwa kubwa kuliko zote nchini leo April 24, 2014.
Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete na Balozi wa Korea nchini Mhe. Chungh IL wakiweka udongo kwa pamoja wakati wa kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Hospitali kubwa na ya kisasa ya Chuo Kikuuu cha Afya na Sayansi Shirikishi cha Muhimbili kijijini Mloganzila Kilometa 25 kutoka jijini Dar es salaam, April 2014.
Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete na Balozi wa Korea nchini Mhe. Chung IL na viongozi wengine wakikata utepe kuashiria uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa Hospitali kubwa na ya kisasa ya Chuo Kikuuu cha Afya na Sayansi Shirikishi cha Muhimbili kijijini Mloganzila maeneo ya Kwembe Kilometa 25 kutoka jijini Dar es salaam, April 24, 2014.
Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi mkasi Mbunge wa Ubungo (CHADEMA) Mhe John Mnyika ili na yeye akate utepe na viongozi wengine kuashiria uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa Hospitali kubwa na ya kisasa ya Chuo Kikuuu cha Afya na Sayansi Shirikishi cha Muhimbili kijijini Mloganzila mkoa wa Pwani leo April 24, 2014.
Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiongea katika sherehe za kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Hospitali kubwa na ya kisasa ya Chuo Kikuuu cha Afya na Sayansi Shirikishi cha Muhimbili kijijini Mloganzila mkoa wa Pwani leo April 2014. 
Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akipeana mikono na Balozi wa Korea nchini Mhe Chung IL wakiwa mbele ya mchoro wa mfano wa Hospitali ya Chuo Kikuuu cha Afya na Sayansi Shirikishi cha Muhimbili kijijini Mloganzila maeneo ya Kwembe, Kilometa 25 kutoka jijini Dar es salaam, baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa hospitali hiyo itakayokuwa kubwa kuliko zote nchini leo April 2014.
Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akifurahi na msanii Mrisho Mpoto baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Hospitali kubwa na ya kisasa ya Chuo Kikuuu cha Afya na Sayansi Shirikishi cha Muhimbili kijijini Mloganzila maeneo ya Kwembe, Kilometa 25 kutoka jijini Dar es salaam, baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa hospitali hiyo itakayokuwa kubwa kuliko zote nchini leo April 2014. leo April 2014. PICHA NA IKULU

UNHWA YA KOREA KUSINI KUISAIDIA NIMR KATIKA UGUNDUZI WA DAWA KWA KUTUMIA MIMEA

 Na Father Kidevu Blog, Dar es Salaam

Taasisi ya taifa ya utafiti wa magonjwa ya binadamu Tanzania (NIMR), imesaini mkataba wa ushirikiano na kampuni ya UNHWA ya Jamhuri ya Korea ambapo kampuni hiyo itaisaidia NIMR teknolojia mpya ya kufanya ugunduzi wa dawa za binadamu kwa kutumia mimea.

Makubaliano hayo yamesainiwa jijini Dar es salaam pembezoni mwa kongamano la 28 la kisayansi la NIMR, ambapo mkurugenzi mkuu wa taasisi hiyo Dk. Mwele Malecela amesema hatua hiyo ni muhimu katika shughuli za utafiti wa afya nchini na maendeleo ya taasisi kwa ujumla.

Dk. Mwele amesema teknolojia hiyo itaongeza uwezo wa kiwanda cha taasisi cha kutengeneza dawa kwa kutumia mimea kilichopo eneo la Mabibo External jijini Dar es salaam na kwamba itawezesha taasisi kujikita zaidi katika utengenezaji wa dawa za saratani mbalimbali pamoja na za kusaidia udhibiti wa virusi vya ukimwi.

Kwa upande wake afisa mtendaji mkuu wa kampuni hiyo ya NHWA bw. YOUNG WOO JIN amesema kampuni yake imefikia hatua hiyo kutokana na mchango wa NIMR katika masuala ya tafiti na ugunduzi wa dawa ambapo ameahidi kuendelea kushirikiana na taasisi hiyo katika kiteknolojia
ili kuiongezea uwezo.

KWA MUJIBU WA JARIDA LA PEOPLE, HUYU NDIYE MWANAMKE MZURI ZAIDI DUNIANI MWAKA 2014

Lupita Nyong'o mwanamke mrembo zaidi duniani mwaka 2014.



  Jarida la People limemtangaza Mkenya Lupita Nyong’o kama mwanamuke mrembo zaidi duniani mwaka 2014.

Lupita ambaye alishinda tuzo ya Oscar kwa uigizaji wake katika filamu '12 years a slave,' yuko kwenye ukurasa wa juu zaidi wa makala ya wiki hii ya jarida hilo.

Katika orodha yake ya wanawake 50 warembo duniani,Lupita amewapiku waigizaji maarufu akiwemo Kerry Washington, ambaye pia alishiriki katika filamu hiyo na mwanamuziki Pink ambao walikuwa katika nafasi ya 10 na 5 mtawalia.

Jarida la People limemtaja Lupita kuwa mwanamke mrembo

Stacy Kiebler ambaye alisifika sana kwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na muigizaji nyota George Clooney, alishikilia nafasi ya nane.
Hatua ya Jarida la People ambalo huchapishwa kila wiki nchini Marekani na kusomwa na karibu watu milioni 40, kumkubali Lupita kama mwanamke mrembo duniani, ni kama tuzo kivyake kwa muigizaji huyo ambaye amegonga vichwa vya habari nchini Marekani tangu kushinda

Mtandao wa People.com, unasema kuwa muigizaji huyo alifurahia sana kutajwa na jarida hilo kama mwanamke mrembo hasa kwa sababu wasichana kama yeye watapata kuwa na matumaini ya kufanikiwa maishani kama yeye.

"Nimefurahi sana na hii ni fursa kuwafanya wasichana wengine wajihisi kuwa wana uwezo wa kufiia chochote maishani mwao.