Wednesday, January 14, 2015

WANANCHI WENYE HASIRA WACHOMA NYUMBA TANO ZA MTU ANAYEDAIWA KUWA NI JAMBAZI SUGU POLILSI WAWATAWANYA KWA RISASI.

NA LUCAS RAPHAEL,TABORA

 
Wananchi wa wenye hasira katika kata ya Igurubi wilayani Igunga mkoani Tabora, wameyakimbia makazi yao kwa ajili ya kukwepa kukamatwa na jeshi la polisi baada ya kutuhumiwa kuchoma nyumba tano za mtu anayedhaniwa kuwa ni jambazi sugu.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti juzi baadhi ya wananchi Richard Ngilya na Amosi Makeleja walisema kuchomwa kwa nyumba hizo tano kumesababishwa na jeshi la polisi wilaya ya Igunga kuwakamata wananchi wanane (8) wa kata hiyo huku wakiendelea kumlinda jambazi huyo.

Aidha Ngilya alidai kuwa kilichowashangaza wananchi ni kitendo kiilichofanywa na jeshi la polisi kwenda katika kata hiyo majira ya saa saba usiku pasipo kutaarifu uongozi uliopo na kuanza kuwafunguza huku wakiwalazimisha wakimama kuwaonyesha waume zao ambao hawajafanya kosa la uchomaji nyumba.

Mwenyekiti wa kitongoji cha Mwakwangu kilichopo katika kata hiyo Luhende Swala alisema askari hao waliingia katika kitongoji chake bila kumtaarifu yeye ambapo waliwakamata baadhi ya wananchi wa kitongoji hicho na kuondoka nao.

Aliendelea kusema baada ya kubebwa wananchi hao ndipo wananchi walishikwa na hasira na kujikusanya na kwenda kuchoma nyumba tatu za matembe  ambazo jambazi huyo alikuwa amewajengea ndugu zake huku idadi ya nyumba zilizochomwa zikifika tano.

Aliongeza kuwa baada ya kuchomwa nyumba hizo tatu kundi la wananchi hao lilielekea katika nyumba za baba yake na jambazi huyo kwa ajili ya kwenda kuzichoma lakini muda mfupi polisi wa kituo kidogo Igurubi walifika na kuanza kufyatua risasi za moto zilizasaidia kuwatawanya wananchi

Naye Mtendaji wa kata ya Igurubi Mdeka Said alibainisha kuwa kuchomwa kwa nyumba hizo kumetokana na baadhi ya wananchi kukamatwa na polisi kufuatia tukio la kuchomwa nyumba za jambazi huyo mwishoni mwa mwaka 2014 aliongeza kuwa hadi sasa ni nyumba tano zilizochomwa huku akifafanua nyumba mbili za bati na tatu za matembe ambapo hakutajwa thamani ya nyumba zote.

Mtendaji huyo alitaja majina ya wananchi walikamatwa Mbeshi Reuben, Shija Jilala, Ng’ombe Igoye, Masesa Pamba, Martin Charles, Lushuminkono Maige, Emmanuel Mwizamhindi, Mwandu Shusha alisema kitendo cha kukamatwa wananchi hao kimeleta mtafaruku mkubwa katika kata ya Igurubi.

Diwani wa kata ya Igurubi ,Edson Sadani alikiri kukamatwa kwa wananchi wake na kusema kuwa kitendo kilichofanywa na polisi sio cha kiungwana kwa kuwa hawakushirikisha uongozi wowote hata walipomaliza kuwakamata wananchi wake.

“Mimi kama diwani wa kata hii natambua Mahona Malendeja ni miongoni mwa majambazi ambao wamekuwa wakiisumbua kata ya Igurubi kwa kuwapora wananchi lakini cha ajabu polisi wameendelea kumlinda mtu huyo huku wakiwakamata wananchi ambao hawana hatia” alisema

Akijibu tuhuma hizo Mahona Malendeja akiwa kituo cha polisi Igunga huku akivinjari bila mashaka alisema yeye sio jambazi wala hajawahi kupatikana na shitaka lolote linalohusu ujambazi.

Alisema kilichosababisha nyumba zake kuchomwa moto ni sababu ya kumwonea wivu wa kibiashara aliongeza kuwa yeye amekuwa mfanyabiashara mkubwa anayeuza mafuta ya petrol, diesel ikiwa ni pamoja na kununua ngozi sambamba na mazao mchangannyiko ikiwa ni pamoja na kuwakopesha wananchi kwa riba.

Kwa upande kamanda wa polisi kamishna msaidizi mkoa wa Tabora Suzana Kaganda alidai kuwa yuko likizo hivyo hawezi kuzungumzia kitu chochote naomba umpigie kamanda aliyepo mimi nipo likizo.

Hata hivyo juhudi za kumpata Kaimu kamanda wa polisi Juma Bwile alisema kuwa mpaka sasa hajapata taarifa zozote zinazohusiana na tukio hilo ila anafuatilia leo.

 


MWISHO:

UKOSEFU WA KAZI KWA VIJANA NI JANGA LA DUNIA


DSC_0499
DSC_0440
DSC_0487
DSC_0481

SIKONGE WAMPONGEZA RAIS KIKWETE KWA JITIHADA ZAKE ZA KUPUNGUZA UMASKINI

 

Washiriki wa warsha ya kunusuru kaya maskini iliyoandaliwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF wilayani sikonge mkoani Tabora,wa kwanza kulia na mbunge wa jimbo la Sikonge Juma Nkumba anayefuata ni kaimu mkurungezi wa Tasaf Peter lwanda na wa kati kati ni mkuu wa walaya ya Dikonge Hanifa Selengua. aliyakaa kulia kwa mkuu wa wilaya ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Sikonge na aliyevaa suti nyeusi ni Mkurungezi mtendaji wa wilaya ya Sikonge Shadrack Mhagama

HALMASHAURI ya wilaya ya Sikonge mkoani Tabora imempongeza Rais Jakaya Mrisho Kikwete kwa jitihada na dhamira yake ya dhati ya kupambana na umaskini hapa nchini kupitia mpango wa kuzinusuru na kuziwezesha kaya maskini kiuchumi.

Pongezi hizo zimetolewa juzi na Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya hiyo Robert Kamoga alipokuwa akihitimisha warsha ya kujenga uelewa wa wadau kuhusu mpango wa kunusuru kaya maskini unaoasisiwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) awamu ya tatu.

Alisema uongozi wa Rais Jakaya Kikwete umeimarisha zaidi dhamira ya nchi kupunguza umaskini kupitia mikakati yake mbalimbali na kuboresha upatikanaji wa huduma za kijamii ambazo ni pamoja na elimu, afya na maji kwa ushirikiano mkubwa na wananchi.

‘Nachukua nafasi hii kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhesh.Dr Jakaya Mrisho Kikwete kwa uongozi wake ambao umeonyesha dhamira ya dhati ya nchi hii kupunguza umaskini wa wananchi sambamba na kuboresha huduma za kijamii’, alisema Kamoga.

Alisema kitendo cha Rais Kikwete kuzindua Mpango maalumu wa Kunusuru Kaya Maskini mnamo tarehe 15 Agosti 2012 kule Dodoma na utekelezaji wake kuanza mara moja mwezi Februari 2013 kwa azma ya kufikia jumla ya halmashauri 161 za Tanzania Bara, Unguja na Pemba kililenga kutokomeza na kundokana na umaskini katika kaya husika sambamba na utekelezaji wa miradi mingine kwa nia ya kuzipatia kaya maskini uwezo wa kujikimu.

Kamoga alibainisha kuwa madhumuni ya mpango huu wa awamu ya tatu ya TASAF ni kuwezesha kaya maskini kuongeza kipato, fursa na uwezo wa kugharamia mahitaji yao muhimu na familia zao mpango ambao utatekelezwa kwa awamu katika kipindi cha miaka 10. 

Aidha aliwakumbusha wanawarsha kuwa TASAF ni chombo cha serikali kilichopewa jukumu la kuwezesha kufikia azma ya serikali ya kupunguza umaskini kama ilivyoainishwa katika awamu ya pili ya MKUKUTA kwa kutumia dhana ya ushirikishwaji jamii.

Aliongeza kuwa tangu nchi yetu ipate uhuru miaka 50 iliyopita, serikali imekuwa ikipambana na maadui watatu ambao ni umaskini, ujinga na maradhi lengo likiwa kumwondolea mwananchi kero na vikwazo mbalimbali vya kimaendeleo.

Kamoga alieleza kuwa serikali kwa kutambua kwamba umaskini bado ni mkubwa miongoni mwa jamii hasa kule vijijini, ndio maana imeandaa Mpango huu wa Kunusuru Kaya Maskini ili kufikia malengo yake iliyoazimia katika Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini Tanzania (MKUKUTA ) awamu ya pili.

Awali akizungumza katika warsha hiyo Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF Bw.Peter Luanda alisema mpango huo wa kunusuru kaya maskini umelenga kuzinufaisha kaya masikini zilizo katika hali duni kule vijijini na katika mitaa mbalimbali hususani watoto wenye umri chini ya miaka 5 na wanaosoma shule na akina mama wajawazito.

 Alisema kaya hizo zitanufaika kwa kupewa ruzuku za aina mbili moja ni ruzuku ya msingi itakayotolewa kwa kaya maskini iliyomo kwenye mpango huo na ruzuku ya pili walengwa ni wale wanaotakiwa kutimiza masharti ya elimu na afya ili waweze kupatiwa huduma za elimu na afya bure.

Akizungumza baada ya warsha hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya Sikonge Shadrack Mhagama alipongeza ujio wa mpango huo wa TASAF wa kunusuru kaya maskini na kuongeza kuwa utasaidia kuboresha maisha ya wananchi wake kwani wengi wao wamekuwa wakishindwa kuchangia hata shughuli za maendeleo kutokana na kuwa na hali duni.

SERIKALI YATAKIWA KUKOMESHA UBABE KWENYE UKEKETAJI


DSC_0300
DSC_0480
DSC_0492
DSC_0433
DSC_0425
DSC_0495
DSC_0504
DSC_0547
DSC_0499
DSC_0555
DSC_0541
DSC_0617
DSC_0585
DSC_0630
DSC_0557
DSC_0702
DSC_0552
DSC_0599