Wednesday, March 5, 2014

"RASIMU YA KATIBA NDIO NINI?"-WAUZA VITUMBUA


Salma Abas  ambaye ni mpishi na muuzaji wa vitumbua Stendi mpya ya mabasi Tabora mjini,wakati alipokuwa akizungumza na Mwandishi wetu kuhusu ufahamu wake juu ya RASIMU  YA KATIBA MPYA ambapo alisema yeye pamoja na washirika wenzake wanaofanya biashara ndogo ndogo hawajui chochote wamekuwa wakisikia tu kwenye vyombo vya habari na tena wanaona mambo hayo ya Rasimu yanawahusu zaidi viongozi na si kwa wao......."Mara tusikie wapo Bungeni huko Dodoma wanataka waongezewe pesa eti laki tatu kwa siku haiwatoshi kwa kujadili hiyo Rasimu kwani ndio kitu gani?...na sisi Wauza vitumbua itatusaidia nini?Baadhi ya Wauza vitumbua hapa Stendi mpya ya mabasi ndivyo walivyo na uelewa huo juu ya Rasimu ya Katiba mpya......SWALI LA MSINGI :-Itakapofikia hatua ya kupigia kura Katiba hiyo nini watafanya watu kama hawa?   

No comments:

Post a Comment