Tuesday, April 16, 2013

ALIYEIGIZA FILAMU YA THE PASSION OF CHRIST, MAMBO SI MAZURI HOLLYWOOD


Taarifa hii ni kwa hisani ya Gospel Kitaa...

Haya msomaji wetu wa Gospel Kitaa karibu katika kipengele chetu cha ''KWA TAARIFA YAKO'' ambacho kinakujia kila siku za alhamisi ndani ya GK kikiwa na lengo la kukupatia habari ambayo iliwahi kutukia lakini yawezekana huijui pia yawezekana ilitukia ukawa unaijua lakini GK ikawa imesahau mahali au kuna sehemu haina usahihi utapata fursa ya kusahihisha kwa kuweka comment yako chini kabisa kwenye habari husika. Karibu


Leo katika kipengele chetu ni kwamba mwigizaji wa Hollywood aliyeigiza filamu ya "The Passion of Christ" ambayo ilipokewa kwa hisia tofauti ikiwemo watu kuripotiwa kufariki dunia mara walipoitazama na baadhi ya Wayahudi kuiponda namna walivyoigizwa, bwana Jim Caviezel amesema tangu aigize filamu hiyo mambo yake hayako sawa ndani ya mji wa Hollywood kutokana na kutopewa tenda za kutosha za ugizaji na kwamba hata zinapokuja sehemu anayotakiwa kuigiza haziendani na utaalamu au kiwango chak

Jim ambaye ni Mkristo Mkatoliki pamoja na mkewe, amesema licha ya filamu hiyo kuuza zaidi ya nakala milioni 400 lakini mambo si shwari kwake kwakuwa hapewi tena nafasi ya kuigiza lakini amesema alishapewa onyo na muongozaji wa filamu hiyo Mel Gibson ambaye alimwambia uamuzi wake wa kutaka kuigiza nafasi ya Yesu katika filamu hiyo utamfanya kutoigiza tena katika Hollywood na kufikia tamati ya uigizaji wake,muigizaji huyo alimjibu akisema kila mmoja atabeba msalaba wake, kwasababu anakiamini kile anachotaka kukifanya hivyo kila mmoja abebe msalaba wake lasivyo uzito wake utatudondokea wenyewe tusipoibeba kwahiyo achana na hayo twende tufanye kazi.

Aidha mwigizaji huyo amekiri kuwa alijua fika kwamba kuigiza nafasi ya Yesu katika filamu hiyo ilikuwa ni kuiweka uigizaji wake matatani lakini hakujali hilo na kuamua kuigiza huku muongozaji wake bwana Gibson amewahi kushutumiwa na watu mbalimbali kuhusu mwenendo wake ikiwemo suala la ulevi jambo ambalo Jim amesema watu waache kuhukumu kama wameona Gibson ni mtenda dhambi jambo wanalotakiwa kufanya ni kumuombea ili aache nasio kumuhukumu. Ameongeza kwamba imani yake ndio muongozo wake binafsi na katika utaalamu wake katika uigizaji.

Jim akipata maelezo kutoka kwa Mel Gibson wakati wakirekodi filamu hiyo.
KWA TAARIFA YAKO tangu kutoka kwa filamu hiyo mwaka 2004 hadi leo hii mwigizaji huyo ameigiza katika tamthilia na filamu nyingine ambazo hata hivyo kwa mtazamo wmingine ni kwamba labda angepata kazi nyingi zaidi. Lakini hata hivyo mwigizaji huyo ametoa kazi yake mwenyewe ya sauti hivi karibuni aliyoipa jina "Words of Promise" Ikiwa ni biblia waliyoweka kwa njia ya sauti akiwashirikisha waigizaji wenzake. Hata hivyo licha ya mambo ya uigizaji Hollywood kutokuwa kama alivyotegemea lakini kwasasa anaonekana kukaza msuli zaidi katika utumishi wa kidini kwakuzungumza kwenye makongamano na mambo mengineyo... Kwahiyo hakijaharibika kitu

No comments:

Post a Comment