Tuesday, April 16, 2013

HAKIMU KIZIMBANI KWA RUSHWA

 
 Na Lucas Raphael,Tabora



TAASISI ya kuzuia na kupambana na rushwa,(TAKUKURU),mkoani Tabora imemkamata na kumfikisha mahakamani  hakimu mkazi wa mahakama ya wilaya ya Urambo,Oscar Bulugu kwa tuhuma tatu za kuomba na kupokea rushwa ya shilingi milioni tano.



Mbele ya hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama ya mkoa Issa Magoli ilidaiwa na mwanasheria wa Takukuru Simon Mashingia kuwa mtuhumia alitenda makosa hayo kati ya tarehe 15 marchi na 22 mwaka huu huko wilayani Urambo.



Upande wa mashitaka ulidai kuwa march 15 mwaka huu mtuhumia akiwa ni hakimu wa mahakama ya wilaya ya Urambo alimshawishi Lucas Raymond Changala ampe fedha hizo ili aweze kumpa dhamana ndugu yake aliyekuwa anakabiliwa na kesi ya wizi wa fedha za benki ya NMB.



Mashingia alidai katika shitaka la pili kuwa tarehe 18/03/2013 hakimu huyo ambaye ni mtuhumiwa alipokea  shilingi milioni moja toka kwa Changala kama malipo ya awali ili aweze kumpa dhamana Phillipo Raymond aliyekuwa mtumishi wa benki ya nmb anayetuhumiwa kuiba zaidi ya shilingi milioni mia moja.



Mwanasheria huyo wa Takukuru alidai katika  shitaka la tatu kuwa tarehe 21/03/2013 mtuhumiwa huyo alipokea tena shilingi milioni moja ikiwa ni endelezo la malipo aliyoomba aweze kumpa dhamana mtumishi huyo wa nmb.



Hakimu huyo baada ya kusomewa mashitaka hayo matatu yote alikana na yuko nje kwa dhamana na kesi hiyo imepangwa kutajwa tena 14/05/2013.



Cha kushangaza mahakama ilimwamuru mtuhumiwa huyo kujidhamini mwenyewe kitendo ambacho kiliwashangaza watu waliokuwepo mahakamani hapo.



Mwisho.


No comments:

Post a Comment