Wednesday, May 8, 2013

SERIKALI YAWATAKA VIONGOZI KUWA NA NIDHAMU MAHALI PAKAZI

Na Lucas Raphael ,Siginda




SERIKALI imewataka viongozi wa kada mbalimbali pamoja na wananchi kuwa na nidhamu na uwajibikaji mahali pakazi ili iwesehemu kubwa ya mabadiliko ya kimaendeleo ya kiuchumi na sayansi na Teknolojia hapa nchini.

Hayo yamesemwa na Waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu Ubinafisishaji na uwekezaji Dkt,Merry Nagu wakati akifunga mkutano wa kuhamasisha matumizi ya sayansi na Tekinolojia kwa kuleta maendeleo ya kiuchumi kanda ya kati singida.

Alisema Serikali imelenga kukuza uchumi kwa wafanya Biashara wakubwa na wadogo kupitia sayansi na Tekinolojia ikiwa na kuzingatia nidhamu na uwajibikaji mahali pakazi.

Alisema kuwa baadhi ya viongozi hawatambui wajibu wao kwa kukosa ni dhamu na uwajibikaji mahali pakzi badala yake husababisha miradi mingi ya kimaendeleo kudorola.

Alesema viongozi wanapaswa kujitambua na kujua uwepo wao katika nafasi husika ili waweze kutekeleza kero za wananchi ikiwa na kuleta maendeleo dhabiti kwa maeneo husika.

Alisema kuwa Baraza la Biashara Tanzania (TNBC) linahakikisha mikutano hiyo inaendelea kupitia makundi mbalimbali ikiwepo na ngazi za mikoa,wilaya na kata lengo likiwa ni kuhamasisha wananchi watumie sayansi na tekinolojia katika kukuza uchumi wa ndani nje.

Waziri Nagu alisema kuwa yote hayo yanatokana na nidhamu kwa viongozi,wadau pamoja na uwajibikaji mahali pakazi ilikuweza kufikia malengo hayo.

Alisema Baraza la Biashara Tanzani TNBC limeweka malengo kuwa ifikapo mwaka 2025 litafikia malengo hayo ya kukuza uchumi kwa watanzania hususani wajasilia mali wa dogo na wa kubwa na kuondokana na umasikini.

Alisema Baraza hilo limeweka vipaumbele vitavyo changia kukuza uchumi huku vikiendelea kufanyiwa malekesho ilikufikia malengo hayo ni pamoja na upatikanaji wa maji safi,Kilimo na mifugo,miundombinu ambayo ni Barabara,Reli na Bandari lengo likiwa ni kuimalisha miundombinu hiyo.

Vipaumbele vingine ni pamoja na kuimalisha nisharti na madini ilikuweza kukuza uzalishaji,ukusanyaji madhubuti wa mapato ya ndani na je pamoja na kutoa elimu mbadala kwa wananchi dhidi ya miradi husika.

Kwaupande wake kamishina  msaidizi,mwandamizi wa polis makao makuu Dar es salaam Lucas Kusima akiwasilisha maada ya umuhimu wa usalama wa watu na mali zao katika mageuzi ya kiuchumi ya sayansi na tekinolojia kwa jamii.

Alisema kuwa jeshi hilo limejipanga kukabiliana na majambazi yanayotumia Tekinolojia  hiyo ikiwepo na huduma ya kibenki A T M,Simu za kiganjani,mitandao ya kijamii pamoja na mitandao mingne.

Kusima amewataka wananchi kutoa ushirikia wa kutosha kwa wahalifu hao kupitia Teknolojia za mawasiliano ilikuweza kukuza uchumi huo na kuimalisha ulinzi na usalama kwa mali za wananchi ikiwa na wananchi kwa ujumla.

Mkutano huo wa kuhamasisha matumizi ya sayansi na tekinolojia kwa kuleta maendeleo ya kiuchumi umeyakutanisha makundi mbalimbali wakiwepo wakuu wa wilaya,wakurugenzi wa halmashauri za wilaya na mikoa pamoja na wakuu wa mikoa kwa mikoa mitatu ikiwa ni Singida,Tabora na Dodoma.

Mwisho.

No comments:

Post a Comment