Tuesday, February 11, 2014

"MAMA ASHAURIWA AMPE SUMU MTOTO WAKE MLEMAVU,AKAA NDANI KWA ZAIDI YA MIAKA KUMI NA MOJA"


Mtoto Tatu Hassan akiwa na mama yake mzazi Bi.Halima Mgelwa,mtoto huyu amekuwa kitandani kwa zaidi ya miaka kumi na moja kutokana na maradhi ya kichwa huko katika kijiji cha Magiri wilayani Uyui mkoani Tabora. 
Mama wa mtoto huyu anaomba msaada wa matibabu kwa wasamalia wema,tatizo kubwa kichwa cha mtoto huyu kimejaa maji na hivyo anahitajika kupelekwa hospitali ya Bungando jijini Mwanza.
Mama huyu kwa mujibu wa maelezo yake amekuwa akilazimika kumfungia ndani ya nyumba kila siku na kwenda kutafuta riziki kwa muda wote huo wa miaka kumi na moja na hivyo hata baadhi ya majirani zake wa karibu hawatambui kama kuna mtoto huyu hapo kijijini.Jambo baya zaidi baadhi ya watu wenye imani  potofu walithubutu kumshawishi mama huyu aweze kumpa SUMU mtoto wake eti kwa madai kwamba amekuwa akihangaika sana kumuhudumia.

No comments:

Post a Comment