Friday, July 18, 2014

BENKI YA EXIM YAFUNGUA MILANGO KUSAIDIA MICHEZO KWA VIJANA TABORA

Meneja masoko wa Benki ya Exim Jeremia Majebele akikabidhi cheti cha mafunzo ya ualimu wa mpira wa miguu ngazi ya kati kwa mmoja wa wahitimu wa kozi hiyo ya siku 14  ambaye pia ni afisa wa Jeshi la Polisi Tabora mjini Hussein Juma Katanga
Meneja masoko wa Exim tawi la Tabora Jeremia Majebele akifunga mafunzo hayo ambapo alisema  kuwa Benki ya Exim inaunga mkono juhudi za kuibua michezo mkoani Tabora na kuahidi kuwa ipo tayari kusaidia michezo kwa vijana.
Mwenyekiti wa chama cha soka mkoa wa Tabora Yusuph Kitumbo akizungumza wakati wa kufunga mafunzo ya walimu wa soka mafunzo yaliyokuwa yakifanyika katika uwanja wa Ali Hassan Mwinyi
Mkufunzi wa mafunzo hayo ya walimu wa soka Meja mstaafu Omari Mingange akitoa maelezo mafupi wakati wa hafla ya ufungaji mafunzo hayo
Mwenyekiti wa chama cha soka mkoa wa Tabora Yusuph Kitumbo akipeana mkono na Meneja Uendeshaji  huduma wa Benki ya  Exim Philip Metusela na Meneja masoko  wa Exim Jeremiah Majebele  akisalimiana na Mwenyekiti wa Chama cha Makocha mkoa wa Tabora TAFCA Mohammed Mozi muda mara baada kukamilika kwa hafla fupi ya kufungwa kwa mafunzo hayo.
Picha ya pamoja wahitimu wa mafunzo ya ualimu wa soka,viongozi wa chama cha mpira wa miguu mkoa wa Tabora TAREFA,TAFCA pamoja na maafisa kutoka Benki ya Exim hali inayoonesha ni jinsi gani Exim ilivyo karibu na wadau wa michezo.


 

No comments:

Post a Comment