Friday, February 6, 2015

WAZIRI WA UJENZI AKAGUA BARABARA MKOANI KATAVI


Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akiagana na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Eng. Stella Manyanya mara baada ya kukagua barabara za mkoa wa Rukwa.

Mkuu wa Wilaya ya Mlele Col.Ngemela Eslom Lubinga akisoma taarifa ya mafanikio ya Serikali ya wilaya hiyo  kwa Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli.
Sehemu ya barabara ya Sumbawanga-Kanazi km 75- ambayo ujenzi wake umekamilika kwa zaidi ya asilimia 60.
Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akiimba pamoja na wanafunzi wa shule ya msingi Wilayani Nkasi mara baada ya kuwasalimia alipokuwa njiani kukagua mradi wa barabara unaopita  karibu na shule hiyo.
Sehemu ya barabara ya Sumbawanga-Matai-Kasanga km 112 ambayo ujenzi wake unaendelea kujengwa kwa kiwango cha lami.
Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akiwahutubia wakazi wa Kibaoni kuhusu kuwasimamia makandarasi wanaojenga barabara za Kanazi-Kizi-Kibaoni kwa kiwango cha lami.
Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akiagana na wakazi wa Kibaoni Wilayani Mlele katika mkoa wa Katavi.
Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akiwa na Mama mzazi wa  Waziri Mkuu Mheshimiwa Mizengo Pinda nyumbani kwake Kibaoni mkoani Katavi. Waziri wa Ujenzi alipita kumsalimia mara baada ya kuwahutubia wakazi wa Kibaoni kuhusu masuala mbalimbali ya barabara na nyumba za Serikali.
Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akihutubia mamia ya wakazi wa Katavi kuhusu miradi mikubwa ya barabara katika mkoa huo.
Waziri wa Ujenzi akiagana na wananchi wa Katavi mara baada ya kuwahutubia.Picha zote na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Wizara ya Ujenzi.

No comments:

Post a Comment