Wednesday, November 27, 2013

KADA AKINUSURU CCM KWA KUWACHIMBIA KISIMA WANANCHI,WALICHOSHWA NA AHADI HEWA

 
Baadhi ya  viongozi  wa CCM wilaya ya Tabora mjini wakiangalia kisima cha maji ya kunywa kinachotumiwa na wakazi wa kijiji cha Kabila manispaa ya Tabora ambapo licha ya kupiga kelele kwa Serikali lakini tatizo la maji bado limeendelea kuwa sugu.
Mama akichota maji ya kunywa katika moja ya kisima ambacho kinategemewa na idadi kubwa ya wanakijiji cha Kabila,ambapo hutumia zaidi ya saa tisa kusubiri maji hayo yanayotiririka katika kisima hicho na kusababisha muda mwingi kutumika kutafuta maji badala ya shughuli nyingine za kiuchumi.Hata hivyo pia imeelezwa kuwa baadhi ya wanawake wamejikuta ndoa zao zikiwa matatani kutokana na adha hiyo ya kutafuta maji.  
Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Tabora mjini Bw.Moshi Abrahamu NKONKOTA akikata utepe ikiwa ni ishara ya kuzindua kisima cha maji kilichojengwa kwa ufadhili wa Mjumbe wa kamati kuu ya CCM wilaya ya Tabora Bw.Emmanuel Adamson Mwakasaka ambaye aliguswa na tatizo hilo la maji akaamua kushirikiana na wananchi katika kijiji cha Kabila la kuchimba kisima hicho.
Hapa kinamama hawa wanaonesha kufurahia huduma hiyo ya maji ya kisima baada ya kusumbuka kwa muda mrefu,huku Serikali ikitumia zaidi ya shiringi Milioni 360 kueneza huduma ya maji ambayo hayakuweza kupatikana mpaka sasa.
Wananchi wa kijiji cha Kabila wakiwasikiliza viongozi wa CCM baada ya kuzinduliwa kwa huduma ya maji ya kisima na kuahidi kuendelea kukipa ushirikiano chama hicho ambacho walianza kukisusa kutokana na ahadi hewa zilizokuwa zikitolewa na viongozi wake. 

No comments:

Post a Comment