Wednesday, November 27, 2013

"MBUNGE ALIYESHINDWA KUTEKELEZA AHADI ZAKE APIGWE CHINI 2015,TUSIMUONEE AIBU ANATUHARIBIA CHAMA"-CCM

Mwenyekiti mstaafu wa CCM mkoa wa Tabora Bw.Juma Samwel Nkumba akizungumza na baadhi ya  wananchi wa mjini Tabora kata  ya  Mtendeni  ambapo  alisisitiza kuwa makini wakati wa uchaguzi mkuu wa 2015,kuchagua viongozi ambao wapo karibu na wananchi wakisaidia kukabiliana na changamoto mbalimbali na si kuchagua viongozi hususani Wabunge ambao hawana muda wa kukaa karibu na wananchi waliowapigia kura na hivyo kuwataka wawapige chini  ambao waliahidi ahadi kibao wakati wa kuomba kura na mara baada ya kuchaguliwa wamekuwa hawataki kusogea karibu na wananchi,jambo ambalo limekuwa likishusha heshima ya CCM kwa wapiga kura. 
Mjumbe wa halmashauri kuu ya CCM wilaya ya Tabora mjini Bw.Emmanuel Mwakasaka akizungumza katika hafla fupi ya shukrani ya  diwani wa kata ya Mtendeni Bw.Ngalu,...Katika hotuba yake Bw.Mwakasaka alitumia fursa hiyo kusisitiza juu ya umuhimu wa kukiimarisha CCM kabla na baada ya uchaguzi jambo ambalo limekuwa likipigwa vita na baadhi ya Viongozi wa CCM  ambao wanashindwa kuwa karibu na wananchi na kufanya mikutano ya mara kwa mara itakayosaidia kukijenga Chama hicho.Aidha ameongeza kusema kuwa ni vema wanaCCM wakajenga mazingira ya ushirikiano utakaowawezesha kuwatumikia wananchi waliokipatia ridhaa  chama hicho kuongoza dola badala ya kuendelea na marumbano yasiyo na tija hasa wakati huu ambao uchaguzi umekwisha kilichobaki ni kutekeleza ilani ya chama hicho.
Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Tabora  mjini Bw.Moshi Abraham  maarufu  Nkonkota naye alipata fursa ya kuzungumza katika hafla hiyo ambapo pamoja na mambo mengine Mwenyekiti  huyo alisema kuwa kwasasa Chama hakina nafasi ya kumuonea aibu kiongozi yeyote aliyeshindwa kutekeleza ahadi zake kwakuwa jambo hilo litaendelea kukichafua CCM mbele ya wananchi....Nkonkota aliongeza kuwa  nia ya CCM ni kutaka kutoa huduma bora kwa wananchi waliowachagua na kamwe hakita kubali kumkumbatia kiongozi anayeshindwa kutekeleza majukumu yake kama alivyoahidi na kubwa zaidi CCM itakuwa macho kuangalia mtu anayekubalika kwa wananchi na si kuwalazimisha wachague kiongozi mjanja mjanja wakati wa uchaguzi mkuu wa 2015 utakapowadia.   

No comments:

Post a Comment