Thursday, May 8, 2014

MWANAMKE AKAMATWA AKIMILIKI BUNDUKI ISIVYO HALALI -TABORA



Kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora ACP Suzan Kaganda.
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI TAREHE 05/05/2014.
Ndugu waandishi wa habari, Jeshi la Polisi mkoa wa Tabora ifuatayo ni taarifa ya tukio moja la kifo na taarifa ya  Operesheni inayoendelea katika wilaya zote za mkoa wa Tabora. Ambapo kufuatia operesheni hizo tulifanikiwa kukamata watuhumiwa wa makosa mbali mbali kama ifuatavyo:-


Mnamo tarehe 04.05.2014 majira ya saa 10:00hrs huko eneo la Utwigu wilaya ya Nzega FRANCE S/O AMBROSE HUSSEIN 11yrs, Mnyamwezi mwanafunzi wa darasa la Tano katika shule ya Msingi Mwanhala alifariki dunia baada ya kutumbukia katika bwawa la maji ambapo alikuwa ameenda kwa ajili ya kuogelea.


Tarehe 01.05.2014 huko wilaya ya Nzega alikamatwa FROLA D/O SHIJA, 28yrs, mnyamwezi, mkulima na mkazi wa kujiji cha Igalula akiwa na bunduki aina ya Gobore ambayo anamiliki kinyume na sheria. Mtuhumiwa amefikishwa mahakamani.


Aidha tarehe 02.05.2014 huko katika eneo la Utwigu kata ya Nyasa wilaya ya Nzega walikamatwa SHIJA S/O KAPONA, 39yrs, Mnyamwezi, Mkulima na BAHATI S/O SHIJA, 28yrs, wote wakazi wa Utwigu wakiwa na vipodozi aina ya Lemon Vate Cream 02, Beater Soap 02, Deproson chupa 15, Demason 01, na Banistar 01, vipodozi hivyo vilibainika kuwa havifai kwa matumizi ya binadamu na mtaalam kutoka TFDA. Watuhumiwa wote wamefikishwa mahakamani.


Katika opereheni hii pia wamekamatwa PILI D/O BUNDALA 65yrs, Mnyamwezi, MACHIBYA S/O MGETE 40 yrs, Mnyamwezi, KULWA S/O MASANJA, 35yrs, Msukuma, DAUDI S/O KABOGA 28yrs, Msukuma, MWAJUMA D/O RAJABU, 30yrs, Mnyamwezi, na MWASITI D/O MUHOJA 37yrs, wote wakazi wa kata ya Nyasa – Nzega wakiwa na Pombe ya moshi lita 15, pia watuhumiwa wote hawa ni watumiaji na wauzaji wa pombe hiyo haramu. Wote wamefikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili.


Jeshi la Polisi linazidi wito kwa wananchi kuendelea kushirikiana na Jeshi lao ili kukomesha na kutokomeza vitendo vyote vya uhalifu na kuwafichua wahalifu, aidha wazazi napenda kuwakumbusha wazazi kuwaangalia watoto na kuwafuatilia katika michezo yao ya kila siku, pia napenda kuwaasa wananchi kufuata sheria za nchi na pia kwa wale wote ambao wanamiliki magobore kinyume na sheria wasalimishe magobore hayo kwa kuwa operessheni hii ni endelevu.

Imetolewa na :-

SUZAN KAGANDA – ACP

KAMANDA WA POLISI

MKOA WA TABORA.

No comments:

Post a Comment