Monday, May 12, 2014

VIONGOZI WA DINI WATAKIWA KUJIENDELEZA KI ELIMU





 NA LUCAS RAPHAEL,NZEGA

VIONGOZI WA Dini  mbalimbali  hapa nchini wametakiwa  kujiendeleza kiEleimu  wasilizike  na Elimu waliyo nayo kutokana na mabadiliko ya kisayansi na Teknolojia nayo jitokeza hivi sasa katika Nyanja mbalimbali za kijamii ikiwa na kiu Tamaduni.

Kauli hiyo imetolewa na Askofu Mkuu wa Kanisa la Eangelistic Assemblis of God Tanzania(EAGT) Stephano Nzowa  wakati wa sherehe za  Kuwatunuku Udakitari wa Falisafa PHD  Askofu Emmanuel  Shani na mkwe Hosena Chales katika Viwanja vya kanisa hilo wilayani Nzega Mkoani Tabora.

Amepata PHD  hiyo katika Chuo Kikuu cha Africas  Graduate University  kutoka  Nchini   Senegal  na  Bregedia General Dk,Timothy  Kasembe  mbele ya  waumini wa kanisa hilo.

Dk,Nzowa alisema kuwa  Elimu ni Bahari pana  ambayo inapaswa kila mtu kuogerea humo kwani  bila Elimu hakuna maisha hivyo kila nyakati yapaswa kupata nafasi ya kujifunza kwa bidiii.

Askofu Nzowa alisema viongozi wa makini hususani wachungaji na maafisko wanapaswa kusomea Elimu mbalimbali ikiwemo ya kidini ili waweze kukabiliana na mabadiliko  ya kisanyans na Teknolojia katika jamii mbalimbali.

Alisema kuwa Viongozi wa Dini wakisoma wataweza kubadilisha Jamii inayo wazunguka kupitia Elimu hiyo na kuongeza kuwa jamii imebadilika kwa kias kikubwa tofauti na hapo zamani.

Alisema kuwa suala la Elimu limeelezwa katika vitabu vya mungu kwa nyamba mbalimbali hivyo Viongozi wa kidini wanapaswa kuyatenda hayo iliwaweze kufikia malengo kwa Nyanja mbalimbali kadri uwe zavyo.

Dk,Askofu Mkuu wa kanisa hilo Stephan Nzowa aliwataka Vijana kuiishika Elimu kama walishikavyo neon la Mungu iliwaweze kufikia malengo yao ya kimaisha ikiwa na kufanya mambo mema kwa jamii inayo wazunguka.

Alisema kuwa jamii ya watu waliosoma hufanya matendo mema kwa wananchi ikiwa na kuendeleza mema na kupinga mabaya kama maandiko yanavyo sema dhidi ya suala hilo la Elimu.

Mara baada ya kukabidhiwa Cheti cha udakitari wa Falisafa PHD Dk,Askofu Emmanueli Shani aliwataka wazazi na walezi kufanya juhudi kupeleka watoto shule ikiwa na kusimamia maendeleo ya wanafunzi iliwaweze kufikia malengo.

Akizungumzia mchakato wa kupata Elimu Dk,Emmanueli Shani  alisema kuwa suala la Elimu lina changamoto nyingi katika kufikia malengo na kuwataka wazazi na walezi kuvumilia changamoto hizo iliwaweze kufikia malengo husika.

Baadhi ya waumini wa kanisa hilo walisema kuwa Elimu nikitu muhimu katika maisha ya mwanadam hivyo wananchi na jamii kwa ujumla inapaswa kujikita katika kuendana na mazingira husika ili kuweza kuleta mabadiliko makubwa.

Alisema kuwa Elimu ya sasa ni ile ya chuo kikuu na vyuo mbalimbali ikiwa na kusomea fani furani ambayo itaweza kukutoa sehem moja hadi kukufikisha sehemu nyingine ya kimaisha ikiwa na kuisaidia jamii husika.

Mwisho.

No comments:

Post a Comment