Sunday, June 15, 2014

CHAMA CHA WALIMU WAUOMBA MFUKO WA BIMA YA AFYA KUSAIDIA HUDUMA YA MENO YA BANDIA KWA WALIMU


Katibu wa Chama Cha Walimu CWT mkoani Tabora Bi.Romana Aloyce Mnyoni akichangia katika majadiliano ya Mkutano wa wadau wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya uliofanyika katika ukumbi wa Isike Mwanakiyungi ambapo alichangia kwa kuuomba mfuko huo kusaidia kulipa huduma za matibabu ya meno kwa Mwalimu atakayepata tatizo la kung'oka meno ili kumsaidia aweze kutamka maneno kwa ufasaha mbele ya wanafunzi wakati wa kufundisha.
Bw.Andrew Karyome Mwenyekiti wa Bodi ya Afya wilaya ya Uyui akichangia mjadala katika mkutano huo wa wadau wa Bima ya Afya NHIF mkoani Tabora.
Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi NHIF Bi.Lyidia Choma akijibu maswali ya wadau wa mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya mkoani Tabora wakati wa mkutano huo.
Wadau wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya mkoani Tabora



No comments:

Post a Comment