Sunday, June 15, 2014

WLF YAOKOA VIFO VYA WAJAWAZITO UKANDA WA ZIWA KIGOMA




IMEELEZWA kuwa,vifo vya kina mama wanaojifungua katika ukanda wa ziwa Tanganyika  Mkoa wa Kigoma vimepungua kutokana na uboreshaji wa huduma ya upasuaji wa dharura katika kituo cha afya cha Buhingu,ambacho awali kilikuwa kiwanda cha vifo hivyo.
 
Akifafanua hilo mbele ya wandishi wa habari kigoma Ujiji  Mtaalamu Magonjwa ya kinamama Dr.Calist Nzambuhakwa alisema awali wanawake wajawazito walikuwa wakihofu kubeba mimba, kutokana na kuzorota kwa huduma hiyo ambapo  kati ya wajawazito 578 kati ya vizazi hai 100,000 walikuwa wakipoteza maisha wakati wa kujifungua 2009-2013.
 
“kumsafirisha mama mjamzito kwenye boti la mbao la abiria ni hatari, na kutoka kituo cha buhingu hadi hospitali  ya rufaa Maweni kigoma mjini masaa 18 ,kifo kwa wenye uzazi pingamizi , wanaovuja damu na  kifafa cha uzazi hali ilikuwa tete,ndo mana kituo kile kiliitwa kiwanda cha kifo kwa wajawazito” alibainisha Dr.Nzimbahukwa.
 
Alisema Mradi wa Afya ya Uzazi wa shirika la World  Lung  Foundation wamekidhi kuondoa idadi ya vifo kwa wahanga hao, kutoka vifo 12 kwa mwaka 2012 hadi  vifo 2 kwa mwaka 2013  kati ya vizazi hai  1000 .
 
Kwa  upande wa wawakilishi wa Mradi wa World Lung Foundation Victoria Marijani na Dr.Ngukie Mwakatundu kwa nyakati tofauti walisema mradi wao umelenga wilaya  ya Kigoma ,Kasulu,Kakonko  kwa kutoa vifaa tiba na mafunzo elekezi kwa wahudumu katika  vituo mtambukwa tisa kikiwemo kituo cha Buhingu.
 
Walisema  huduma yao imeokoa  vifo vya uzazi pingamizi  171 kwa  wanawake waliojifungua kwa njia ya kisu mkoani hapa na kuahidi kutumia tathimini zao  kujenga majengo bora ya mapumziko ya kinamama wajamzito  kutoka vijiji vilivyopo mbali na vituo vya afya,kwa lengo la kuokoa maisha ya mama na mtoto  Huku wakiitaka serikali ichangie katika hilo.
 
Naye Mganga Mkuu huo  alisema 80% ya damu salama inatumika kwa wakina mama na watoto,ambapo changamoto kubwa ya vifo hivyo ni kuvuja damu kwa mlengwa  wakati wa kujifungua ambapo vifo 68 katika vizazi hai 100,000 na kudai kuwa, hali hiyo itakwisha endapo jamii itaendelea na hulka ya kutoa damu kwa hiari .
 
Alisema lengo la serikali na wadau wa afya ni kuboresha huduma za wahanga hao,ambao ni chachu ya maendeleo ya nchi ,Huku akiwaonya wahudumu wanaouza damu kwa wahanga hao na wananchi kwa ujumla,ambapo kisheria ni kosa kuuza damu.
 
Aidha aliwataka wandishi wa habari wajikite kutoa elimu ya umuhimu wa kutoa damu kwa hiari ,ambapo serikali kwa kushirikiana na wadau hao wanajenga kituo cha kukusanyia damu salama mkoani hapo, kutokana na mwitikio wa umma husika kuchangia asilimia 114 ya damu  salama .

No comments:

Post a Comment