Sunday, June 15, 2014

UTUMIKISHWAJI WATOTO KWENYE MASHAMBA YA TUMBAKU WILAYANI SIKONGE NI ASILIMIA 48.4


Baadhi ya Watoto wa Shule ya Msingi Udogo wilayani Sikonge wakifanya maandamano wakati wa Sherehe ya Siku ya kupinga utumikishwaji watoto iliyofanyika wilayani humo iliyoandaliwa na Mradi wa Prosper ambao unashughulikia kuondoa ajira mbaya kwa Watoto.
Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Sikonge Bw.Robert Kamoga akizungumza katika sherehe za Siku ya kupinga utumikishwaji watoto ambapo aliwataka wazazi na wananchi kwa ujumla kuacha tabia ya kuwatumikisha watoto na badala yake kuwapa muda mwingi na kuwawezesha kielimu.
Mkurugenzi wa Mradi wa Prosper Bw.Bahati Nzunda akitoa taarifa ya utekelezaji wa mradi huo kwa kipindi cha muda wa miaka minne pamoja na changamoto wanazokabiliana nazo katika kumkomboa mtoto na ajira mbaya hasa katika mashamba ya tumbaku.

Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Sikonge Bw.Robert Kamoga akisalimiana na wanamichezo wa mpira wa pete wa Shule ya msingi Udongo.
Wachezaji wa ngoma ya asili  RADU wakionesha vitu vyao wakati wa Sherehe hizo za Siku ya kupinga ajira mbaya kwa watoto.

No comments:

Post a Comment