Wednesday, December 17, 2014

RAIS DKT.JAKAYA MRISHO KIKWETE ATUMA SALAM ZA RAMBIRAMBI ZA MSIBA WA MAMA MZAZI WA KULWA,DOTTO NA NICO MWAIBALE, MWILI WASAFIRISHWA KWENDA MBEYA LEO KWA MAZISHI.


 
 Kulia ni Kulwa na kushoto ni Dotto Mwaibale wakiwa na sura za Majonzi wakati wa Ibada fupi ya Kumuombea Mama yao Mpendwa kabla ya kuanza Safari ya kwenda Mbeya
Wa kwanza Kulia ni Mdogo wao wa Mwisho wa Akina Mwaibale Ambwene  na wa pili kutoka kulia ni Dada yao Mkubwa wa akina Mwaibale  Mary Anyitike ambaye ni Kamishna Mkuu Msaidizi wa Skauti  Shughuli za Vijana Taifa
 
 Mwili wa Marehemu Bi. Twitikege Mlagha Mfumu
mama yao Dotto, Kulwa na Nico Mwaibale ukiwa unaandaliwa tayari kwa kuombewa, Kuagwa na kusafirishwa
 Mchungaji Ephraim Mwakajwanga Akiwa anaongoza Ibada ya Kumuaga Mama mzazi wa Dotto, Kulwa na Nico Mwaibale  Bi. Twitikege Mlagha Mfumu leo katika Hospitali ya Temeke
 Baba Mchungaji akitoa Neno la Kiroho (Mahubiri mafupi) wakati wa kuuaga Mwili wa Marehemu, Katika Mahubiri hayo alisisitiza kuwa Duniani tunapita kila kitu kinabaki hivyo ni vizuri kila mmoja ajiandae  na kuwa mama ametangulia na sisi tunafuata hivyo yatupasa kuwa tayari
 Meneja Mkuu wa Kampuni ya Global Publishers Abdalah Mrisho akitoa salam za Rambi rambi kwa wafiwa ambapo Kulwa Mwaibale anafanyia kazi hapo.
Joachim Mushi akisoma utaratibu na kutoa maelezo mbalimbali wakati wa shughuli za kuuaga mwili wa Marehemu.
 Muwakilishi kutoka Jambo Concept ambao ndio wachapishaji wa Gazeti la Jambo leo ambapo Dotto Mwaibale anafanyia kazi huko Mkurugenzi Beny Kisaka wakitoa salam za Rambi rambi ambapo walitoa mkono wa pole wa kiasi cha Shilingi Laki tano.
 Muwakilishi kutoka Skauti ambako Dada yao Mkubwa wa akina Mwaibale anafanyia kazi akitoa salam za Rambi rambi
 Msemaji wa kwa Niaba ya Familia Noah Mwakalasya  akitoa neno la Shukurani kwa niaba ya wanafamilia na kushukuru kwa moyo waliojitolea kuja kumsindikiza mama yao mpendwa
Dada Mkubwa wa akina Mwaibale  Mary Anyitike ambaye ni Kamishna Mkuu Msaidizi  wa Skauti Shughuli za Vijana Taifa akisoma wasifu wa Marehemu mama yao

No comments:

Post a Comment