Saturday, August 25, 2012

IGALULA KUJENGEWA UJASILI WA KUHOJI KUHUSU KATIIBA MPYA


Na. Mwandishi wetu

SHIRIKA la Mtandao wa Maendelea wilaya ya Uyui mkoani Tabora (UCODEN) linatarajia kutumia shilingi milioni 30 kwa ajili ya kufanya midahalo mbalimbali kwa wananchi ili kuwajengea ujasili wa kutoa maoni yao bila woga, kuhusu madiliko ya katiba mpya.

Hayo yalielezwa na Mwenyekiti wa Shirika hilo, Ally Magoha wakati akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa, kuhusiana na kazi hiyo watakavyoifanya katika kipindi cha mwaka mmoja.

Magoha alisema kwamba lengo kuu la midahalo hiyo ni kuwajengea ujasili na uwezo wananchi ili wakati ukifika wakutoa maoni kwenye tume ya kukusanya maoni ya katiba mpya watoe maoni yao bila ya woga wowote jinsi ambavyo wanataka katiba iwe na muundo upi.

Alieleza kwamba iwapo wananchi watajengewa uwezo huo bila shaka katiba itayoundwa itakuwa na tija zaidi kwa wananchi kuliko ilivyo sasa katiba hiyo haiwapi uhuru wa kufanya mambo yao ya msingi.

“Midahalo hiyo itawajengea ujasili wananchi juu ya kuwahoji  wajumbe wa tume ya kukusanya maoni kuhusu katiba mpya pia nao kutoa maoni wanahitaji katiba hiyo iwe na muundo wa namna gani”alisema Magoha.

Kwa upande wake Mratibu wa Shirika hilo ,Christopher Nyamwanji alisema kuwa lengo lingine la kufanya midahalo hiyo pia ni kukuza mahusiano kati ya wananchi na viongozi wa Serikali.

Nyamwanji pia alisema midahalo  hiyo pia italenga kutoa elimu kwa wananchi hao, kuhusu tabia nchi na mabadiliko ya hali ya hewa ambayo yanapelekea kwa sasa katika baadhi ya mikoa hapa nchini mvua kutonyesha kwa wakati.

Alisema kama uhusiano utakuwawepo baina ya wananchi na viongozi kazi za miradi mablimbali ya maendeleo zitasonga mbele na kwamba midahalo inatarajiwa kufanyika katika vijiji vya Igalula na Goweko wilayani Uyui.

Mwisho.



No comments:

Post a Comment