Thursday, August 23, 2012

NA LUCAS RAPHAELTABORA
 
MAKALA YA MICHEZO.
 
“ili kiwango cha michezo mkoani Tabora kiweze kukua wanatakiwa wapatikane viongozi watakaojitoa kwa hali na mali kwa ajili ya kuendeleza soka la mkoa wa huo.
 
Kusimamia michezo kwa vitendo ,kukuza vipaji na kuwa na mbinu mbadala kwa ajili ya kukuza viwango vya michezo mbalimbali ya mpira wa miguu wa wananwake ,watoto na watu wazima wenye umri wa miaka 20 hadi 25.
 
Bila ya kuchaguliwa kwa na viongozi bora wenye nia ya dhati ya kuendeleza soka la mkoa  huu,  tena wenye uwezo wa kujitolea na kuendeleza michezo mkoani hapa,katu kiwango cha mpira hakitafanikiwa kukua kama ilivyokuwa miaka 20 iliyopita”
 
Kauli hiyo imetolewa na mjumbe wa mkutano mkuu wa TFF kutoka mkoani Tabora, Yussuf Kitumbo katika mahojiano maalum na gazeti hili,amesema kwamba wakati umefika mkoa wa Tabora kuchangua viongozi watakaokuwa tayari kujitolea kwa ajili ya soka la mkoa huu.
 
Amesema kwamba katika kipindi cha kupata viongozi wa wilaya hakikishe wanapata viongozi wanaopenda michezo ili kujenga timu bora ya uongozi katika kukuza kiwango cha soka mkoani Tabora kwa kipindi cha miaka minne ijayo.
 
Amesema kuwa umefika wakati  sasa wa kuhakikisha soka la mkoa linakua ili kuweza kurejea rekodi ya miaka iliyopita ambayo soka linakuwa bora na kuweza kuwatoa wachezaji bora kwenye timu ya mkoa na timu ya Taifa .
 
Kitumbo amesema kwamba kwa kipindi hicho cha kuelekea kwa uchaguzi huo wa TAREFA basi hakuna budi kuhakikisha viongozi wanachaguliwa kuongoza vyama vya michezo wilayani wawe wakereketwa wa michezo kwa maana ya kujitolea kwa hali na mali katika maswala ya michezo .
 
Amesema kwamba bila kuwa na uongozi mzuri katika vyama vya michezo ndio chanzo kikubwa cha kushuka kwa kiwango cha soko mkoani hapa .
 
Amesema kuwa wakipatikana viongozi wazuri katika vyama hivyo na kufanya kazi kama timu ya ushindi, ushindi utapatina kwa ushirikiano bila kuwepo kwa makundi ,soka la Tabora litakuwa na mafanikio yatakayonekana.
 
Amesema kwamba viongozi hao wakipatika na kuongoza vizuri vyama vya soka na chama cha soka mkoa wanaweza kufanya vizuri katika kukuza soka la mkoa wa Tabora.
 
Mjumbe huyo wa mkutano mkuu wa Tff amendelea kusema kwamba dawa ya kukuza soka la mkoa ni kupata viongozi wenye nia ya dhati ya kukuza kiwango cha mpira wa miguu na kukuza vipaji kwa vijana chini nya miaka 13,15 na 17.
 
“Viongozi watakao changuliwa warejeshe imani kwa wadau wasoka ili waweze kujitokeza kuzichangia timu za mkoa zinazoshiriki katika michezo mbalimbali ya ndani na nje ya mkoa huo”amesma kitumbo.
 
Amesema kwamba wadau wa michezo hawaoni nini wachangia kwani uongozi  wa chama cha soka mkoa wa Tabora ,TAREFA umeshindwa kufanya kazi kama timu ili kuweza kuwavuta wadau wa soka ambao wapo tayari kuchangia maendeleo ya soka .

Amesema kwamba lazima viongozi wanaopata nafasi ya kukiendesha chama cha soka mkoa wa Tabora wahakikishe  wanarudiasha imani kwa wadau kwenye mchezo wa mpira wa miguu”
 
Amesema kwamba hilo likifanyika tutakuwa tumeishirikisha jamii nzima kwenye soka ambapo mwisho wa siku watakuwa na uwezo wa kuchangia soka mkoani hapa.
 
Amesema hali hiyo inatokana na viongozi wa mkoa wa cha soka umedhamirie kukuza kiwango cha mpira mkaoni Tabora kuwa timu zake zote zinafanya vizuri katika mashindano mbalimbali.
 
Kitumbo amesema kwamba chama chochote cha  soka kama akina mipango madhubuti ya kuendeleza soka ni lazimakitakuwa akina dira wale mwelekeo wa badaye , chama kiwe na fedha kwa ajili ya kuzisaidia timu ambazo zinashiriki katika mashindano mbalimbali.
 
Akizungumzia swala la vyama kukosa mipango na ukosefu wa fedha na kushindwa  kuzisaidia timu zinashirikia katika michezo mbalimbali amesema tatizo hilo linasababishwa na viongozi kutojitoa katika kukuza soka la sehemu husika na kushindwa kupandisha hata daraja, hawana mipango endelevu ya michezo.
 
Amesema kuwa iwapo cha cha soka cha sehemu husika kikiwa na mikakati madhubuti ya kupata fedha na kiaminika akiwezi kushindwa kukosa fedha kwa ajili ya kuisaidia timu ambayo inashiriki katika mashindano ndani na nje ya mkoa wa Tabora.
 
Amesema kwamba mkoa wowote upate timu zinashirikia katika ligi daraja la kwanza kama ilivyotokea kwa mkoa wa Tabora huko morogoro,iwapo chama kingikuwa na fedha za kutosha timu hizo zingeweza kufanya vizuri.
 
Amesema ni lazima tuvisaidie vilabu kimkakati kwa maana ya kujipanga lengo likiwa ni kupata timu itakayoshiriki ligi ya voda com na wilaya nazo ziwe na mikakati ya kuhakikisha kupandisha timu daraja Fulani hayo yote ni mikakati ya chama cha soka cha mkoa .
 
“Lakini chama cha soka wilaya na  mkoa hawana mipango endelevu yenye lengo la kukuza kiwango cha soka ”amesema kitumbo .
 
Hata hivyo amesema kwamba mipango mingine ya chama cha soka kwa viongozi wanaotaka nafasi ya kuongoza vyama vya soka kuhakikisha wanasimamia soka la watoto wadogo ili kesho na keshokutwa TAREFA wawe na wachezaji katika vilabu vinavyoshiriki ligi kuu ikiwemo AZAM,YANGA na SIMBA.
 
AIDHA amesema kuwa Tabora kuwepo na kituo cha michezo kwa ajili ya kukuza vipaji vya watoto hasa wanaoshirikia Copa coca cola.kichosimamiwa na chama cha soka mkoa wa Tabora .
 
Haya yote yanaweza kufanikiwa kukuza kiwango cha soka mkoani hapa iwapo wanamichezo wataondokana  na malumbano mbayo yanachangia kwa kiwango kikubwa kudidimiza soka .
 
Licha ya hivyo viongozi kushindwa kuonesha mshikamano wakuendeleza soka la mkoa wa Tabora na kusababaisha hata wadau wa michezo kushindwa kushirikiana na chama hicho kwa kukosa imani na viongozi waliopa madarakani.
 
Wadau mbali mbali wa soka mkoani hapa wamempongeza mjumbe huyo kwa kujitole kuendeleza soka la mkoa huu licha ya kuwepo kwa malumbanao kwa baadhi ya viongozi .
 
Wadau hao wamesema mdau huo wa soka  amekuwa akujitolea kuzichangia timu za Polisi  na Rhino Rangers za mjini hapa ambazo  zinashiriki ligi daraja la kwanza pamoja na timu ya Majimaji ambayo ni bingwa wa mkoa kwa msimu  uliopita.
 
Mwisho


No comments:

Post a Comment