Thursday, August 23, 2012

WAJITOKEZA KUWANIA NAFASI YA MWENYEKITI MKOA NA WILAYAN TABORA

Na Lucas Raphael,Tabora
CCM

Kinyanganyiro cha kuwania nafasi ya wenyeviti wa mkoa na wilaya kimepamba moto baada ya wananchma wa chama cha mapinduzi kujitokeza kuchukua fomu za kuwania nafasi mbalimbali za uongozi wa chama hicho.

Waliojitokeza kuchukua fomu hizo ni wale waliokuwa wakishikilia nafasi zao za uongozi na wengine kujitokeza kwa mara ya kwanza kuwania uongozi wa chama hicho.

Akizungumza na waandishi wa habari katibu msaidizi wa mkoa wa Tabora ,Elia Kimaro alisema kwamba hadi kufikia jana ni mwenyekiti anayemaliza muda wake Hassani Wakasuvi ndiye alikuwa amechukua fomu kwa ajili ya kutetea kiti chake hicho.

Alisema kwamba muda bado hupo hadi angasti 28 mwaka huu ambayo itakuwa ndio siku ya mwisho kuchukua na kurudisha fomu hizo kwa nafasi ya mwenyekiti na wajumbe wa halmashauri kuu ya Taifa (nec)

Katika wilaya za Uyui waliojitokeza kuchukua fomu kuwani nafasi ya mwenyekiti wa wilaya hiyo ni Mussa Ntimizi ,Hamisi Bundala na Abdallla Kazwika ambaye natetea nafasi yake ya kiti.

Katika wilaya Igunga katibu wa wilaya hiyo Mary Maziku aliwataja waliochukua fomu hizo kwa nasafi ya wenyekiti wa wilaya hiyo ni Costa Olomi na Felix Mkunde.

Nzega aliyekuchukua fomui hizo ni Patric Bulubuza pekee hadi leo hiyo sikonge aliyechukua nafasi hiyo fomu za kuwania nafasi ya wenyekiti Abed Malifedha  ambapo kwa Tabora mjini aliyechukua fomu hiyo ni Simon Madolu .

Mwisho

No comments:

Post a Comment