Tuesday, April 15, 2014

NHIF YAKUTANA NA WAKUU WA SHULE ZA SEKONDARI MIKOA YA SHINYANGA,SIMIYU NA TABORA.

Afisa Matekelezo na Uratibu NHIF mkoa wa Tabora Bw.Hema Daniel akizungumza katika mkutano wa Wakuu wa Shule za Sekondari kanda ya Magharibi ambapo aliwataka  wakuu hao kuwahamasisha wanafunzi kujiunga na mfuko wa afya ya Jamii.
Bw.Hema alipata fursa pia ya kujibu maswali ya wakuu hao wa Shule za Sekondari kuhusu changamoto za mfuko huo ambao umeboreshwa na kupanua wigo kwa kuhakikisha kila mwananchi anajiunga na kunufaika na mfuko huo wa afya ya Jamii

Baadhi ya wakuu wa shule za Sekondari  mikoa ya Tabora,Shinyanga na Simiyu wakimsikiliza kwa makini Afisa Matekelezo na Uratibu NHIF mkoa wa Tabora Bw.Hema wakati alipokuwa akizungumza na wakuu hao juu ya mfuko wa Afya ya Jamii.

No comments:

Post a Comment