Tuesday, December 31, 2013

WATU WATATU WAFARIKI DUNIA KWA KULA UYOGA

Na Lucas Raphael,Urambo

 

WATU watatu wamefariki dunia baada ya kula mboga aina ya uyoga unaodhaniwa kuwa na sumu wilayani Urambo mkoani Tabora.

Alizungumza na waandishi wa habari katika hospital ya wilaya ya urambo, Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya hiyo, Dk.Kheri Kagya,alisema kwamba  watu hao walikuwa wanane na walikula ugali kwa mboga aina ya uyoga ambao unadhaniwa kuwa na sumu katika kijijini Igunguli, katika Kata ya Uyogo wilayani humo.

alisema kwamba mmoja wa wazazi katika familia hiyo Makoye Tongele (35) aliamua kuwapeleka Hospitali ya wilaya ya Urambo, watoto Kija Makoye (3) aliyefariki njiani na Wande Mahinge (5) na Mahigi Tongele waliofariki wakipata matibabu katika Hospitali hiyo. 

 
 Dk. Kagya alibainisha kuwa wengine waliokula chakula hicho walisalimika akiwemo Baba wa watoto hao Makoye pamoja na watoto wengine Gimili Makoye(miezi kumi) na Talekwa Mahigi(3) akiwemo pia aliyepika chakula hicho Nyanzobe Mswahili(25).

Dk.Kagya alisema wameshindwa kuchukua sampuli ya chakula hicho kinachohisiwa kuwa na sumu kwa vile kililiwa chote na hata aina ya uyoga wameshindwa kuutambua kwa vile nao ulichumwa wote.

Ameeleza kuwa Nyanzobe aliwaeleza kuwa uyoga aliochuma  porini ulikuwa unafanana na uyoga waliowahi kula na hivyo kukwama kuutambua uyoga huo.

Kamamda wa Polisi Mkoani Tabora,Kamishna Msaidizi wa Polisi Peter Ouma alisema wamepata taarifa za tukio hilo na kusisitiza kwamba wananachi kuwa waangalifu kipindi hiki cha masika kwani uyoga nyingi zinaota kutokana na rutuba zilizopo maeneo mbalimbali kwa ajili ya mvua zinazonyesha mkoani hapa

Hata hivyo aliwataka wananchi wanaopenda mboga aina hiyo kuchukua tahadhari ili wasikutane na mboga aina ya  uyoga wenye sumu kama huo .

mwisho-

No comments:

Post a Comment