Wednesday, March 20, 2013

TUWASA YATOA MSAADA WA MIL.3KATIKA WIKI YA MAJI

 Mkuu wa wilaya ya Tabora Bw.Suleiman Kumchaya akikabidhi mfano wa hundi ya shilingi mil.3 kwa mwalimu mkuu wa shule ya msingi Chemchem kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa darasa katika shule hiyo fedha zilizotolewa na Mamlaka ya maji Safi na Maji taka mjini Tabora Tuwasa wakati wa ufunguzi wa wiki ya maji.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Tuwasa Mchungaji Paul Misigalo akizungumza na wananchi wakati wa wiki ya maji.
 Watumishi wa Tuwasa  Mwanasheria na mhasibu wakijaribu kushauriana jambo katika picha waliokuwa wakiangalia kwenye kamera ya Digital
 Watalaam wa Tuwasa wakisikiliza kwa makini hotuba ya mkuu wa wilaya katika uzinduzi wa wiki ya maji
 Mkuu wa wilaya Bw.Suleiman Kumchaya akizungumza na wananchi katika uzinduzi huo wa wiki ya maji
 Afisa habari wa Tuwasa akimsikiliza kwa  makini mkuu wa wilaya na huku akitafakari namna atakavyowezesha Mamlaka hiyo kujitangaza kwa mwaka huu wa 2013 kwa maana ya uboreshaji wa huduma kwa wananchi.
Kutoka kushoto ni Meya wa manispaa ya Tabora Bw.Ghulam Dewji pamoja na mjumbe wa bodi ya Tuwasa na Mwenyekiti wa UWT mkoa wa Tabora Bi.Mwanne Mchemba.

No comments:

Post a Comment