Wednesday, March 20, 2013

"VIONGOZI WA IGUNGA WALIMDANGANYA RAIS KIKWETE KUHUSU KERO YA MAJI IGUNGA"CHADEMA

 
 Baadhi ya wananchi wa wilaya ya Igunga wakiwa katika mkutano wa hadhara ulioitishwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema kuzungumzia kero ya maji wilayani humo iliyodumu kwa muda mrefu.
 Kiongozi wa Chadema Kamanda Mwita Waitara akizungumza na wakazi wa wilaya ya Igunga ambapo alitumia fursa hiyo kumuomba Rais Kikwete kuliangalia upya suala la kero ya maji wilayani humo ambapo alidai kuwa baadhi ya viongozi ngazi ya wilaya hawakumwambia ukweli Rais Kikwete juu ya kero hiyo ya maji inayoendelea kusumbua wakazi wa Igunga.

 Mkurugenzi wa Chadema anayeshughulikia Bunge na halmashauri Bw.John Mrema akizungumza katika mkutano huo wa hadhara ambao ulihudhuriwa na idadi kubwa ya wakazi wa Igunga.
 Wakazi wa Igunga wakichangamkia kununua kadi za Chadema mara baada ya mkutano huo wa hadhara.
 Mkurugenzi wa Organaizesheni makao makuu ya Chadema Bw.Benson Kigaila naye alipataa fursa ya kuzungumza katika mkutano huo.

No comments:

Post a Comment