Monday, September 23, 2013

HAPPINESS WATIMANYWA NDIYE MLIMBWENDE WA TANZANIA BAADA YA KUTWAA TAJI LA REDD'S MISS TANZANIA

 
Happiness Watimanywa akipungia mkono mara baada ya kutangazwa mshindi wa Taji hilo kwa mwaka huu.Kushoto ni mshindi wa pili, Latifa Mohamed na kulia ni mshindi wa tatu,
HAPPINESS WATIMANYWA | MISS TZ 2013
Warembo wa Redd's Miss Tanzania 2013 wakiwa jukwaani usiku huu wakati wa Onyesho la Taifa la Urembo lililofanyika kwenye Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.
Warembo wa Redd's Miss Tanzania 2013 wakifungua shindano la mwaka huu kwa kuonyesha ufundi wao wa kucheza muziki. Shindano la mwaka huu ambalo limedhaminiwa na kampuni ya vinywaji Tanzania.Tanzania Breweries Limited kupitia kinywaji cha Redds limefanyikia katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar-es-salaam. Jumla ya warembo 30 kutoka mikoa mbalimbali,vyuo nk wameshiriki.
Warembo walioingia hatua ya kumi na tano bora 
Jaji Mkuu wa Shindano la Redd's Miss Tanzania,Dkt. Ramesh Shah akitangaza Warembo walioingia hatua ya tano bora. 
Warembo walioingia hatua ya tano bora,toka shoto ni Happiness Watimanya,Elizabert Peter,Clara Bayo,Lucy Tomeka pamoja na Latifa Mohamed.
Warembo wa Redd's Miss Tanzania 2013 wakipita jukwaani na mavazi ya aina mbali mbali wakati wa Onyesho la Taifa Redd's Miss Tanzania 2013 linalofanyika usiku huu kwenye Ukumbi wa Mlimani City,jijini Dar es Salaam usiku huu. 
Mwanamuziki Mkongwe wa Muziki wa Kizazi kipya hapa nchini,Lady Jay Dee akitoa burudani kwenye Onyesho la Redd's Miss Tanzania 2013,linalofanyika hivi sasa kwenye Ukumbi wa Mlimani City,jijini Dar es Salaam.

Fainali za Miss Tanzania 2013 ndio zinaendelea usiku huu ndani ya Mlimani City jijini Dar es Salaam. Gari ndo hilo hapo Je nani ataingia ndani na kuliendesha? Tusubiri Majaji. Hadi sasa Top 5 ndo ishatajwa.

Wadau wakifuatilia shindano la Redds Miss Tanzania lililomalizika kwa Kumpata Mlimbwende Happyness Watimanywa Kutoka Dodoma
PICHA ZOTE: CATHBERT KAJUNA (Kajunason Blog) NA OTHMAN MICHUZI (Mtaa kwa Mtaa Blog)

No comments:

Post a Comment