Tuesday, September 3, 2013

RASIMU ITAMKE JUU NAFASI ZA UKILISHI KWA WALEMAVU





 NA LUCAS RAPHAEL,URAMBO


SHIRIKISHO la vyama vya watu wenye ulemavu wilayani urambo mkoani Tabora (SHIVYAWATA) limesema kwamba rasmu ya katiba itamke wazi juu ya nafasi za uwakilishi kwa watu wenye ulemavu kuanzia ngazi ya kijijji na mabaraza ya halmashauri .

Kuwepo kwa viti vya upendeleo kwa watu wenye ulemavu katika nafasi za uwakilishi katika mabaraza ya madiwani ili kuweza kupata mtu wakuwasemea walemavu .

Wito huo umetolewa wakati wakuitimisha mabaraza ya katiba wilayani urambo yaliyoanyika katika ukumbi wa Cinema Gik na kufadhiliwa na the foundation civel socerty  kwa muda wa siku tatu.

Wakichangia juu ya rasimu ya katiba mpya Shija Nyanda alisema kwamba walemavu wanatakiwa wapata mwakilishi wao katika sehemu za maamuazi hasa kwenye ngazi wa udiwani ili wapate mtu wakusemea watu wenye ulemavu.

Alisema kwamba uwakilishi huo upate nafasi  tatu za uwakilishi kwa kila baraza la madiwani hivyo itakuwa nafasi  mzuri kwa watu wenye ulemavu kupata mtu wa kuwesemea walemavu hao ndani na je ya mabaraza hayo
.
Wakati huo huo chama cha walemavu wa ngozi (TAS)wilayani urambo wamependekeza kuwepo na baraza moja la mitiani la Jamhuri ya muungano wa Tanzania ili kuwepo na kiwango sawa cha elimu, bara na visiwani.

Kauli hiyo ilitolewa wakati wakuitimisha  mabarza ya katiba kwa asasi na makundi ya watu wenye malengo yanayofanana iliyofanyika katika ukumbi wa  Victoria wilayani humo.

Akichangia mjadala huo wa rasimu ya katiba mpya Mikael Emamnuel alisema kwamba kuwepo kwa baraza moja la mitiahani kutasaidia sana kuwepo kwa kiwango cha elimu kilicho sawa tofauti na sasa .

Alisema kwamba licha ya kuwa na elimu iliyosawa pia mfumo wa elimu nao utakuwa sawa kwa upande zote za nchi hii.

Aidha alisema kwamba swala hilo litapunguza wimbi la wizi wa mitihani na hivyo  uthibiti utakuwepo  kutosha  kwa kila sehemu kulinda kwa umakini mkubwa .



No comments:

Post a Comment