Monday, September 16, 2013

!!LOWASSA AINGIA NGOME YA SITTA,WANANCHI WAMKUBALI KUWA MTETEZI WA WANYONGE!!


Waziri mkuu mstaafu na mbunge wa Jimbo la Monduli Bw.Edward Lowassa akikabidhiwa mkuki kama ishara ya kukabidhiwa majukumu ya kuwa mlezi wa Machifu Tanzania,Kulia ni Mtemi ya Unyanyembe Chifu Msagatti Ngulyati Said Fundikira wakati wa maadhimisho ya kumbukumbu ya Mtemi Isike MwanaKiyungi yaliyofanyika Itetemia  katika ukoo ambao Waziri wa Afrika Mashariki Bw.Samwel Sitta ni ndugu wa karibu.
Mtemi Msagatti akimkabidhi Cheti Bw.Lowassa kama hatua ya kumtunuku kuwa Kiongozi bora anayejali maisha ya wanyonge ambao kimsingi ni watanzania wenzake na kuwa sasa ni Mlezi kamili wa Machifu wa Tanzania.
Bw.Lowassa pamoja na kupokelewa kama Mfalme lakini pia ngoma za Dola ya Wanyanyembe ambazo zilikuwa zikitumbuiza katika Maadhimisho hayo.
  Bw.Lowassa akijaribu kushika Kibuyu cha matambiko kwa kinadada walikuwa wakimuimbia nyimbo za Kinyamwezi
Bw.Lowassa aliweka jiwe la msingi mahali ambako panatakiwa kujengwa mnara wa Ngome ya Mtemi Isike MwanaKiyungi Itetemia Tabora mjini.
.

No comments:

Post a Comment