Sunday, September 29, 2013

MUNDE AWATAKA WANAFUNZI WANAOHITIMU DARASA LA SABA KUEPUKA DAWA ZA KULEVYA NA NGONO!!!

Thursday, September 26, 2013

Mbunge wa vitimaalumu na mjumbe wa NEC CCM akizungumza katika mahafali ya darasa la Saba ya Shule ya msingi Isike Bi.Munde Tambwe ambapo alitumia fursa hiyo kuwataka wanafunzi kujiepusha na matumizi ya dawa za kulevya pamoja na kuepuka vitendo hatarishi vya kujihusisha na masuala ya ngono hatua ambayo pia itawasaidia kuepukana na janga la ukimwi huko mitaani.
Mbunge huyo Bi.Munde alipata fursa ya kukabidhi vyeti kwa wahitimu ikiwa ni ishara kwa wanafunzi hao kukamilisha elimu ya msingi ambayo ndio chanzo cha kuianza safari ya elimu nchini.
Mh.Munde akikabidhi msaada wa shilingi laki tatu kwa mkuu wa Shule hiyo Bw.Charles Kidifu kama sehemu ya mchango wake katika shule hiyo ya Isike inayohitaji fedha kwa ajili ya ukarabati wa baadhi ya madarasa mawili.
Wahitimu wa darasa la Saba Shule ya msingi Isike wakati wa mahafali yaliyofanyika shuleni hapo.
Mh.Munde sambamba na kutoa msaada wa fedha hizo pia alikabidhi Ngoma zinazotumika wakati wa gwaride la Shule kwa wanafunzi,Munde alifanya hivyo ikiwa ni kumbukumbu yake muhimu ya kusomea katika shule hiyo elimu yake ya msingi.

No comments:

Post a Comment