Thursday, January 2, 2014

SERIKALI YA WAAHIDI WACHIMBAJI WADOGO KUWA PATIA ENEO




 NA LUCAS RAPHAELNZEGA

 
SERIKALI imetoa ahadi kwa wachimbaji wadogo katika mgodi mdogo wa dhahabu mwanshina wilayani Nzega mkoani Tabora kuwapatia Reseni ya uchimbaji ikiwa na kuwapatia eneo maalum la kuchimba katika mdogo huo.

Hayo yalisemwa na Naibu waziri wa Nishati
na Madini Steven Masele kuwa serikali imelidhia maombi ya wachimbaji ambao wameibua mgodi mdogo pembezoni mwa mgodi mkubwa wa dhahabu wa Resolute Gorden Pride na kuanza kuendesha shuguli hizo bila kufuata taratibu na sheria za madini.


Kauli hiyo imetolewa baada ya Serikali ya wilaya na ofisi za madini Tabora na shinyanga kusitisha shuguli za uchimbaji wa dhahabu katika mgodi huo mdogo wa mwanshina hali iliyopelekea mgogoro baina ya wachimbaji na serikali.

Naibu huyo mwenye dhamana alisema kuwa serikali itahakikisha wachimbaji wadogo wananufaika na rasilimali za Taifa kutokana na wao kuzilinda kwa muda mrefu hivyo wana wajibu wa kupatiwa kipaumbele katika kupewa maeneo kwa kufuata sheria na taratibu za madini.

Alisema kuwa serikali itahakikisha wawekezaji hao wanazungumza na kufikia muafaka ili wapinishe reseni yao ya umiliki wa eneo hilo ili wachimbaji wadogo waweze kupatiwa resen ndogo itakayo wapatia fursa ya uchimbaji wa kiharali.

Aliwataka viongozi wa serikali,chama pamoja na viongozi wa wachimbaji kushirikiana kwa haraka ilizoezi hilo liweze kukamilika ikiwa na kupatiwa reseni pamoja na wachimbaji waendelee na shuguli za uzalishaji mali.

Naibu waziri Masele aliwaahidi wananchi na wachimbaji kuwa suala hilo atalifanyia uharaka mkubwa ili wachimbaji waendelee na kazi ikiwa na kutatua kero hiyo kwa muda mfupi huku akitumia uzoefu alikuwa nao.

‘’Tutakacho kifanya  tutakaa na wawekezaji hawa na kuwaambia wapindishe umiliki wa eneo hilo ili wachimbaji wapate fursa ya kufanya kazi ikiwa na kuwapatia reseni ndogo ya umiliki harali wa eneo hilo’’alisema Naibu waziri Maselle.

Rais wa shilikisho la wa chimbaji wadogo nchini John Wambura Bina  alimuomba Naibu huyo kulifanyia kazi suala hilo kwa haraka na kuongeza kuwa viongozi wote wa serikali waungane kuhakikisha zoezi hilo linatimia ili wananchi wanufaike na rasilimali zilizopo.

Kwaupande wake Mbunge wa Jimbo la Nzega Dk,Hamis Kigwangalla alimpongeza Naibu waziri huyo kwa kuwaahidi wachimbaji hao kutatua kero hiyo ikiwa na kuwapatia reseni ndogo ya umiliki harali wa eneo hilo.

Baadhi ya wachimbaji wadogo wa eneo hilo Joseph Mbondo,mihambo Seleli,Erasto shila pamoja  na Charles  Yota wakizungumza na waandishi wa habari waliitaka serikali wialayani humo iweze kumuunga mkono waziri huyo katika kuhakikisha kero hiyo inatekelezwa mara moja na wachimbaji waendelee na kazi zao.

Mwisho.



No comments:

Post a Comment