Thursday, January 2, 2014

WACHUNGAJI ZANZIBAR WAMTEMBELEA RAIS MSTAAFU DR. SALMIN AMOUR JUMA


01

Mratibu wa Dua Maalum ya kuiyombea Zanzibar kwenye mkesha wa mwaka mpya Allen Mbaga kutoka kanisa la Tanzania fellowship of churches (TFC) aliesimama kulia akiwatambulisha wachungaji waliofika nyumbani kwa Rais mstaafu wa Zanzibar Dkt Salmin Amour Juma kwa lengo la kumtembele na kumuomea huko Migombani nje kidogo ya Mji wa Zanzibar.
02
Rais mstaafu wa Zanzibar Dkt. Salmin Amour Juma kulia alievaa kofia akiwapa historia ya Bara la Afrika kabla ya ukombozi wachungaji wa Zanzibar walipofika nyumbani kwake kumtembele jana nyumbani kwake Migombani nje kidogo ya Mji wa Zanzibar.
03
Mratibu wa Dua Maalum ya kuliombea Zanzibar Allen Mbaga kutoka kanisa la Tanzania fellowship of churches (TFC) wakati na wenzake wakimkadhi zawadi Rais mstaafu wa Zanzibar Dkt. Salmin Amour Juma walipofika nyumbani kwake Migombani.
04
Wachungaji wakiongozwa na Askofu Fabian Obedi kutoka kanisa la Sentekoste Zanzibar wa tatu kushoto wakimuaga Rais mstaafu wa Zanzibar Dkt. Salmin Amour Juma mara baada ya kumaliza kumuombea nyumbani kwake Migombani Zanzibar Dec 31/2013.(Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar).

No comments:

Post a Comment