Saturday, August 24, 2013

PSI YAHAMASISHA UZAZI WA MPANGO KWA KILA KATA MKOANI TABORA





                        
NA LUCAS RAPHAEL,TABORA
WANANCHI KUTOKA SEHEMU MBALIMBALI MKOANI TABORA WAKIPATA MAELEZO KUTOKA KWA MSIMAMISI WA BANDA LA PSI KWENYE VIWANJA VYA NANENANE MKOANI HAPA JUU YA UZAZI WA MPANGO
HATA WANAFUNZI HAWAKUWA MBALI KWA AJILI YA KUJIFUNZA MASWALA YA UZAZI WA MPANGO NA MAMBO MENGINE KWA AJILI YA MASOMA YA SANYASI

Shirika la Psi mkoa wa Tabora limetoa hamasa kwa wananchi juu ya umuhimu wa uzazi wa mpangona huduma hiyo utolewa bure kwa kina mama wanaotaka huduma hiyo

Huduma hiyo imekuwa ikitolewa kwa kushirikiana na wizara ya afya na ustawi wa jamii mkoani hapa katika zahanati zilizopo katika kata zaote za mahispaa ya Tabora

Akizungumza na watu waliofika katika banda hilo la PSI afisa mhamasishaji maswala ya uzazi wa mpango wa shirika  mkoani Tabora. Haika Msuya alisema  kuwa shirika hilo linafanya kazi kwa kushirikiana na Idara ya afya mkoa katika kutoa huduma hiyo kimkoa yaliyofanyika hivi karibuni katika viwanja vya nanenane mkoani hapa.

Alisema kwamba Katika kutoa huduma hiyo wanatembelea vituo vya afya  mbalimbali kwenye kata zote za mkoa wa Tabora na kutoa huduma hiyo bure  kwa akina mama wanao taka kupanga uzazi.
Afisa huyo aliwashauri pia akina baba waliotembelea banda hilo kwenye maonesho ya nanenane kukaa na wake zao na kupanga nao juu maswala ya uzazi wa mpango maana itawasaidia katika kupanga mambo ya kimaendeleo.

Pamoja na mambo mengine katika maonesho hayo banda la shirika hilo lilikuwa likitoa elimu ya ukimwi juu ya matumizi sahihi ya kondomu pamoja na kutoa elimu juu ya maswala ya uzazi wa mpango.

Katika wiki hiyo ya maonesho ya nanenane shirika hilo la Psi lilikuwa likitoa huduma hiyo bure ya kufunga uzazi kwa muda mrefu kwa njia ya vitanzi na vipandikizi katika zahanati ya Isevya mkoani Tabora.

mwisho

No comments:

Post a Comment