Tuesday, August 6, 2013

WAISLAMU WAPONGEZA MAHUSIANO BAINA YAO NA WAKRISTO TABORA



NA LUCAS RAPHAEL,TABORA
Mjumbe wa halmashauri kuu ya CCM wilaya ya Tabora Bw.Emmanuel Mwakasaka akiongea na waumini wa dini za kikristo na kiislamu katika hafla fupi ya Futari aliyoiandaa ambapo zaidi ya watu 450 walihudhuria katika ukumbi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tabora mjini.
Sheikh mkuu wa mkoa wa Tabora Sheikh Shaaban Salum akizungumza katika hadhara hiyo.
Mjumbe wa halmashauri kuu ya CCM wilaya  ya Tabora Bw.Emmanuel Mwakasaka akijumuika na waumini wa dini ya Kiislamu katika hafla ya Futari hiyo.


Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi  wilaya ya TABORA mjini, Moshi Abdulrahman-Nkonkota amekemea vitendo vya ubaguzi wa dini, ukabila na rangi katika jamii kwani vinahatarisha amani ya nchi.

Amesema suala la ubaguzi wa dini, ukabila na rangi halifai na halitakiwa katika jamii kwa lengo la kuimaisha usalama na amani ya wanajamii.

Moshi alikuwa akizungumza kwenye hafla ya futari iliyoandaliwa na Mjumbe  wa Halmashauri Kuu ya CCM wilaya ya TABORA mjini,  Emmanuel Mwakasaka katika ukumbi wa Chuo cha Utumishi wa Umma, tawi la TABORA.

Kwa upande wake, Sheikh wa mkoa wa TABORA, Sheikh Shaban Salum amempongeza ,Mwakasaka kwa  ushirikiano wake na kuwa karibu na jamii ya kiislamu.

Amesema kitendo chake cha kuwaandalia futari waislamu, kinaoneyesha jinsi alivyo na ushirikiano  wa karibu na mshikamano na jamii ya waislamu.

Naye Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM wilaya ya TABORA mjini, Emmanuel Mwakasaka amesema uamuzi wake wa kufuturisha  waislamu unatokana na jinsi anavyothamini jamii hiyo bila kujali tofauti za dini wala rangi.


 Mwisho

No comments:

Post a Comment