Saturday, August 24, 2013

USIKU WA SERENGETI FIESTA 2013 TABORA MJINI

 
Tamasha la Serengeti Fiesta  2013 katika uwanja wa Aly Hassan Mwinyi mjini Tabora.

Msanii machachari wa muziki wa bongofleva/filamu Shilole akiimba huku akiwa na shabiki wake,huku shangwe na miluzi za mashabiki zikiwa zimetawala kila kona.
Baadhi ya mashabiki waliojitokeza kucheza jukwaani,wakionesha umahiri wao wa kukata nyonga mbele ya umati mkubwa wa washabiki waliojitokeza kwenye tamasha la Serengeti Fiesta 2013 ndani ya uwanja wa Al-Hassan.


Msanii  wa muziki wa Bongo Fleva Kassim Mganga- akiwa jukwaani



Umati wa watu

Diamond na Ney nao walikuwa kivutio kikubwa katika tamasha hilo lililohudhuriwa na Maelfu ya washabiki.


Juma Nature na wenzie
Joh Makini na weusi picha ya chini


Wacheza Show wanaoibuka kwa kasi mkoani  Tabora nao walipata nafasi ya kuonesha ukali na umahiri walionao.

kutoka kundi la Tip Top Connections,Msanii  wa muziki wa kizazi kipya Madee alipanda jukwaani kukonga nyoyo za mashabiki wake katika tamasha la Serengeti Fiesta 2013 Tabora.

Abdul Kiba,msanii wa muziki wa bongofleva akiimba mbele ya umati mkubwa wa wapenzi wa muziki wa kizazi kipya  Tabora waliohudhuria  tamasha la Serengeti Fiesta 2013.
Msanii wa muziki wa kizazi kipya,Neylee akiimba kwa hisia mbele ya baadhi ya wapenzi wa muziki wa kizazi kipya waliohudhuria tamasha la Serengeti Fiesta 2013 katika uwanja wa Aly Hassan Mwinyi Tabora.

Msanii wa muziki wa kizazi kipya,Linah akiendelea kuwapatia burudani maelfu ya watu waliofurika katika show hiyo ya Fiesta.
  Msanii Amin  akiwa jukwaani wakati wa show hiyo kubwa ya Serengeti Fiesta  2013 mkoani Tabora,
Mmoja kati ya wasanii  wa  muziki wa kizazi kipya anayefahamika kama Baba Levo ambaye alipata fursa ya kupanda jukwaani kutoa burudani katika tamasha la Serengeti  Fiesta 2013 lililofanyika uwanja wa Aly Hassan  Mwinyi mjini Tabora.
Wakali wa kudansi kutoka THT,wakijulikana kwa jina la Makomanda wakionesha umahiri wao wa kucheza jukwaani usiku wa tamasha la Serengeti Fiesta 2013.

Christian Bella akiwaimbisha mashabiki wa muziki wa dansi  kwenye tamasha la Serengeti Fiesta,liinalofanyika katika uwanja wa Al-Hassan Mwinyi.

Msanii wa muziki wa bongofleva,Rachael akicheza jukwaani na mmoja wa madensa wake,huku mashabiki wake wakipiga mayowe ya shangwe.


Wadau wa Muziki wa Dansi mkoani Tabora Eddy Ngwasuma akiwa na Christian Bela wakati wa tamasha hilo la Serengeti Fiesta 2013.

Wadau wa TABORALEOhabari.COM nao hawakubaki nyuma


No comments:

Post a Comment