Wednesday, February 6, 2013

DIWANI MBARONI KWA WIZI WA MAHINDI



NA LUCAS RAPHAEL,NZEGA
 
Diwani  wa Kata ya Mwamala  wilaya ya nzega mkoani Tabora Hamis Lubunga  Shomali anashikiliwa na jeshi la Polis kwa  tuhuma za ubadhirifu wa zaidi ya gunia  39 za mahindi ya msada yaliyotowa kwa ajili ya watu waliopata tatiza la njaa.

Hayo yalisemwa na Mkuu wa Wilaya ya Nzega Bituni Msangi kuwa viongozi hao wanakabiliwa na tuhuma hizo za wizi wa mahindi kwa gunia 39 za kata ya mwamala ambapo mahindi hayo yalipotea.

Msangi akizungumza na gazeti hili jana alisema kuwa tukio hilo lilitokea 29 January mwaka huu na taarifa hizo kufika ofiosni kwake ziliwasilishwa na wananchi wasamalia wema juzi.

Alisema kuwa wananchi hao ambao majina yao yamehifadhiwa walitoa taarifa hiyo na hatua kali za ufuatiliaji ulianza katika kata hiyo ya mwamala ambapo uchunguzi wa awari ulibani kuwa viongozi hao akiwepo na diwani wa kata hiyo aliyetambulika kwa jina la Hamis Lubunga Shomali wanatuhumiwa kuhusika na ubadhilifu huo.

Akitaja majina nya watuhumiwa hao kuwani Diwani wa Kata hiyo Hamis lubunga Shomali,Mtendaji wa kijiji Saidi Madua Saidi,mwenyekiti wa kijiji Amosi Wambura pamoja na mlinzi aliyefahamika kwa jina moja la Mashaka.

Alisema kuwa watuhumiwa wengine wanao tafutwa kuhusika na tukio hilo kuwa ni kaim mtendaji wa kijiji Nseka Munete,mlinzi mwingine Wambura mwita pamoja na Dereva wa roli hilo jina lake halikufahamika.

Mkuu huyo alili ambia gazeti hili kuwa kata hiyo ilipaswa kupokea magunia 193 sawa na tani 18 hata hivyo magunia ya awari yaliyo pelekwa yalikuwa magunia 130 ambapo magunia hayo yalipo hesabiwi hayo  na kamati ya ulinzi na u8salama ya wilaya walikuta magunia 91.

Msangi alisema kuwa mahindi hayo hayakupokelewa na kamati ya maafa haikupata taarifa kuwa mahindi yamefika na kuongeza kuwa viongozi hao hawapaswi kupokea mahin di badala yake wao nikuwa waangalizi.

Aliongeza kuwa uchunguzi unaendelea ilikubaini mahindi yaliyo potea na kuwapata washiriki wengine ambao watakao bainika kuhusika na ub adhilifu huo wa mahindi ya m saada.

Aliwataka wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa vion gozi wa wilaya pal,e wanapo kuwa na mashakla ya utekelezaji wa maihindi hayo pamoja na kuwahim iza viongozi wa ngazi za kata na vijiji kutambua wajibu wao.

Kaimu Mkurugenzi  Mtendaji wa Halmashauri hiyo Rozalia Magoti alisema kuwa kamati za maafa zigawe mahin di hayo huku viongozi wa kata na vijiji wasimamie zoezi hilo.

Alisema kuwa viongozi hao wanapaswa kutopa taarifa za kila siku za ugawaji wa mahindi hao wa klila siku ikiwa na kugawa mahindi hayo kwa uangalifu zaidi ili zoezi hilo lifanikiwe.

Magoti amewataka wananchi kutoa ushirikiano wa kutosha katika kutoa taarifa hizo na kutoa ushirikiano kwa vion gozi wa kata na vijiji,aliongeza kuwa uchunguzi wa jeshi la polis unaendelea ili kupata ukweli zaidi katika suala hilo.

Mwisho.

No comments:

Post a Comment