Thursday, June 20, 2013

KADA WA CCM EMMANUEL MWAKASAKA AOKOA MAISHA YA MWANACHAMA WA CHADEMA


Mwanachama wa Chadema  Bi.Esther Moses  Ngoho mkazi wa kata ya Kakola manispaa ya Tabora ambaye amepatiwa msaada wa matibabu  na Kada wa CCM Bw.Emmanuel Mwakasaka ambaye alisema yuko tayari kumsaidia mama huyu ambapo aliweka ahadi ya kumpeleka katika hospitali yoyote duniani ilimradi aweze kupona magonjwa yanayomsumbua ambayo yamesababisha hali yake kuwa mbaya zaidi.
Baada ya Kada huyo wa CCM Emmanuel Mwakasaka  kuonesha moyo wa uzalendo wa kuwasaidia wananchi baadhi ya viongozi wa Chadema kata ya Kakola walivutika na kuamua kujiunga na CCM na wengine walidiriki kurejesha hata bendera za Chadema pamoja na kadi za Chama hicho.
Mmoja kati ya waliokuwa viongozi wa Chadema wakikabidhi bendera na kadi zao na kujiunga na CCM.
Mwenyekiti wa jumuiya ya Umoja wa vijana wa CCM wilaya ya Tabora mjini akionesha bendera ya Chadema iliyorudishwa na viongozi wa Chadema.


No comments:

Post a Comment