Sunday, June 2, 2013

WAKULIMA WA TUMBAKU WAONDOLEWA HOFU RC TABORA



 NA LUCAS RAPHAEL,TABORA

Serikali imewataka wakulima wa Tumbaku mkoani Tabora kuacha kutorosha Tumbaku nje ya mkoa huo na kuiuza katika masoko maalum ya maeneo yaokwani hawatakwatwa fedha zao kwa mwaka huu na mabenki yanayovidai vyama vya msingi.

Mkuu wa mkoa wa Tabora ,Fatuma Mwassa, ametoa kauli hiyo alipokwenda kutembelea maghala ya kuhifadhia Tumbaku eneo la Kiloleni mjini Tabora, ikiwa ni kuwatoa hofu wakulima wa zao hilo wanaohofia kukatwa fedha nyingi na taasisi za fedha.

Alisema mgogoro baina ya taasisi za fedha na vyama vya msingi vya wakulima wa Tumbaku hautawahusu wakulima hao kwa sasa wapeleke zao hilo katika masoko yao kwa kupitia vyama vyao vya msingi.

Akifafanua mkuu wa mkoa amesema kwamba serikali imweka utaratibu utakaowezesha taasisi za fedha na vyama vya msingi kuzungumza na kufikia muafaka bila ya kuwakata wakulima fedha zao halali zinazotokana na malipo ya Tumbaku.

Mwassa, aliwataka wakulima wa Tumbaku kutohofu kuuza Tumbaku katika masoko maalum yaliyopangwa na kuacha kutorosha Tumbaku na kuiuza nje ya mkoa huo.

Alisema hivi karibuni baadhi ya wakulima wa Tumbaku katika wilaya za mkoa wa Tabora wameanza kutorosha Tumbaku nje ya mkoa huo kwa kuhofia kuhusishwa na makato yanayotokana mgogoro wa madeni baina ya taasisi za fedha na vyama vya msingi vinavyowawakilisha katika mauzo na mikopo ya pembejeo.

Jambo hilo limepelekea wa kulima wengi kushindwa kupeleka Tumbaku yao sokoni hadi hapo hali itakapotengemaa na hivyo kuleta sinto fahamu ya biashara ya zao hilo mwaka huu.

Mwisho.


No comments:

Post a Comment