Sunday, June 30, 2013

MKUTANO WA KWANZA WA CG FM RADIO UKIJADILI UZALISHAJI WA VIPINDI VIPYA VYA KIJAMII


Mkutano wa kwanza wa wadau wa CG FM Radio unaendelea katika ukumbi wa Kalindimya -Moravian hostel Tabora ukiwa na lengo la kujadili juu ya uanzishwaji wa vipindi vipya vya kijamii vya Nufaika na Fumbuka.Vipindi hivi vya kijamii vinatarajiwa kuanza kurushwa hivi karibuni kupitia CG FM Radio.Mkutano umehudhuriwa na wadau mbalimbali kutoka asasi za kiraia,vyama vya ushirika na makampuni mbalimbali

MKURUGENZI WA 89.5 CG FM RADIO BW.CHARSE GEORGE
MENEJA WA 89.5 CG FM RADIOBW. TITUS PHILIPOSAMADA MADUHU | MSHAURI WA VIPINDI KATIKA KITUO CHA MATANGAZO CHA 89.5 CG FM RADIO CHA MKOANI TABORA AKITO MAWASILISHOYAKEYALIYOTOA MWONGOZO WA NINI KIMEWAKUTANISHA WADAU MBALIMBALI MKOANI HAPO TABORA
WADAU WAALIKWAWADAU WAALIKWA
wazee wa mitambo

Meneja wa mamlaka ya haliya hewa Tabora na Mpanda
 Wadau wakisikiliza kwa umakini
 Meneja wa mamlaka ya hali ya hewa akitumia mchoro kuelezea hoja
 Ibrahim Haruna-Mtangazaji na muandaaji wa kipindi cha FUMBUKA | Akikitambulisha kipindi hicho kipya.
(PICHA NA Aloy-Son-Blog)
-------------------------------
CG FM RADIO IMEKWISHA ONESHA KIPINDI KIPYA CHA NUFAIKA KITAKACHOLENGA KUJIHUSISHA NA MAMBO YA WAKULIMA KWA KUWAPA ELIMU, UTOAJI TAARIFA ZA HALI ZA HEWA, KUSHIRIKISHA WATAALAMU NA WADAU WAKIWEMO WAKULIMA WENYEWE KUJADILI MAMBO YAHUSUYO KILIMO KWA MANUFAA, TAARIFA ZAAIDI ZITATOLEWA KUHUSU BEI NA MASOKO, TAARIFA ZA TAFITI ZA KILIMO.
-----------------------------------------------------------------
MAWASILISHO YA WADAU
====================================
MKUU WA CHUO CHA KILIMO CHA TUMBI
  • Aina mpya ya mpunga iitwayo AMKA/NERICA- Mradi wa Wajapani
  • Kilimo SHADIDI (Mazao maradufu
MRATIBU WA KILIMO MIRADI VIIJIJI VYA MILENIA-MBOLA
  • Kanuni bora za kilimo
  • Matumizi sahihi ya mbolea
  • Ufuatiliaji na ukaguzi wa miradi ya kilimo
  • Mikopo naafuu kwa mkulima
  • Usisitizaji wa mbegu stahimilifu za maeneo ya Tabora.
MENEJA WA MAMLAKA YA HALI YA HEWA TABORA NA MPANDA.
  • Upimwaji wa hali ya hewa na uwasilishaji wake kwa jamii kupitia vyombo vya habari
  • Matumizi ya hali ya hewa kwenye kilimo, usafirishaji, maji, nguvu za uzalishaji, utalii.
  • Utoaji wa taarifa za hali za hewa kwa misimu (siku 10 na kuendelea) 
  • Umuhimu wa hali ya hewa kwa kilimo (utambuzi wa udongo n.k)
  • Madhara ya hali ya hewa- ukame, migogoro ya wafugaji na wakulima, ugomvi wa maji, mafuriko,n.k
MUWAKILISHI WA CHUO CHA ARDHI
  • Umuhimu wa sheria za usimamizi na matumizi bora ya aridhi
  • Kujua taratibu za kisheria ya aridhi zilivyo na mamlaka zake
  • Mpango wa matumizi bora ya aridhi na faida zake.
  • Hati za haki miliki za aridhikama zakimila na nyinginezo.
MUWAKILISHI CHUO CHA NYUKI-TABORA
  • Umuhimu wa nyuki kiuchumi na kibaolojia.
  • Teknolojia ya ufugaji nyuki na tafiti.
  • Ubora wa asali na mabadiliko ya mbinu zaufugaji nyuki kupitia teknonojia.
  • Mbinu bora za kisasa katika uvunaji asali (Teknolojia Mwafaka).
  • Zana na aina zake za uvunaji asali (Gun-boot, Kofia,groves n.k)
  • Faida za ufugaji nyuk
  • Umuhimu wa mimea kwa nyuki

MAWASILISHO YA WADAU YALIKUWA YAKILENGA UPATIKANAJI WA NAMNA UBORESHWAJI WA VIPINDI VIPYA VIMLENGAVYO HASA MKULIMA WOTE NA WAFUGAJI KWA KUTOA MWANGA NA MWELEKEO HATA PIA KATIKA KUSHIRIKIANA KUIKOMBOA JAMII YA WANATABORA KWA WAO KUUONA UMUHIMU WA KITUO CHA RADIO KWA MANUFAA YAO.

No comments:

Post a Comment