Sunday, July 7, 2013

PAMBA YA KUUZWA KILO MMOJA TSH,700 BEI YA KUANZIA



NA LUCAS RAPHAEL,NZEGA


MSIMU wa ununuzi wa zao la pamba umezinduliwa Rasmi katika kijiji cha Mbogwe kata ya Mbongwe wilayani Nzega Mkoani Tabora huku  bei ya kuanzia kwa kilo moja ya pamba ikiwa ni shilingi 700 kwa msimu wa mwaka 2013/2014.

Akizindua msimu huo Mkuu wa Mkoa wa Tabora Fatuma Mwasa alisema kuwa bei hiyo ya shilingi 700 ni bei ya kuanzia na mategemeo yake itazidi kupanda siku hadi siku kutokana na zao hilo kuwa chache kwa msimu huu wa mavuno.

Alisema kuwa makampuni ya ununuzi wa zao hilo la pamba yatashindana kuinunua pamba hiyo ambapo bei hiyo itabadilika kwa manufaa ya mkulima ilikuweza kumpatia faida.

Mkuu huyo alisema kuwa ilikuweza kudhibiti bei ya pamba kuwa na masirahi kwa wakulima serikali inatarajia kufufua viwanda vya nyuzi na kuimalisha viwanda vya nguo pamoja na kuanzisha viwanda vingine ili pamba hiyo iweze kununuliwa hapa nchini kwa bei itakayo mnufaisha mkulima.

Aliwataka wakulima kuongeza tija ya kulima zao hilo hapa nchini ambalo halina uhalibifu wa mazingira kama baadhi ya mazao ya kibiashara na kuongeza kuwa serikali imejipanga kuhakikisha wakulima wanapata pembejeo za zao hilo kwa muda muafaka ilikuweza kuendana na kalenda za kilimo hicho.

Aliwataka maofisa ugani kuhakikisha wanafanya kazi kwa kujituma ikiwa na kuandaa mashamba darasa ya wakulima ambayo yataweza kutoa mwanga kwa wakulima katika kulima pamba kwa kufuata taratibu za zao hilo.

Kwaupande wake Mwenyekiti wa Bodi ya pamba Taifa Dkt,Buluma karidushi alisema kuwa bei ya pamba inatokana na soko la Dunia hata hivyo alisema kuwa jitihada kubwa zilifanyika hadi kufika bei hiyo.

Alisema kuwa kutokana na tamko la serikali la kufungua viwanda vya nyuzi litaweza kusaidia kuongeza bei hiyo ya pamba ambayo itaweza kumfidia mkulima wa zao hilo.

Alisema kuwa uzalishaji wa pamba mwaka 2012 ulikuwa mkubwa ambapo zaidi ya tani 3.5million zilizalishwa kitaifa huku mwaka 2013 uzalishaji umeshuka zaidi hadi kufikia tani zaidi ya 2.5 million.

Mwenyekiti huyo akizungumzia changamoto za kushuka kwa uzalishaji wa zao hilo kuwa ni pamoja na sehemu nyingi kuwa na mafuriko huku sehem nyingine ikiwa na ukame mkubwa.

Alisema sabab u nyingine ya kushuka ni upatikanaji wa pembejeo ulikuwa hafifu ambao ulitumia mfumo wa stakabadhi gharani pamoja na kushuka kwa bei ambapo wakulima wengi walikata tama.

Akitoa tahadhari kwa wakulima kuwa makini na matapeli dhidi ya pesa bandia ambaopo katika msimu huu matapeli hayo huingilia biashara hiyo na kujipatia mali kwa njia ya udanganyifu.

Hata hivyo aliwatoa hofu wakulima hao kuwa vyombo vya Dora vimejipanga kukabiliana na waharifu hao kwanyakati mbalimbali ilikuhakikisha wakulima wana uza mazao yao kwa usalama.

Wakizungumza kwanyakati mbalimbali baadhi ya wakulima wa zao hilo walisema kuwa bei hiyo ya shilingi 700  bado haijalidhisha kutokana na gharama zauendeshaji wa kilimo na kuiomba serikali iweke mikakati mikubwa ya kuwaangalia wakulima hao.

Joseph kadoshi mkulima mkazi wa kijiji hicho alisema kuwa bei hiyo bado haitoshelezi kulingana na gharama za uendeshaji wa zao hilo na kuongezxa kuwa serikali iongeze bei hiyo ifikie 1000 ili mkulima aweze kunufaika na zao hilo la pamba.

‘’Bei hii ya pamba bado haijaridhisha wakulima nadhani umeona hata walipo tamka ni kias gain wakulima walikaa kimya jibu hilo hawakulidhika na bei hiyo tunaomba bei ifike japo 1000 kwani uendeshaji wa kilimo hiki ni mkubwa sana serikali itusikie’’alisema Joseph kadoshi mkulima wa kijiji hicho.

Mwisho.



No comments:

Post a Comment