Monday, July 22, 2013

WAISLAMU TABORA WAIPONGEZA BENKI YA CRDB KWA KUWA KARIBU NA WANANCHI





NA LUCAS RAPHAEL,TABORA


Sheikh wa mkoa wa Tabora Shaaban Salum akichukua futari  wakati wa hafla fupi iliyoandaliwa na Benk ya CRDB tawi la Tabora ikiwa ni hatua ya kuwa karibu na wananchi wakiwemo wateja wa Benk hiyo.
Hawa ni baadhi ya kinamama wa kiislamu waliojumuika pamoja na wafanyakazi wa CRDB katika hafla hiyo mahususi.
Ilikuwa ni faraja kwa waislamu na wasiowaislamu waliokaribisha na CRDB katika Futari
Baadhi ya waislamu na viongozi wa vyama vya siasa nao walihudhuria.
Viongozi wa dini wakiwa katika meza kuu ya hafla hiyo ya Futari.
Wageni  na wafanyabiashara mjini Tabora nao walihudhuria
Maafisa wa CRDB wakizungumza na msemaji wa waislamu katika hafla hiyo ya Futari.



BENKI ya CRDB imetoa futari kwa waumini wa dini ya kiislamu na wasio waumini wa dini hiyo katika kuwaweka watu wa tofauti pamoja.

Akizungumz akwa niaba ya mkurugenzi mtendaji wa benki hiyo dk charlei kimei,meneja wa mkoa,sydney bakari alisema wameamua kufanya hivyo katika kutimiza wajibu wao kwa jamii

Dk.Kimei aliongeza kuwa Benki yake itaendelea kufanya shughuli za kijamii kwa kushirikiana na Taasisi mbalimbali kusaidia watoto yatima,walemavu,wagonjwa na waliopatwa na majanga mbambali,wakiamini Benki hiyo inatokana na jamii.

Aliongeza kwamba CRDB itaendelea na utaratibu wake wa kutenga sehemu ya faida yake ili kusaidia jamii ambayo ni moja ya sera zake.

katika kujitanua na kuwasogelea wateja wao,itafungua matawi katika wilaya za Urambo na sikonge kabla ya mwisho wa mwaka huu.

Alisema hata Manispaa ya Tabora pia wameboresha huduma kwa kufungua jengo jipya ambalo ni kubwa na la kisasa na huduma zake ni bora zaidi kuliko awali.

kwa uapande wake Shehe wa mkoa wa Tabora,Shaban salum,aliishukuru benki hiyo kwa tendo lake la kutoa futari kwa waumini wa Imani zote akisema ni utaratibu mzuri unaowaweka pamoja watu wa imani zote na kudumisha mshikamano.

Alieelza ni lazima wananchi wawe pamoja na kuwa na imani tofauti kwa lengo la kudumisha amani na kwamna tofauti za imani zisiwatenganishe wananchi.


mwisho

No comments:

Post a Comment