Tuesday, July 16, 2013

PICHA NA MAJINA YA ASKARI 7 WA JESHI LA TANZANIA WALIOFARIKI KWENYE SHAMBULIO LA GHAFLA MJINI DARFUR

 


Majina ya askari saba wa Tanzania waliokufa kwenye shambulio la ghafla mjini Darfur yamepatikana.
Askari hao waliokufa ambao walikuwa kwenye vikosi vya kulinda amani vya Umoja wa Mataifa huko nchini Sudan ni;

  1. Sajenti Shaibu Othuman,
  2. Koplo Oswald Chaula,
  3. Koplo Mohamed Juma,
  4. Koplo Mohamed Chikilizo,
  5. Pte. Rodney Ndunguru,
  6. Pte. Peter Werema 
  7. Pte. Fortunatus Msofe.
Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana kwenye mtandao ni kwamba askari hao walikwenda kujaribu kumwokoa mwenzao (ambaye hakutajwa) ambaye alisemekana kutekwa na vikosi vya waasi nchini humo.

Wakati wakijiandaa, ghafla walizingirwa na askari hao waasi na kisha kushambuliwa kwa risasi hadi kufa.
Haikufahamika hali ya askari huyo ambaye alidaiwa kutekwa kama bado yu hai ama ni miongoni mwa waliokufa.

Miili ya Askaria hao inatarajiwa kuwasili nchi kwa ajili ya maziko siku ya Alhamisi ama Ijumaa
Mungu azilaze roho za askari wetu mahali pema peponi, Amina.

No comments:

Post a Comment